kaburunye
JF-Expert Member
- May 12, 2010
- 672
- 74
Wadau, kwa taarifa za TCU viongozi wengi wametunukiwa PhD feki. Je ile aliyotunukiwa rais wetu JK ni miongoni mwa PhD zilizochakachuliwa? Kama ni hivyo je mkulu atanyang'anywa hiyo "hadhi"? Hii si itakuwa hatari? Kwa wale ambao hawakupata muda wa kupitia magazeti, mnaweza kusoma habari hapa chini.
Viongozi wanatunukiwa PhD feki za heshima-TCU
Friday, 06 August 2010 05:14
Mwandishi Wetu
TUME ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU), imesema shahada mbalimbali za uzamivu za heshima wanazotunukiwa viongozi wengi barani Afrika ikiwamo Tanzania ni batili.
Viongozi wengi waliodaiwa kutunukiwa shahada hizo batili ni watu maarufu kama vile marais, mawaziri, wabunge na viongozi wengine.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa Dar es Salaam jana na Katibu Mtendaji wa TCU, Profesa Mayunga Nkunya katika gazeti moja, ilisema kuwa taasisi yake imeshtushwa na ongezeko na nyendo za taasisi na vyuo vikuu visivyotambuliwa nchini na hata duniani.
Alisema vyuo hivyo ambavyo vimepewa jina la utani "Viwanda vya kutengeneza Digrii au stashahada" vinawadanganya Watanzania kwa kuwatunukuu digrii za uzamivu kama ishara ya heshima katika jamii.
"Katika miaka ya hivi karibuni TCU imebaini ongezeko la tuzo za digrii za uzamivu za heshima yaani, honorary Doctorates (honoris causa) zikitolewa kwa watu wenye haiba na wadhifa mkubwa katika maeneo mengi ya Afrika.
"Hali hii pia inaongezeka kujitokeza kwa kasi nchini, hali hii haishangazi kuona kwamba katika kipindi cha muongo mmoja uliopita hadi sasa watu maarufu wakitunukiwa digrii za aina hii kutoka katika taasisi ambazo kutambuliwa kwake kunatia shaka siyo Tanzania pekee bali hata katika nchi zilizomo taasisi hizo," alisema.
Bw. Nkunya ametaadharisha umma kuwa makini ili kuepusha wasitapeliwe zaidi na taasisi ambazo ni viwanda vya kutengenezea digrii, ambazo nia yao kubwa ni kujipatia fedha au umaarufu kwa nia zisizo halali.
Alisema licha ya taasisi hizo kutunuku shahada bandia za heshima pia zimewatapeli watu wengi wa Tanzania kwa kuwapa shahada, shahada za uzamili na hata za uzamivu bila ya wahusika kufanya kazi yoyote ya kitaaluma inayolingana na matakwa ya kutunukiwa shahada hizo.
"Baadhi ya taasisi hizo zinazotoa digrii hizo zimefika mbali zaidi kwa kudai kuwa eti wanafanya hivyo kwa ajili ya kutoa heshima kwa Bara la Afrika kwa kuwa Waafrika walioleta mafanikio hawaheshimiwi na kuleta mafanikio na kuenziwa ipasavyo ndani ya nchi zao," alisema.
Alisema kwa sababu hiyo pengo hilo lizibwa kwa kupewa tunzo ya shahada ya uzamivu za heshima kwa watu hao kwa walengwa hasa watu maarufu na viongozi, ikiwa ni pamoja na marais, mawaziri na wabunge
XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX
-Kwa walio na taarifa tupeni orodha ya waheshimiwa wenye PhD feki.
Viongozi wanatunukiwa PhD feki za heshima-TCU
Mwandishi Wetu
TUME ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU), imesema shahada mbalimbali za uzamivu za heshima wanazotunukiwa viongozi wengi barani Afrika ikiwamo Tanzania ni batili.
Viongozi wengi waliodaiwa kutunukiwa shahada hizo batili ni watu maarufu kama vile marais, mawaziri, wabunge na viongozi wengine.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa Dar es Salaam jana na Katibu Mtendaji wa TCU, Profesa Mayunga Nkunya katika gazeti moja, ilisema kuwa taasisi yake imeshtushwa na ongezeko na nyendo za taasisi na vyuo vikuu visivyotambuliwa nchini na hata duniani.
Alisema vyuo hivyo ambavyo vimepewa jina la utani "Viwanda vya kutengeneza Digrii au stashahada" vinawadanganya Watanzania kwa kuwatunukuu digrii za uzamivu kama ishara ya heshima katika jamii.
"Katika miaka ya hivi karibuni TCU imebaini ongezeko la tuzo za digrii za uzamivu za heshima yaani, honorary Doctorates (honoris causa) zikitolewa kwa watu wenye haiba na wadhifa mkubwa katika maeneo mengi ya Afrika.
"Hali hii pia inaongezeka kujitokeza kwa kasi nchini, hali hii haishangazi kuona kwamba katika kipindi cha muongo mmoja uliopita hadi sasa watu maarufu wakitunukiwa digrii za aina hii kutoka katika taasisi ambazo kutambuliwa kwake kunatia shaka siyo Tanzania pekee bali hata katika nchi zilizomo taasisi hizo," alisema.
Bw. Nkunya ametaadharisha umma kuwa makini ili kuepusha wasitapeliwe zaidi na taasisi ambazo ni viwanda vya kutengenezea digrii, ambazo nia yao kubwa ni kujipatia fedha au umaarufu kwa nia zisizo halali.
Alisema licha ya taasisi hizo kutunuku shahada bandia za heshima pia zimewatapeli watu wengi wa Tanzania kwa kuwapa shahada, shahada za uzamili na hata za uzamivu bila ya wahusika kufanya kazi yoyote ya kitaaluma inayolingana na matakwa ya kutunukiwa shahada hizo.
"Baadhi ya taasisi hizo zinazotoa digrii hizo zimefika mbali zaidi kwa kudai kuwa eti wanafanya hivyo kwa ajili ya kutoa heshima kwa Bara la Afrika kwa kuwa Waafrika walioleta mafanikio hawaheshimiwi na kuleta mafanikio na kuenziwa ipasavyo ndani ya nchi zao," alisema.
Alisema kwa sababu hiyo pengo hilo lizibwa kwa kupewa tunzo ya shahada ya uzamivu za heshima kwa watu hao kwa walengwa hasa watu maarufu na viongozi, ikiwa ni pamoja na marais, mawaziri na wabunge
XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX
-Kwa walio na taarifa tupeni orodha ya waheshimiwa wenye PhD feki.