Je, Binadamu tuna free will (Hiari)?

Mcqueenen

JF-Expert Member
Nov 2, 2019
6,818
11,542
Nasilsiniz JF üye?

Naomba unisamehe maana kwa haraka haraka hata mimi najishangaa kuuliza hili swali, kwasababu it's a No-brainer right?, Namaanisha ofcourse binadamu sisi sio kama wanyama wanaotawaliwa kwa instincts, sisi tuna free will right?, Maana tokea nianze kujitambua mpaka sasa kila nachofanya nimefanya kwa hiari yangu. nikitaka kunyanyua mkono nanyanyua nikitaka kucheka nacheka. Mimi ndiyo nauendesha huu mwili si ndio?

Sadly, sikuizi mwenzenu nimeanza ku'second guess hayo mawazo baada ya ku'consider hizi factors.

1. Uwepo wa Mungu anayetaka ufuate masharti yake: Uwe mkristo au Muislam, Mungu anataka ufuate masharti yake, kuna mambo unatakiwa kuyafanya na kuna mambo hutakiwi kuyafanya. Kuna zawadi na adhabu kwa watakomfuata au kumpinga. Kitendo cha kuwepo tu adhabu nisipomfuata Mungu kinamaanisha sina hiari/free will katika maisha yangu hapa duniani, maana ningekuwa nayo ningekuwa na uhuru wa kufanya jambo lolote liwe jema au baya bila kuwa na consequences. Ni sawa na mtu akuwekee bunduki kichwani akuambie una uhuru wa kutaja au kutotaja password yako ya benki, ila usipotaja nakuua. Sasa hapo unao huo uhuru?

2. Mazingira: Hapa nazungumzia mazingira yanayonizunguka tangu nizaliwe, ikihusisha vitu kama utamaduni wa jamii inayonizunguka(mfano jinsi ninavyovaa, ninavyoongea, ninayolia msibani, ninavyokula nk. Siwezi kwenda kinyume na utamaduni wa jamii niliyopo. Siwezi kwenda msibani na boxa tu huku nacheka, sina huo uhuru),Sheria inayonitawala (Siwezi kuendesha gari upande wa kulia), Malezi niliyokulia(Kwetu mwanaume Siwezi kusuka nywele nitakataliwa na ukoo), Elimu niliyoijaza kichwani (Elimu naweka mwenyewe kichwani ila ikishakaa yenyewe ndiyo inanitawala na kuniongoza, nilishasoma bailojia kwahyo siwezi kula vyakula vilivyochacha.), Status niliyo nayo katika jamii (Hakimu siwezi kushinda kwenye vijiwe vya kubeti na kulewa gongo),teknolojia, nk. Hivi vyote ni vitu ambavyo vinanipokonya uhuru wangu wa machaguzi. Ndiyo maana ukichukua binadamu waliokulia katika mazingira tofauti lazima watakuwa na tabia tofauti, ina maana hawana uhuru wa hizo tabia bali mazingira ndiyo huwaamulia. Vilevile binadamu waliokulia mazingira yanayofanana huwa na tabia inazofanana (Mf. Kuna tabia zinajulikana za wazaramo,wahaya,wazungu,wachina nk.)

3. Vizingiti vya kibaiolojia: Ninaweza kuwa na uhuru wote ila siwezi kuipinga baiolojia yangu, Siwezi kuacha kula, kulala, kupumua, kujisaidia nk. Pia siwezi kupaa,kubeba gari, kujifupisha, kujirefusha, kula viwembe, kupiga bao 10 nk.

Hivyo kwasababu lazima nile kuna vitu lazima nifanye ili nile (mf. kuomba, kufanya kazi, kubeti, kuiba nk.) na sina hiari katika hilo.

