Je, bodaboda wapo juu ya sheria za usalama barabarani?

Sir robby

JF-Expert Member
Jun 22, 2022
2,400
4,074
Wadau nawasabahi,

Kama kichwa cha habari kilivyo, nitafurahi sana endapo Waziri wa Mambo ya Ndani Mwenyekiti wa Usalama barabarani Taifa na IGP na Kamishna wa Kikosi cha Usalama barabarani Taifa watalitolea ufafanuzi suala la hawa bodaboda kutokuheshimu Sheria za Usalama barabarani tena kwa makusudi mbele ya Askari wa Usalama barabarani na kusababisha ajali za makusudi ambazo zingeweza kuepukika.

Bodaboda wamekuwa;
1. Hawaheshimi taa za kuongoza vyombo vya usafiri barabarani.

2. Bodaboda wamekuwa wanakatisha popote watakapo hata kama Sheria za Usalama zinakataza.

3. Bodaboda wamekuwa wanabeba abiria zaidi ya 2 tena mbele ya Askari wa Barabarani lakini hawachukuliwi Sheria.

Je, ni kweli bodaboda wapo juu ya Sheria za Usalama Barabarani ndio maana hawachukuliwi hatua? Naamini ingekuwa wanaadhibiwa nadhani hata wingi wa ajali za bodaboda ungepungua kwa kiwango kikubwa lakini ndio kwanza zinaongezeka!

Bodaboda tiini Sheria bila shuruti. Tanzania bila ajali za bodaboda inawezekana.
 
Front page, Hawa wameachwa hata hawakamatwi njoo ARUSHA ukipita wakati wapo mwendo wa kibati unapewa na Tusi hapohapo.
 
Wadau Nawasabahi.
Kama Kichwa cha Habari kilivyo nitafurahi sana Endapo Waziri wa Mambo ya Ndani Mwenyekiti wa Usalama barabarani Taifa na IGP na Kamishna wa Kikosi cha Usalama barabarani Taifa Watalitolea Ufafanuzi Suala la hawa BODABODA kutokuheshimu Sheria za Usalama barabarani tena kwa Makusudi mbele ya Askari wa Usalama barabarani na kusababisha AJALI za MAKUSUDI ambazo zingeweza KUEPUKIKA.
BODABODA wamekuwa
1.Hawaheshimi TAA za Kuongoza Vyombo vya Usafiri barabarani
2.BODABODA wamekuwa wanakatisha popote Watakapo hata kama Sheria za Usalama zinakataza
3.BODABODA wamekuwa wanabeba Abiria zaidi ya 2 tena mbele ya ASKARI wa barabarani lakini Hawachukuliwi Sheria je ni KWELI BODABODA wapo juu ya SHERIA za USALAMA BARABARANI ndio maana HAWACHUKULIWI HATUA?Naamini ingekuwa Wanaadhibiwa nadhani hata Wingi wa AJALI za BODABODA Ungepungua kwa kiwango kikubwa lakini ndio kwanza ZINAONGEZEKA.
BODA BODA TIINI SHERIA BILA SHURUTI
TANZANIA bila Bila AJALI za BODABODA ingewezekana.
Lakini mkuu,ni hawahawa askari wa usalama barabarani wakisimamia sheria vema na kuwabana kisawasawa bodaboda kuna mambo yatajitokeza:-
1-Yatazuka malalamiko ya kuonewa kwa bodaboda/bajaj kutoka kwa wananchi,
2-Wengi wa bodaboda na bajaj wataikimbia kazi hiyo kwa kukosa sifa hasa leseni,
3-Umma kwa wingi utarudi kwenye usafiri wa daladala zenye msongamano na mwendo wa kobe mzee,
4-Vikundi haramu vya uhalifu kurudi mitaani na kuzua rabsha katika jamii,
5-Tatizo la ajira kuongezeka na kuwa mzigo kwa serikali,
6-Uchumi wa familia nyingi zitegemeazo biashara za bodaboda na bajaj kuyumba au kusambaratisha familia hizo

NK NK WAKADHAA!
 
Wamewalea wenyewe, NI aibu kwa Jeshi la polisi. Imagine Tragic Polisi anaongoza magari kwenye junction's then bodaboda au bajaji anakuja pale mbele ya Askari anaangaza angaza na kupita jinsi anavyotaka', wengine wrong site n.k Polisi anatozama tu. Wao sheria no kwa magari tu.
 
Tatizo ni Wanasiasa.
Polisi wakisema wafanye kazi yao, wanasiasa watapingana nao na kusema wanaonea wanyonge.

Siasa ndo chanzo cha ushenzi wote Tanzania
 
Wamewalea wenyewe, NI aibu kwa Jeshi la polisi. Imagine Tragic Polisi anaongoza magari kwenye junction's then bodaboda au bajaji anakuja pale mbele ya Askari anaangaza angaza na kupita jinsi anavyotaka', wengine wrong site n.k Polisi anatozama tu. Wao sheria no kwa magari tu.
Kwa uwingi wa watu na vyombo vya usafiri maeneo kama uliyoyataja,ungeshauri askari aache eneo la kazi awe anawakimbiza hao wavunja sheria?Toa ushauri mkuu.
 
Kuna changamoto nyingi kwa hawa jamaa
Kwanza wakivunja sheria wakisimamishwa hawasimami
Wakikimbizwa na askari wa pikipiki matokeo yake huwa mabaya na mpaka vifo kwa wasiokuwa na hatia

Lingine hata police wakichukua namba wengine hawatii sheria na wengine wanawapoza za kubrashia yanaisha na maisha ya ajali yanaendelea

Kama kweli wana nia ya kumaliza hili tatizo watoe sheria kali kabisa za jela na kama ni faini zisipungue million

Linawezekana kama na police hawatachukua laki 5 ila kama nao watafungwa camera kama police wa majuu basi rushwa itapungua na ajali zitapungua na sheria zitafuatwa

Camera wataziangalia kama zimezimwa imekula kwa huyo police na adhabu ni kutimuliwa kazi
 
Kwa uendeshaji huu lazima hatua zichukuliwe kudhibiti hili. Wenye mamlaka wanalichekea kwa kigezo cha wapiga kura ila ni hatari kwa usalama wa taifa na maendeleo ya nchi huko mbeleni
 

Attachments

  • VID-20230217-WA0056.mp4
    3.7 MB
Back
Top Bottom