Hakuna kitu cha kijinga nilichowahi kukisikia kama hicho. Hivi fursa zilizokuwepo Tanzania wewe huzioni?
Kila kitu kikubwa na kizuri tunachokiona sasa hivi kuna watu wa sampuli yako wanasema "cha Ridhwan", na mijitu kama wewe mnaamini bila kupima wala kufikiri.
Tanzania ya leo imefunguka na ni land of opportunities, vast opportunities, ukiziona na ukiwa mfatiliaji, unalala masikini unaamka tajiri.
Binafsi nimetumiwa email na taasisi ya funds za Uingereza ambayo inatafuta "projects" za kufanya na pesa zipo tayari tena za Serikali ya Uingereza, haina longo longo wala hiyana, unachotakiwa uwe tu kwenye hizo field walizoainisha.
Nawashangaa sana, jana nimeona kipindi cha
Pasco Mayala kuhusu VETA na nikafurahi sana nilivyoona wanavyojuwa kutumia fursa, kusikia makampuni ya nje yanakuja kusini kwa mambo ya Gas, wameleta mpishi kutoka Europe wamempeleka huko huko Mtwara kuwafundisha wapishi na wanafunzi kupika vyakula ambavyo kwa wale wazungu watahisi kama wako nyumbani na wameshapata kazi ya kuwalisha wazungu wa kampuni za gas.
Fursa kama hizo zipo kibao, uko wapi wewe? umelala doro.