4. Brain Chemistry: Neuroscientists bado wanaendelea kugundua mchango mkubwa wa kemikali mbalimbali katika ubongo ambazo zinaweza kutengeneza,kubadili au kuondoa tabia kwa mnyama. Ubongo wa binadamu umeundwa kurespond to chemicals mbalimbal ndani yake. Mfano wa hizi chemicals ni Dopamine, Adrenaline, Oxytocin, Serotonin, Testosterone, Oestrogen na zingine nyingi. Viwango vya hizi chemicals vinaathiri tabia ya mtu. Mfano Dopamine inatoka pale unapopata raha, kwahyo Dopamine husababisha mtu kufanya vitu ambavyo vinampa raha (kama Chaputa, kubeti, ngono, Kutumia mihadarati, kucheza mpira nk. nk.) Ukiondolewa dopamine unaweza ukafa maana unaweza ukaacha hata kula kwasababu huoni raha yake. Vilevile ikizidishwa dopamine kwenye ubongo unaweza ukafanya kile kitu kinachokuletea dopamine mpaka ukafa (mfano unaweza ukaacha kula ili utumie cocaine)

Kuna panya aliwekewa cocaine na chakula, ila akaacha chakula ili ale cocaine mpaka akafa kwa njaa.
Mfano mwingine ni hizi kemikali za kijinsia kama Oestrogen na Testosterone ndio hufanya mwanaume au mwanamke kuwa na tabia za kiume au kike anapobarehe. Oestrogen inapozalishwa mda wa hedhi/mimbA hubadili tabia ya mwanamke. Ukiachana na hizi kemikali natural kwenye ubongo, hata hizi artificial tunazokula binadamu kama bangi, pombe, Cocaine Nk. zinaonyesha jinsi ambavyo kemikali kwenye ubongo huathiri tabia ya mtu. Sasa kama tabia zetu zinaathiriwa na viwango vya kemikali kwenye ubongo wetu, utasemaje kuwa tuna free will?
 
5. Brain Wiring: Neuroscientists wamegundua kuwa ubongo unafanya kazi kama kifaa cha umeme kupitia miunganiko maalumu ya neurones. Hizi seli ndani ya ubongo (Neurones) zimeungana na kutengeneza pathways (circuits) tofauti tofauti. Kuna neurones zaidi ya billioni 100 kwenye ubongo na kila neurone inaweza kuungana na neurones zingine jirani mpaka 1000. Kwahyo possible combinations ni ngapi hapo wanamahesabu?

Hiyo ni nje ya point, lakini point ni kuwa hizi circuits ndogondogo kwenye ubongo ndio hufanya specific functions,
iwe ni circuit kwa ajili ya kucontrol mapigo ya moyo au circuit kwa ajili ya kunyanyua kidole gumba au circuit kwa ajili ya kusema I love you (Nasimplify lakini its a lil bit complex than that na bado hatujui vingi kuhusu hili).
Ndiomaana huwa ngumu kubadili tabia ya mtu kwa siku moja (Mfano introvert kuwa extrovert,mvivu kuwa mchapakazi au Katili kuwa mpole nk.) kwasababu tayari circuits zinazotengeneza hizo tabia zinakuwa tayari zimeshajitengeneza,ili ubadili inabidi uache kutumia hizi circuits na uanze kutumia zingine zenye tabia mbadala. ambayo huwa ngumu and near impossible kuzifuta circuit zilizokwisha kujitengeneza.

Sasa kama tabia zetu,matendo yetu,mawazo yetu ni miunganiko ya circuits ndani ya ubongo ambazo huwezi kuzicontrol, utasemaje una free will?

Kuna vifaa vinavyoweza kupima activity ya ubongo na imeshagundulika experimentally kuwa kabla conscious mind yako haijafanya maamuzi yoyote mf. kunyanyua kidole, subconcsious mind inakuwa tayari imeshaamua..Kuna vifaa vinaweza kupima hizi neuurones za subconscious na wanasayansi wanaweza kuvitumia kutabiri utafanya nini milliseconds kabla wewe mwenyewe hujaamua utafanya nini. Na wanakuwa sahihi 99% of the time.

6. Determinism: Hii ni imani kuwa ulimwengu unatabirika, yani hali ya ulimwengu ulivyo sekunde hii ndio itakayoathiri na kuleteleza hali ya utakavyokuwa baadae. Maana yake ukijua hali ya kila kitu kilivyo sasa basi unaweza kutabiri kitakuwaje baadae. Mfano Ukijua gari lina spidi gani kuelekea upande fulani na ukajua acceleration yake, basi unaweza kutabiri kwa uhakika kuwa baada ya muda fulani litakuwa wapi na litakuwa na spidi gani. Samia leo ni raisi inamaana kesho samia atakuwa raisi.

