Maalim Raphael
Member
- Nov 23, 2018
- 49
- 87
Bila shaka hamjambo na wale mnaoumwa nawatakia afya njema.
Baada ya salamu naomba niwasilishe mada muhimu mahususi kwa vijana ambao ni mustakabali wa taifa letu. Tafadhali soma yote itakufaa sana. Sasa moja kwa moja nielekee kwenye mada.
Katika pitapita zangu mtandaoni kupitia ukurasa wa Meta (zamani Fecebook) wa mwanaharakati Hilmi Hilal nilikutana na kipande cha video iliyoniacha mdomo wazi.
Ni video iliyomhusisha msanii mmoja maarufu hapa Tanzania akiwa amelala kitandani akitazama kwa makini maudhui fulani kwenye simu yake aina ya iPhone huku dushelele likiwa limesimama. Ni dhahiri kwa muktadha ule msanii huyo alikuwa anaangalia ponografia.
Jambo hilo ndilo hasa limenisukuma kuandika makala hii. Kwa kuzingatia kuwa jambo hilo limefanywa na msanii msanii maarufu linaweza kuwafanya vijana wengi wenye uraibu wa ponografia na hata wale wasio waraibu kupata mashiko ya kuzidisha tabia hiyo โtunajua nguvu ya wasanii katika kushawishi.
Kwa mujibu wa TUKI (2006), Ponografia ni picha au maandishi yenye kutia ashiki. Picha hizo zinaweza kuwa mgando (zisizojongea) au picha jongefu (video).
Kundi kubwa la vijana hawafahamu kuwa kutazama ponografia husababisha uraibu mkubwa zaidi ya ule wa dawa za kulevya.
Kibaolojia binadamu kama viumbe wengine hupata msukumo wa kuzaliana lakini mfumo wa hamasa na zawadi wa mwili (dopamineโreward based system) haujui kutenganisha kati ya mwanadamu halisi na picha ya mwanamke aliye uchi anayeonekana kupitia skrini ya luninga au simu.
Sitii chumvi nikikwambia kuwa vijana wengi hapa Tanzania ni waraibu wakubwa wa ponografia. Kundi kubwa kati yao hawajui kuwa ni waathirika wa uraibu huo kwakuwa hawajawahi kufanya juhudi ya kuacha kutazama.
Kutokana na maendeleo ya TEHAMA maudhui ya kiponografia yamekuwa yakienezwa kirahisi kupitia mtandao wa intaneti. Hapo awali ilikuwa ni mwiko mkubwa kueneza maudhui ya ponografia.
Miaka ya 90 hadi 2000 kulikuwa na maeneo machacheโ hasa mabanda ya sinema ambapo ponografia zilioneshwa kwa malipo maalumu kwa watu wazima pekee. Kwa wanaokumbuka, ponografia ziliitwa "pilau" na mara zote zilioneshwa kwa siri tena usiku.
Miaka ya hivi karibuni umezuka mtindo miongoni mwa vijana wa Tanzania wa kusambaza video za utupu za watu mashuhuri wanazoziita "๐ฐ๐ผ๐ป๐ป๐ฒ๐ฐ๐๐ถ๐ผ๐ป".
Bila kufahamu athari zake au kwa sababu ya uraibu vijana wa kike na wakiume hujitokeza mitandaoni kuomba watumiwe video hizo.
Baadhi hutambua kuwa jambo hilo halifai, ndio utakuta wanaomba kwakutumia misemo kama; "๐๐๐ด๐ฎ๐๐ฎ๐ป๐ฒ ๐ฑ๐ต๐ฎ๐บ๐ฏ๐ถ."
