Je Cremation Ni Mbaya?!

Kifupi turudi vitabu vya dini vilivyosema hizi gharama za misiba ya sifa tutaiepuka, siku hizi msibani budget mpaka ya mziki ipo dah sad sana.

Nashukuru wazazi wangu kunikuza katika imani ya kiislam na nikifa nizikwe kiislam no kulala kwenye friji, no majeneza, no muziki,no misafara ya magari In Sha Allah
 
Hii tabia ya kuchoma miili moto iendee huko huko walikozoea. Maana utajisikiaje mtoto wako uliempenda anateketezwa kwa moto?! Bora nimtupe aliwe hata na ndege kuliko kumteketeza kwa moto. Hii tabia ikija huku itaongeza uchungu na maumivu kwa wafiwa.
 
Logic yako ni dhaifu sana, kwani ukioza si wadudu wanakukula...je unakuwa hauhisi maumivu? Inabidi tuchomwe tu...maeneo ya kuzikiia yanaisha sasa
 
Reactions: Ctr
Mbona nikifa sijitambui so laia watakalo amua kunistili kwangu poa tu
 
Mimi nachagua cremation, kisha jivu langu walipukutishe tu hewani, nahisi nafsi yangu otakuwa huru zaidi napunga hata hewa. Kitendo cha kufukiwa chini peke yangu kisha naachwa hapo siwezi toka inaniba hisia mbaya, nahisi nitalia sana nikiomba msaada nitolewe ila hamna wa kunisaidia. Ni upweke wa milele.
Cremation kwa tanzania ikatokea mtu kachagua inawezekana?
 
Kabisa ni maamuzi yako ata ukitaka baadhi ya viungo vyako vitolewe
 
Pia ndugu au jamaa zako wakiuona huo mti wanakua kama wamekuona wewe
 
 
 
Lakini mkuu sayansi inatutanabahisha mafuta na gas vinatokana na mabaki ya viumbe hai waliokufa miaka mingi iliyopita, tukichomana Moto itakuwaje dunia ijayo si watakosa wese ....
 
Ukija kwenye issue ya Cremation nahisi sio njia sahihi ya ku-dispose corpes, pia si agizo la Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema wafu wachomwe Moto( maana biblia inasema mavumbi yatairudia nchi na roho itarudi Kwa Mungu aliyoitoa, sijaribu kupinga taratibu na Imani ya mtu yeyote.

Ukiangalia soil composition is compactible to body composition by 99%. Minerals,organic na matter zinazopatina kwenye udongo ndizo zinazopatikana kwny mwili wa binadamu.

Kwahiyo Kwa hitimisho, ardhi ndio sehemu mahususi ya kumuhifadhi mfu, kwakua anarudi kuwa udongo Kwa asilimia zaidi ya tisini. Mengine yote aliyoyafanya yataletwa hukumuni siku Mola wake akimfufua tena.
 

Una uhakika gani kama huwa hawatoi baadhi ya viungo kwa maiti
 
Hata mwili wako ukichomwa haimaanishi ndo umekwepa adhabu ya moto wa jehanamu aka mauti ya pili, uchomwe uzikwe ardhini , adhabu ya siku ya mwisho iko pale pale
 
Kwa wale wasiojua cremation ninini ......ni kuchoma moto mwili wa mfu kulingana na tamaduni husika
Binafsi naipenda kwakuwa tunaipunguzia ardhi kuilisha uozo na uvundo laana na mabalaa

Kwa mtu eliyekutwa na kifo cha asilia (natural causes) cremation inaweza kuwa njia rahisi ya kuzika katika maeneo ambayo makaburi yana gharama kubwa. Ila katika mazingira ya kutatanisha, cremation huweza kuondoa ushahidi ambao ungepatikana baada miaka kupita. Ukifuatilia vipindi vya Foresinc Files, utaona kuwa kuna kesi kadhaa ambapo wahalifu hugunduliwa baada ya kufukua maiti na kuifanyia uchunguzi tena kufikia kun'gamua kuwa walilishwa sumu makusudi.
 
mimi wauchome tu wachimbe shimo waoteshee mgomba jivu liwe mbolea
 
Mimi binafsi nafikiri ni njia nzuri yakuyalinda mazingira,...
Cremation ni njia nzuri sana na inaokoa gharama na kupunguza matumizi mabaya ya ardhi
Unailinda ardhi ikusaidie nini ikiwa utakuwa umekufa
 
Kwa wale wasiojua cremation ninini ......ni kuchoma moto mwili wa mfu kulingana na tamaduni husika
Binafsi naipenda kwakuwa tunaipunguzia ardhi kuilisha uozo na uvundo laana na mabalaa
Hiyo kiroho, kisayansi bora kuzika ardhini
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…