Sasa kama imani hii iko sahihi, ulimwengu ni determined, inamaana tunaishi kwenye Movie. Ukiwa unaangalia movie ukafika katikati ukapause, wale waigizaji mule ndani hawajui movie itaishaje na hawawezi kubadili movie yani inabidi iendelee tu kama ilivyokwisha andaliwa. ingawa wanapoigiza ni kama vile kila wanaloanya wanafanya kwa hiari yao. Unaweza kukuta katikati ya movie anafanya kitu halafu anakuja kukijutia baadae.

Huenda hata haya maisha yameshapangwa sema tu sisi hatujui.
Yani ukiamua ucheke sasa, sio wewe uliyeamua ila ulikuwa umepangiwa kucheka muda huu. Na nadhani wanaoamini kuwa Mungu anajua kesho yetu, inabidi waamini katika hii determinism.
Sasa kama ulimwengu ni determined na kila kitu kimeshapangwa, je sisi tuna free will?

7. Indeterminism: Hii imani ni kinyume cha hiyo deteminism, yaani kwamba ulimwengu hautabiriki ila kila kitu kinatokea randomly by chance. Ulimwengu hauna end-goal au lengo lolote. maisha yanaplay out by chance tu kulingana na hiyo scenario/case husika. Mfano, Samia kuwa raisi haikuwa imepangwa ila ilitokea tu randomly by chance baada ya mkuu wake kufariki. Hakuna mpango au anayepanga chochote ila ni bahati u ndio inatawala ulimwengu...Sasa hata kama ukiamini hii indeterminism, bado tu hakuna free will maana kumbe sio hiari yetu tena bali ni bahati/chance/randomness ndio inaendesha maisha yetu. Sisi hatuna uhuru wa kufanya lolote kwenye haya maisha maana kila kitu kinatokea by chance.

Mimi bado nakuna kichwa sijapata jibu kama binadamu tuna free will au la!
Vipi wewe mkuu, unadhani binadamu tuna free will? Kwanini?
Uhakika Bro
 
Free will tunayo, Mungu ametupa free choice ya kutenda mema au maovu, ila ni choice with consequences...Kama ilivyo kwenda shule ni choice ya mtu ila asipoenda kuna consquence kama kukosa ajira.
 
You have no free will. Why do you end up doing things that you sweared to yourself that you will never do them again?
Why wont you will yourself to be good?
Why wont you will yourself to have perfect peace?
You have no free will. You are either influenced by good or evil
When you realize this, it makes you give up the fight and let God remove evil from your heart.
As long as you believe you have free will you will never overcome.
 
Mada fikirishi sana.

Free will ipo mkuu,utashi wa kuifanya future yako kuwa sawa na matarajio yako. Kila mtu anayo hiyo lakini sio kila binadamu anao uwezo wa kuitumia hiyo FREE WILL
 
You have no free will. Why do you end up doing things that you sweared to yourself that you will never do them again?
Why wont you will yourself to be good?
Why wont you will yourself to have perfect peace?
You have no free will. You are either influenced by good or evil
When you realize this, it makes you give up the fight and let God remove evil from your heart.
As long as you believe you have free will you will never overcome.
Ooh so what I get from you, is that human beings are like vehicles that can not drive themselves. Either Good (God) or evil (Satan) can drive them right?

When satan drives it we say he is demon possesed.
When God drives it we say he is led by the holy spirit.
Is that what you mean?
 
Nasilsiniz JF üye?
Naomba unisamehe maana kwa haraka haraka hata mimi najishangaa kuuliza hili swali, kwasababu it's a No-brainer right?, Namaanisha ofcourse binadamu sisi sio kama wanyama wanaotawaliwa kwa instincts, sisi tuna free will right?, Maana tokea nianze kujitambua mpaka sasa kila nachofanya nimefanya kwa hiari yangu. nikitaka kunyanyua mkono nanyanyua nikitaka kucheka nacheka..Mimi ndiyo nauendesha huu mwili si ndio?

Sadly, sikuizi mwenzenu nimeanza ku'second guess hayo mawazo baada ya ku'consider hizi factors.

