Zanzibar-ASP
JF-Expert Member
- Nov 28, 2013
- 12,151
- 44,071
Kuna kipindi Spika Ndugai iliwahi kusema mule bungeni kuna wavuta bangi balaa, na akashauri ikiwezekana hatua madhubiti zifanyike ili kunusuru ile hali. Bunge likazizima kwa makofi ikiwa ishara kuunga mkono hoja ile.
Juzi juzi, Mbunge Waitara akatoa pendekezo la kuomba ofisi ya spika ifanye haraka kuleta mashine mahsusi wa kuwapima ushoga kwa wabunge. Bunge likazizima kwa makofi ikiwa ishara kuunga mkono hoja!
Siku ya leo, Spika Tulia ameibuka na kusema kuwa, mijadala kadhaa iliyofanyika siku chache zilizopita ndani ya bunge ilikuwa na makosa makubwa ya kikanuni na kisheria na bunge halihusiki nayo. Wabunge na kiti cha spika kilichohusika katika kipindi hicho, kwa kutokujua (umbumbumbu) walifanya hayo kimakosa na Spika akaonya hayo mambo yasiendelee na yasije yakajitokeza tena. Baada ya Spika kusema hayo, wabunge wakapiga makofi kuachiria kuunga mkono hoja!
Nimebaki nimejiuliza haya;
1. Kwenye pendekezo la kudhibiti uvutaji bangi miongoni mwa wabunge, bunge liliunga mkono hoja kwa makofi mengi!
2. Kwenye pendekezo la kuletwa mashine maalum ya kupima ushoga kwa wabunge wote, bunge liliunga mkono hoja kwa makofi mengi!
3. Kwenye pendekezo la kudhibiti umbumbumbu (ujinga) miongoni mwa wabunge, bunge liliunga mkono hoja kwa makofi mengi!
Juzi juzi, Mbunge Waitara akatoa pendekezo la kuomba ofisi ya spika ifanye haraka kuleta mashine mahsusi wa kuwapima ushoga kwa wabunge. Bunge likazizima kwa makofi ikiwa ishara kuunga mkono hoja!
Siku ya leo, Spika Tulia ameibuka na kusema kuwa, mijadala kadhaa iliyofanyika siku chache zilizopita ndani ya bunge ilikuwa na makosa makubwa ya kikanuni na kisheria na bunge halihusiki nayo. Wabunge na kiti cha spika kilichohusika katika kipindi hicho, kwa kutokujua (umbumbumbu) walifanya hayo kimakosa na Spika akaonya hayo mambo yasiendelee na yasije yakajitokeza tena. Baada ya Spika kusema hayo, wabunge wakapiga makofi kuachiria kuunga mkono hoja!
Nimebaki nimejiuliza haya;
1. Kwenye pendekezo la kudhibiti uvutaji bangi miongoni mwa wabunge, bunge liliunga mkono hoja kwa makofi mengi!
2. Kwenye pendekezo la kuletwa mashine maalum ya kupima ushoga kwa wabunge wote, bunge liliunga mkono hoja kwa makofi mengi!
3. Kwenye pendekezo la kudhibiti umbumbumbu (ujinga) miongoni mwa wabunge, bunge liliunga mkono hoja kwa makofi mengi!