Je, Bunge letu ni Bunge Butu?. Angalia Bunge la Uingereza lenye meno linavyong'ata Serikali. Je, Kuna ubaya tukiiga?

Hizo sababu za katiba, mwenyekiti ni raisi ni nzuri kuzisikia lakini ni kazi gani nyingine itakayokupa marupurupu na mshahara sawa sawa na anaolipwa mbunge wa Tanzania? Tena hapo ni kwavile unajua kusoma na kuandika tu.

Tuache utani.
 
Kwakuwa BREXIT ni swala la free vote mmbunge anapiga kura kutokana na msimamo wake (maana ata wao kuna maswala lazima upige kura kichama) hiyo concession ya bunge kuamua wanataka solution gani kwenye sakata la BREXIT 'prime minister' kaitoa mwenyewe kwa ridhaa yake baada ya plan yake kukataliwa.

Ahadi ya kuachia madaraka pia plan yake ikipitishwa kaitoa mwenyewe, not that its going to work atasingesema ataachia madaraka angepewa tu challenge ya uongozi kutokana na kuboronga kwake.
 
Hili bunge letu la ndio. Wabunge wanasema lolote hata kama ni uongo ilia aonekane yuko upande wa chama. Kila jambo likija kila kitu ni ndioooo..ndioooo
Mambo yakibuma mbeleni wanaanza udai tumehujumiwa wanamtafuta mchawi..



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mazingira ya kisiasa ya nchi yetu hayaruhusu hayo unayotaka tuyaige labda mpaka siku upepo wa kisiasa ubadilike.
 
Wanabodi,
Naomba kuanza na angalizo, hii ni thread ya swali na sio statement.

Jee Bunge Letu Ni Bunge Butu?. Angalia Bunge la Uingereza Lenye Meno Linavyong'ata Serikali. Jee Kuna Ubaya Wowote na sisi Bunge Letu Tukiiga Mazuri ya Mabunge Mengine Katika Kuisimamia Serikali Zao?.

Kumewahi kutolewa tuhuma kadhaa kuhudu udhaifu wa mhimili wetu wa Bunge, hadi kuitwa "Bunge Dhaifu" au "Bunge Butu" kwa hoja kuwa halina meno makali ya kuweza kung'ata Mhimili mmoja wa The Executive, wakati mhimili huo unapokwenda kinyume cha sheria, taratibu na kanuni nikitolea mfano mmoja tuu wa matumizi ya fedha za umma.

Hoja za watoa hoja ni hatua mbali mbali zinazochukuliwa na Bunge, kunyamazia makosa ya the executive.

Kwa vile Bunge letu tunafuata mfumo wa Westiminster wa Uingereza ambao pia ndio unaofutwa na mabunge mengi ya nchi za Jumuiya ya Madola, jee kuna ubaya Bunge letu na Wabunge wetu, wakanoa meno na kuwa makali kama Bunge la Uingereza ambalo ni Bunge lenye meno kweli, ukilinganisha na Bunge letu, mtu unaweza kuliita Bunge letu ni Bunge...(sitaki kuitwa tena Dodoma).

Ripoti ya CAG ya Ukaguzi wa Hesabu za Serikali, itashuka Bungeni Dodoma hivi karibuni, tuifuatilie kuona ripoti hiyo itabaini nini na kulifuatilia Bunge letu litafanya nini.

Natoa wito kwa Wabunge wetu, kufuatilia kwa karibu kinachoendelea kwenye Bunge la Uingereza kwa sasa, ambapo Bunge la nchi ,linaonyesha perliamentary supremacy kwa kuiathibu The Executive, na kura zikitosha, Waziri Mkuu Bi Theresa May ndio safari.

Soma hii
Our cover in Britain dissects a week in which Theresa May, the prime minister, has offered to resign and Parliament has seized control of Brexit—sidelining the executive for the first time in over a century. Sadly, Mrs May’s sacrifice does nothing to solve Britain’s Brexit mess. Her resignation depends on Parliament voting through her deal after two crushing defeats. Even if she succeeds (a very big if), Parliament remains hopelessly divided about Britain’s future relationship with Europe. If her deal fails and Parliament forces its own alternative on her, she could resist. If she goes, the next prime minister’s Brexit plan will have no popular mandate. Brexit remains as radically uncertain as it has ever been.
Source ni The Economist.

Nawatakia Furahi Dei Njema.

Paskali
Paskali kuna kitu umeruka,nacho ni inferiority complex.
Unapewa madaraka lakini huna uhuru na nyadhifa hiyo.Ukileta ngebe wakikuheshimu sana wanakwambia uwapishe yaani ujiuzuru.
Na haya mambo yameanzia pale tu tulipopewa uhuru yameisha ota mizizi.
Hawa wabunge wakina Njeru Kasaka,Kinyondo,Jenerali Ulimwengu mbona walipitisha hoja ya serikali tatu ikapita?Kama si Nyerere kutokea kustaafu kuwakandamiza walikuwa wameishashinda.
Badirisha mazingira leo hii hao wabunge hao hao watacheza premium ligi ya Uingereza.
 
Umeuliza Swali: Je, Bunge letu ni Bunge Butu?.

Jibu: NDIO!

Sababu: Linashindwa Kuisimamia Serikali Ipasavyo Na Hii Ni Kutokana Na Kujawa Na Watu Ambao Wadau Humu Wanapenda Kuwaita "Wachumia Tumbo" Ambao Kwao Priority Ni 'Matumbo' Yao Na Si Maslahi Ya Taifa Kwa Ujumla. Na Hii Inaweza Kuchangiwa Pengine Na Madhaifu Ya Mfumo Unaoweza Kuwapata Viongozi Wanaolifaa Taifa.
 
Hivi Pascal Mayalla uliishawahi kutupa mrejesho wa kilichojiri kwenye mahojiano na Kamati ya Maadili na Haki za Burge? Ni swali mkuu sio statement!
 
Nchi hii ina bunge jina tu lakini bunge lenye kutimiza wajibu wake kwa wananchi hatuna.

Hili bunge la hovyo kazi yake ni kutunga sheria za kuumiza raia wa nchi hii.

Toka Magufuli na ndugai waingie kwenye nafasi zao bunge kazi yake imekuwa ni kutunga sheria zenye kuumiza raia.

Bunge linalopokea amri toka kwa rais ya kushughulikia wapinzani ndani ya bunge ili rais awashughulikie nje ya bunge.

Hili ni bunge la kipuuzi kuwahi kutokea nchi hii.
 
Uwe makini, hivyo viulizo wenzio huwa hawavioni.

Utasikia umelikashifu bunge kwa kuliita butu.!

Na huku kwetu tatizo sio bunge kuwa na meno, tatizo ni katiba ya nchi ndio inalea Madudu yote haya..

Kwetu chama ndio kinamvua ubunge mbunge.

Katiba haijampa mwananchi haki yake kumlinda mwakilishi wake.

Siku bunge likiwa huru labda ndio tutaona mijadala moto na yenye nguvu dhidi ya serikali.
Hatuna bunge sisi zaidi ya wapiga vigelegele wa CCM, ni kama toy la mbwa
 
Kichwa cha hili bandiko kingeondoa maneno mawili yaani JE? ya kwanza na JE? ya pili kingesomeka vizuri na kingeleta maana zaid.
 
Back
Top Bottom