1. Uwepo wa Mungu anayetaka ufuate masharti yake: Uwe mkristo au Muislam, Mungu anataka ufuate masharti yake, kuna mambo unatakiwa kuyafanya na kuna mambo hutakiwi kuyafanya. Kuna zawadi na adhabu kwa watakomfuata au kumpinga. Kitendo cha kuwepo tu adhabu nisipomfuata Mungu kinamaanisha sina hiari/free will katika maisha yangu hapa duniani, maana ningekuwa nayo ningekuwa na uhuru wa kufanya jambo lolote liwe jema au baya bila kuwa na consequences. Ni sawa na mtu akuwekee bunduki kichwani akuambie una uhuru wa kutaja au kutotaja password yako ya benki, ila usipotaja nakuua. Sasa hapo unao huo uhuru?
‘Free will’ ipo mkuu ktk mfano huu maana kuwepo kwa ‘consequences’ hakumaanishi tendo hilo halikuwa na ‘Free will’ kwa maana hakuna mtu kaumbwa kama malaika kuwa hana chaguo ila kufanya mema tu, kila mtu yuko huru kuchagua, ‘with consequences’ lakini na kwa bahati mbaya hakuna kitu hakina ‘consequences’.

Ila umeachwa huru huku ukipewa taarifa kuwa ukiswali kuna zawadi ila kama hutaswali kuna adhabu kwa maneno mengine uko huru kuchagua aidha zawadi au adhabu, hulazimishwi.

Hata mfano wa mwizi kukuwekea silaha akitaka utaje nywila ya benki bado uko huru kwa namna fulani, maana unaweza kuchagua
1. Kupigana nae
2. Kutaja nywila ukitumai atakuacha
3. Kukataa ili akuue kirahisi
(Sisi waislam kwenye hili tunaambiwa tuchague ya kwanza kwa maana Muumini mnyonge kamwe hawezi kuwa kwenye daraja sawa na Muumini mwenye nguvu)

2. Mazingira: Hapa nazungumzia mazingira yanayonizunguka tangu nizaliwe, ikihusisha vitu kama utamaduni wa jamii inayonizunguka(mfano jinsi ninavyovaa, ninavyoongea, ninayolia msibani, ninavyokula nk. Siwezi kwenda kinyume na utamaduni wa jamii niliyopo. Siwezi kwenda msibani na boxa tu huku nacheka, sina huo uhuru),Sheria inayonitawala (Siwezi kuendesha gari upande wa kulia),Malezi niliyokulia(Kwetu mwanaume Siwezi kusuka nywele nitakataliwa na ukoo),Elimu niliyoijaza kichwani(Elimu naweka mwenyewe kichwani ila ikishakaa yenyewe ndiyo inanitawala na kuniongoza, nilishasoma bailojia kwahyo siwezi kula vyakula vilivyochacha.),Status niliyo nayo katika jamii(Hakimu siwezi kushinda kwenye vijiwe vya kubeti na kulewa gongo),teknolojia, nk. Hivi vyote ni vitu ambavyo vinanipokonya uhuru wangu wa machaguzi. Ndiyo maana ukichukua binadamu waliokulia katika mazingira tofauti lazima watakuwa na tabia tofauti, ina maana hawana uhuru wa hizo tabia bali mazingira ndiyo huwaamulia. Vilevile binadamu waliokulia mazingira yanayofanana huwa na tabia inazofanana (Mf. Kuna tabia zinajulikana za wazaramo,wahaya,wazungu,wachina nk.)
Bado una ‘Free will’ mkuu, unaweza ongea tofauti ukitaka, ukavaa tofauti na ukaachana na tamaduni zako.
Mfano tu Tanzania tuna zaidi ya makabila 120 na kwa sasa watu wengi wanaacha kuzungumza kikabila na tunazungumza kiswahili, tufahamu kuwa hapo kabla makabila yao hayakujua kiswahili.

Tazama tunavyovyaa, sio sisi tuliokuwa tunavaa magome ya miti? Muziki tulikuwa tukipiga kwa ngoma? Na taarifa tuliitaka kwa mbiu?
Tazama vijana wetu mabarobaro wanavyopendeza kwa mavazi ya ki Magharibi, tazama Masheikh zetu kutwa kubadili kanzu za Dubai, unafikiri hatuna uhuru wa kuchagua?

Leo hii ukiamua kuvaa magome ya miti hakuna wa kukukataza mkuu ni chaguo lako, Mpoto bado anaendeleza utamaduni wa kutembea peku na mavazi asili akiamua, yuko huru.