Katika bandiko hili litakalojadili athari za ponografia nitaegemea zaidi utafiti uliofanywa na Taasisi ya maendeleo ya Mwanadamu ya Max Plank (Max Plank Institute for Human Development) ya jijini Berlin nchini Ujerumani (2014) na utafiti wa Kituo cha Uraibu wa Ponografia ya Mtandao (Neuroscience of Internet Pornography Addiction) [2015]
Utafiti wa Max Plank uliohusisha watafitiwa 64, uligundua uhusiano kati ya kiasi cha ponografia watafitiwa walichotazama (dosage) na mabadiliko kwenye bongo zao katika maeneo ya ubongo yanayohusika na ufanyaji maamuzi, tabia na motisha.
Utafiti uligundua kuwa matumizi ya ponografia ya mara kwa mara husababisha mabadiliko mabaya ya kimuundo na utendaji wa ubongo, yaani: 1.Kupungua eneo la kijivu (reduced gray matter)
2.Muunganisho mdogo wa utendaji kati ya mfumo wa hamasa na gamba la mbele la ubongo (prefrontal cortex) na mabadiliko mengine.
Kwa hivyo, utafiti huu ulionyesha kuwa watumiaji sugu wa ponografia na wale kawaida wana mifumo duni ya hamasa ikilinganishwa na wale wasiotumia.
Aidha ilionekana kupitia kipimo cha MRI kuwa eneo la ubongo linahusika na hamasa (Striatum) husinyaa kila mtu anapotazama ponografia. Vilevile ilionekana kuharibika muunganisho kati ya Striatum na eneo la mbele la ubongo (prefrontal cortex) linalohusika na tabia na kufanya maamuzi.
Matokeo ya utafiti yalipendekeza kwamba; "watu walio na matumizi makubwa ya ponografia huhitaji msukumo mkubwa zaidi ili kufikia kiwango sawa cha hamasa na hawana uwezo wa kufanya maamuzi sahihi."
๐๐๐ต๐ฎ๐ฟ๐ถ ๐๐ฎ ๐ท๐๐บ๐น๐ฎ ๐๐ฎ ๐ธ๐๐๐ฎ๐๐ฎ๐บ๐ฎ ๐ฝ๐ผ๐ป๐ผ๐ด๐ฟ๐ฎ๐ณ๐ถ๐ฎ ๐ธ๐๐ฒ๐ป๐๐ฒ ๐๐ฏ๐ผ๐ป๐ด๐ผ ๐๐ฎ๐ธ๐ผ
Zifuatazo ni athari za kutazama ponografia ziazojitokeza kwenye ubongo wako:
1.๐๐๐๐ฎ๐๐ฎ๐บ๐ฎ ๐ฝ๐ผ๐ป๐ผ๐ด๐ฟ๐ฎ๐ณ๐ถ๐ฎ ๐ต๐๐ฑ๐ฎ๐ป๐ด๐ฎ๐ป๐๐ฎ ๐๐ฏ๐ผ๐ป๐ด๐ผ ๐๐ฎ๐ธ๐ผ ๐ป๐ฎ ๐ธ๐๐ธ๐๐ณ๐ฎ๐ป๐๐ฎ ๐บ๐ฟ๐ฎ๐ถ๐ฏ๐ ๐๐ฎ ๐ธ๐๐ฝ๐ถ๐ป๐ฑ๐๐ธ๐ถ๐ฎ
Katika ubongo wako kuna eneo liitwalo kwa kimombo "reward center" ambalo husaidia kujenga tabia. Eneo hili pia huhusika na uzalishaji wa kemikali iitwayo ๐๐๐๐๐๐๐๐ ambayo huunganisha kati ya matendo na shauku ya kuyatenda matendo hayo.
๐๐๐ฎ ๐๐ถ๐ฝ๐ถ ๐ฝ๐ผ๐ป๐ผ๐ด๐ฟ๐ฎ๐ณ๐ถ๐ฎ ๐ต๐๐ฎ๐๐ต๐ถ๐ฟ๐ถ ๐ฑ๐ผ๐ฝ๐ฎ๐บ๐ถ๐ป๐ฒ?
