Konakali
JF-Expert Member
- Dec 15, 2009
- 1,533
- 263
Fikiria kuwa wewe una miaka kama mitatu hivi ndani ya ndoa. Ulianza kuwa na mkeo/mmeo kama GF/BF (japo kwa dhamira ya kuja kuwa mke na mume) kwa takribani miezi sita kabla ya kuona. Kwa muda wote huu mlikuwa mkipendana, na hujawahi kupata hisia zilizokupa ushahidi kuwa mwenzio anakula nje. Lakini pamoja na mapishano ya hapa na pale, mliweza kuishi kwa amani kabisa na upendo wa hali ya juu. Lakini siku moja (huku akiomba msamaha, na kuapa kuwa ukweli ndio huo, na kamwe haitatokea tena) akakujulisha kuwa katikati ya kipindi mlipokuwa GF na BF, alipata kukusaliti mara moja tu, na akakutajia mtu ambaye kwa kipindi chote hadi sasa unamfahamu na huishi mahali ambapo yupo accessible kwa mwenzio iwapo wamepania kuendeleza. Ukichukulia kuwa kwa kipindi kama mwaka mmoja sasa alishawahi kukuambia kuwa huyo mtu aliwahi kumtaka, lakini akampiga chini...! Je, ukitafakari ungehisi ukweli ni upi; ni siku moja kweli, au ni affair ya siku kadhaa? Itakuwa ni huyo tu, au huenda wapo na wengine? Kwa siku za mbeleni, utamwamini mwenzio kama mwanzo?