Kuhusu vyakula tunavyo vya asili yetu na historia inatuambia hata mahindi hatukuwa nayo hapa, yaliletwa toka ardhi ya mbali, leo hii tunachagua kula Pizza, Burger au Ugali mlenda, Uhuru wa kimaamuzi tunao.

Elimu haizuii uhuru wako, Elimu inakuongezea wigo wa uhuru wako, nilikwambia kila jambo lina ‘consequences’ hii haikwepeki abadan, ukisoma hata ngazi ya PhD bado unaweza kula chakula kilichochacha ukiamua, ukisoma dini bado unaweza zini ukiamua.
Uhuru upo pale pale ila elimu itakuongoza kufanya machaguo sahihi na si laIma uifuate ukiamua unaweza kuisigina.

Wewe ni Hakimu ukitaka unaweza kulewa na kushinda vijiwe vya kubeti, ukiamua unaweza ila hilo lina ‘consequences’ kama ambavyo umechagua kutoenda hilo pia lina ‘consequences’ ambayo ni unaona huna uhuru ilhali unao.
3. Vizingiti vya kibaiolojia: Ninaweza kuwa na uhuru wote ila siwezi kuipinga baiolojia yangu, Siwezi kuacha kula,kulala,kupumua,kujisaidia nk. Pia siwezi kupaa,kubeba gari, kujifupisha, kujirefusha, kula viwembe, kupiga bao 10 nk.
Mkuu unaweza hivi vyote ila hujaamua tu. Ukiamua unaweza acha kula ila kuna ‘consequences’ na unavyoamua kuendelea kula vilevile kuna ‘consequences’
‘Consequences’ hazikwepeki mkuu.

Ukitaka unaweza acha kulala ila vilevile kuna ‘consequences’

Unaweza acha kujisaidia, unaweza jaribu kupaa, unaweza jaribu kubeba gari, unaweza jirefusha unaweza jifupisha, unaweza meza viwembe na unaweza piga bao 20 nini 10, haya yote ukiamua unayaweza vizuri sana ila hautakuwa tayari kubeba ‘consequences’ zake ila unaweza kuchagua.

Hivyo kwasababu lazima nile kuna vitu lazima nifanye ili nile (mf. kuomba,kufanya kazi,kubeti,kuiba nk.) na sina hiari katika hilo.
Hiyari ipo mkuu, unaweza amua kuacha kula tu hayo ni maamuzi yako.

Ila kuna ‘consequences’ kwenye kila maamuzi.
4. Brain Chemistry: Neuroscientists bado wanaendelea kugundua mchango mkubwa wa kemikali mbalimbali katika ubongo ambazo zinaweza kutengeneza,kubadili au kuondoa tabia kwa mnyama. Ubongo wa binadamu umeundwa kurespond to chemicals mbalimbal ndani yake. Mfano wa hizi chemicals ni Dopamine,Adrenaline,Oxytocin,Serotonin,Testosterone,Oestrogen na zingine nyingi.... Viwango vya hizi chemicals vinaathiri tabia ya mtu.Mfano Dopamine inatoka pale unapopata raha, kwahyo Dopamine husababisha mtu kufanya vitu ambavyo vinampa raha (kama Chaputa,kubeti,ngono,Kutumia mihadarati,kucheza mpira nk. nk.) Ukiondolewa dopamine unaweza ukafa maana unaweza ukaacha hata kula kwasababu huoni raha yake. Vilevile ikizidishwa dopamine kwenye ubongo unaweza ukafanya kile kitu kinachokuletea dopamine mpaka ukafa (mfano unaweza ukaacha kula ili utumie cocaine)
kuna panya aliwekewa cocaine na chakula, ila akaacha chakula ili ale cocaine mpaka akafa kwa njaa.
Mfano mwingine ni hizi kemikali za kijinsia kama Oestrogen na Testosterone ndio hufanya mwanaume au mwanamke kuwa na tabia za kiume au kike anapobarehe...Oestrogen inapozalishwa mda wa hedhi/mimbA hubadili tabia ya mwanamke....Ukiachana na hizi kemikali natural kwenye ubongo,hata hizi artificial tunazokula binadamu kama bangi,pombe,Cocaine Nk. zinaonyesha jinsi ambavyo kemikali kwenye ubongo huathiri tabia ya mtu. Sasa kama tabia zetu zinaathiriwa na viwango vya kemikali kwenye ubongo wetu, utasemaje kuwa tuna free will?
Kwenye kemikali asili za mwili bado tuko huru kuamua ukitaka utazipunguza au kuendelea nazo.