Dopamine ni kemikali inayomfanya mtu ajisikie vizuri. Shughuli kama vile mazoezi, kula chakula kitamu na ngono husababisha kuzalishwa kemikali hii.
Hata hivyo, uzalishaji wa dopamine wakati wa kutazama ponografia huwa tofauti na ule wa shughuli nyingine kama kukimbia, kula au kufanya mapenzi. Kwa tabia nyingi za kila siku, ubongo una swichi ya "kuzima" ambayo huzuia kutolewa kwa dopamine mara tu shauku inapofika kikomo.
Kinyume chake, ponografia huathiri ubongo kwa kuzalisha kiwango kikubwa cha dopamine mchakato ambao pia hutokea kwa mtumiaji wa dawa za kulevya.
Baada ya muda, ubongo hujenga uwezo wa kustahimili dopamine ya ziada hivyo huhitaji kiwango kikubwa cha maudhui ili kufikia kiwango cha furaha kinachohitajikaโhali hii ndio humfanya mtu kuwa mraibu sugu.
Ripoti ya utafiti ya Kituo cha Uraibu wa Ponografia ya Mtandao (Neuroscience of Internet Pornography Addiction) inaonyesha kuwa kutazama ponografia hupunguza kwa kiasi kikubwa hamasa kwenye ubongo na kumfanya mtumiaji kuwa mraibu sugu.
2. ๐๐๐๐ฎ๐๐ฎ๐บ๐ฎ ๐ฝ๐ผ๐ป๐ผ๐ด๐ฟ๐ฎ๐ณ๐ถ๐ฎ ๐ต๐๐ต๐ฎ๐ฟ๐ถ๐ฏ๐ ๐บ๐๐๐ป๐ด๐ฎ๐ป๐ผ ๐๐ฎ ๐๐ฒ๐ต๐ฒ๐บ๐ ๐๐ฎ ๐๐ฏ๐ผ๐ป๐ด๐ผ ๐๐ฎ๐ธ๐ผ
Wakati "reward center" ya ubongo wako inapochochea kutolewa kwa "dopamine" pia hutoa protini iitwayo "๐ท๐๐๐ก๐๐น๐๐ ๐ต" ambayo hutumika kama "kichocheo."
Protini hii, huunda njia za neva ili kuunganisha kile mtu anachofanya na jinsi anavyohisiโkatika hali hii, mtu anapotazama ponografia mara kwa mara "DeltaFosB" huunganisha kwa nguvu furaha na kitendo cha kutazama ponografia.
Muunganisho wa namna hii husababisha mahitaji makubwa ya maudhui ya ponografia hivyo kumfanya mtu kurejea kutazama mara kwa mara.
Kwa mujibu wa Ripoti ya Neuroscience of Internet Pornography Addiction, ikiwa protini hii itaongezeka, inaweza kusababisha mabadiliko ya kudumu kwenye ubongo wako ambayo hukuachia uraibu mkubwa zaidi ya ule wa dawa za kulevya.
Njia za neva zinapounganisha "reward center" ya ubongo wako na kitu kinachodhuru kama ponografia, huharibu imani iliyojengwa awali kuhusu mambo yanayofaa na yasiyofaa na kukufanya ufikiri kwamba mambo yasiyo ya kimaadili ni ya kawaida.
Utafiti mmoja uligundua kuwa watu watazamao ponografia mara kwa mara hudhani kuwa matendo kama vile ubakaji na kishambuliwa wanawake ni mambo ya kawaida tu.
3. ๐๐๐๐ฎ๐๐ฎ๐บ๐ฎ ๐ฝ๐ผ๐ป๐ผ๐ด๐ฟ๐ฎ๐ณ๐ถ๐ฎ ๐ต๐๐ฎ๐๐ต๐ถ๐ฟ๐ถ ๐บ๐ฎ๐ต๐๐๐ถ๐ฎ๐ป๐ผ ๐๐ฎ๐ธ๐ผ
Kutazama ponografia husababisha uharibifu wa kudumu kwa vijana kuwa na mahusiano mazuri.