Dopamine hizo hutokea kutuzawadia pale tendo la furaha tunapolifanya, hivyo ukiwa huitaki hiyo usifanye matendo yanayokupa furaha.

Adrenaline kuna mahali pake huwa inatokea na kama huitaki suluhu ni kuepuka hali zitakazoifanya ije.

Bangi na cocaine vile vile ni hiyari yetu kuvitumia au la.
Bado tuna uhuru wa kufanya maamuzi ni vile hatuutumii makusudi tu.
 
Mada fikirishi sana.

Free will ipo mkuu,utashi wa kuifanya future yako kuwa sawa na matarajio yako. Kila mtu anayo hiyo lakini sio kila binadamu anao uwezo wa kuitumia hiyo FREE WILL
Mbona kila mtu ana struggle kesho awe tajiri lakini wachache ambao wanafanikiwa? Tena wengi wanafanikiwa randomly kama vile kuna ka bahati kana play part.
Either bahati ya kuzaliwa familia ya ukwasi kama Ridhiwani
Au bahati ya kuitwa interview na kuajiriwa
Au bahati ya kufanya uhalifu bila kushikwa
Au hata bahati tu ya kuzaliwa nchi yenye fursa
 
Don't and don't do. Hizi ni social nature
Matendo ya hiari na matendo ya lazima hii ishu ya biology
 
5. Brain Wiring: Neuroscientists wamegundua kuwa ubongo unafanya kazi kama kifaa cha umeme kupitia miunganiko maalumu ya neurones. Hizi seli ndani ya ubongo (Neurones) zimeungana na kutengeneza pathways (circuits) tofauti tofauti. Kuna neurones zaidi ya billioni 100 kwenye ubongo na kila neurone inaweza kuungana na neurones zingine jirani mpaka 1000. Kwahyo possible combinations ni ngapi hapo wanamahesabu?

Hiyo ni nje ya point, lakini point ni kuwa hizi circuits ndogondogo kwenye ubongo ndio hufanya specific functions,
iwe ni circuit kwa ajili ya kucontrol mapigo ya moyo au circuit kwa ajili ya kunyanyua kidole gumba au circuit kwa ajili ya kusema I love you (Nasimplify lakini its a lil bit complex than that na bado hatujui vingi kuhusu hili).
Ndiomaana huwa ngumu kubadili tabia ya mtu kwa siku moja (Mfano introvert kuwa extrovert,mvivu kuwa mchapakazi au Katili kuwa mpole nk.) kwasababu tayari circuits zinazotengeneza hizo tabia zinakuwa tayari zimeshajitengeneza,ili ubadili inabidi uache kutumia hizi circuits na uanze kutumia zingine zenye tabia mbadala. ambayo huwa ngumu and near impossible kuzifuta circuit zilizokwisha kujitengeneza.

Sasa kama tabia zetu,matendo yetu,mawazo yetu ni miunganiko ya circuits ndani ya ubongo ambazo huwezi kuzicontrol, utasemaje una free will?

Kuna vifaa vinavyoweza kupima activity ya ubongo na imeshagundulika experimentally kuwa kabla conscious mind yako haijafanya maamuzi yoyote mf. kunyanyua kidole, subconcsious mind inakuwa tayari imeshaamua..Kuna vifaa vinaweza kupima hizi neuurones za subconscious na wanasayansi wanaweza kuvitumia kutabiri utafanya nini milliseconds kabla wewe mwenyewe hujaamua utafanya nini. Na wanakuwa sahihi 99% of the time.
Pia wanasema kadri unavyoendelea kufanya jambo fulani na ndivyo sakiti hizo huzidi kujiunga, sasa hapo hulazimishwi kumbe maamuzi yako ndiyo huathiri sakiti hizo, basi kama hupendi vile zimeungwa badili maamuzi yako.

(Naelewa si rahisi ila nasisitiza tu kuwa uhuru tunao, sisi si kama roboti)
6. Determinism: Hii ni imani kuwa ulimwengu unatabirika, yani hali ya ulimwengu ulivyo sekunde hii ndio itakayoathiri na kuleteleza hali ya utakavyokuwa baadae. Maana yake ukijua hali ya kila kitu kilivyo sasa basi unaweza kutabiri kitakuwaje baadae. Mfano Ukijua gari lina spidi gani kuelekea upande fulani na ukajua acceleration yake, basi unaweza kutabiri kwa uhakika kuwa baada ya muda fulani litakuwa wapi na litakuwa na spidi gani. Samia leo ni raisi inamaana kesho samia atakuwa raisi.

Sasa kama imani hii iko sahihi, ulimwengu ni determined, inamaana tunaishi kwenye Movie. Ukiwa unaangalia movie ukafika katikati ukapause, wale waigizaji mule ndani hawajui movie itaishaje na hawawezi kubadili movie yani inabidi iendelee tu kama ilivyokwisha andaliwa. ingawa wanapoigiza ni kama vile kila wanaloanya wanafanya kwa hiari yao. Unaweza kukuta katikati ya movie anafanya kitu halafu anakuja kukijutia baadae.

Huenda hata haya maisha yameshapangwa sema tu sisi hatujui.
Yani ukiamua ucheke sasa, sio wewe uliyeamua ila ulikuwa umepangiwa kucheka muda huu. Na nadhani wanaoamini kuwa Mungu anajua kesho yetu, inabidi waamini katika hii determinism.
Sasa kama ulimwengu ni determined na kila kitu kimeshapangwa, je sisi tuna free will?
‘as long as am concerned’ bado ninaamini tuna ‘free will’, maana siku nikiamka ninaamua leo niswali au nisiswali kwa uhuru kabisa.
Hii dhana ya ‘determinism’ Ninakubaliana nayo ila bado napata nayo ukakasi ila ‘so far’ bado najihisi niko huru kufanya maamuzi yote maishani.

7. Indeterminism: Hii imani ni kinyume cha hiyo deteminism, yaani kwamba ulimwengu hautabiriki ila kila kitu kinatokea randomly by chance. Ulimwengu hauna end-goal au lengo lolote. maisha yanaplay out by chance tu kulingana na hiyo scenario/case husika. Mfano, Samia kuwa raisi haikuwa imepangwa ila ilitokea tu randomly by chance baada ya mkuu wake kufariki. Hakuna mpango au anayepanga chochote ila ni bahati u ndio inatawala ulimwengu...Sasa hata kama ukiamini hii indeterminism, bado tu hakuna free will maana kumbe sio hiari yetu tena bali ni bahati/chance/randomness ndio inaendesha maisha yetu. Sisi hatuna uhuru wa kufanya lolote kwenye haya maisha maana kila kitu kinatokea by chance.
Hii sikubaliani nayo hata kidogo. Kila mmoja wetu anayo nafasi ya kuamua uelekeo wa maisha yake.

Mathalan, unataka kuwa hakimu, ni lazima ukasome sheria, na ili usome sheria ni lazima usome mpaka ngazi fulani, sijawahi ona mtu kawa hakimu kwa bahati mbaya, ‘and I think this idea of universe events occurring by chance is laughable and absurd’
Mimi bado nakuna kichwa sijapata jibu kama binadamu tuna free will au la!
Vipi wewe mkuu, unadhani binadamu tuna free will? Kwanini?
Uhakika Bro
‘free will’ tunayo mkuu, na tunaitumia kila siku kila saa kila dakika, vitu ambavyo havina ‘free will’ ni maroboti ambayo mienendo yao na tabia zao inakuwa tayari zimepangwa kwa ‘algorithm’.

Leo mwanaadamu akiendeaha lori kwa kasi mbele akakuta bi kizee na gari iliyobeba wanafunzi yuko huru kuchagua amgonge nani kati ya hao wawili kulingana na hisia zake na akili yake, nilimsikia mtaalam mmoja akizungumzia mustakabali wa ‘self driving cars’ akasema kwenye ‘situations’ kama hizo roboti itaamua kulingana na ‘Alogarithm’ yake ilivyoundwa na akatoa wito kuwa watu wa maadili wahusishwe kwenye uundaji wa ‘Algorithm’ za magari hayo ili kuamua kimaadili nani afe katika ‘situation’ za namna hiyo.
 
Mkuu binafsi ninaweza kukusaidia kufanya chochote utachotaka ambacho unadhani hauko huru kufanya, andika tu hapa nitakupa hatua kwa hatua namna ya kufanya mkuu.
 
Back
Top Bottom