Kwa mfano, tafiti zinaonyesha kuwa kutazama ponografia ngumu (hard-core porn) huweza kubadilisha mitazamo kuhusu wanawake. Aghalabu wanaume wanaotazama ponografia mara kwa mara wana uwezekano mkubwa wa kuwadhania vibaya wanawake na kuwa na mitazamo ya chuki dhidi yao.
Kwa kuwa ponografia ndio chanzo cha taarifa zihusuzo ngono kwa vijana wadogo wa siku hizi, huchangia kuunda mawazo yaliyopotoka kuhusu wanawake.
Uchokozi wa kingono (sexual aggressiveness) ni ujumbe mkuu unaoonyeshwa katika ponografia ya kisasa, na utafiti mmoja wa video za ponografia uligundua kwamba 9 kati ya 10, mwanamke alikuwa akipigwa, kupayukiwa, au kudhuriwa kwa kupigwa makofi n.k. Hivyo kijana atakayeiga mfumo wa mahusiano ya kiponografia atajikuta anavuruga mahusiano yake.
๐จ๐๐ต๐ฎ๐๐ฟ๐ถ ๐ธ๐๐ฎ ๐๐ฎ๐ฟ๐ฎ๐ถ๐ฏ๐ ๐๐ฎ ๐ฝ๐ผ๐ป๐ผ๐ด๐ฟ๐ฎ๐ณ๐ถ๐ฎ
Bila shaka tabia ya kutazama ponografia umeijenga kwa miaka mingi, kama sio miongo. Hivyo haitakuwa rahisi kuivunja.
Utakapojaribu kuacha kuangalia ponografia utapata wakati mgumu hasa majuma mawili ya mwanzo kisha taratibu tabia hii hatarishi itaanza kufutika.
Haijalishi mara ngapi umeanguka kwa kurejea kutazama ponografia, unatakiwa ujitie hima kuacha kabisa.
Tambua kuwa hakuna mtu anayeweza kukulazimisha kuacha tabia hiyo bali ni wewe mwenyewe kuamua sasa.
Kama inakuwia vigumu kuacha, nakushauri ugoogle "nofap" โni jumuiya ya mtandaoni inayopambana na ponografia na kujichua (masturbation).
Humo utakutana na watu wanaohamasishana kuacha matumizi ya ponografia hasa katika kipindi kigumu cha uraibu.
Ndimi mwalimu wenu;
Longino, A.R
Morogoro
Tanzania
2023
adolfrafael.ar@gmail.com
Baada ya salamu naomba niwasilishe mada muhimu mahususi kwa vijana ambao ni mustakabali wa taifa letu. Tafadhali soma yote itakufaa sana. Sasa moja kwa moja nielekee kwenye mada.
Katika pitapita zangu mtandaoni kupitia ukurasa wa Meta (zamani Fecebook) wa mwanaharakati Hilmi Hilal nilikutana na kipande cha video iliyoniacha mdomo wazi.
Ni video iliyomhusisha msanii mmoja maarufu hapa Tanzania akiwa amelala kitandani akitazama kwa makini maudhui fulani kwenye simu yake aina ya iPhone huku dushelele likiwa limesimama. Ni dhahiri kwa muktadha ule msanii huyo alikuwa anaangalia ponografia.
Jambo hilo ndilo hasa limenisukuma kuandika makala hii. Kwa kuzingatia kuwa jambo hilo limefanywa na msanii msanii maarufu linaweza kuwafanya vijana wengi wenye uraibu wa ponografia na hata wale wasio waraibu kupata mashiko ya kuzidisha tabia hiyo โtunajua nguvu ya wasanii katika kushawishi.
Kwa mujibu wa TUKI (2006), Ponografia ni picha au maandishi yenye kutia ashiki. Picha hizo zinaweza kuwa mgando (zisizojongea) au picha jongefu (video).
Kundi kubwa la vijana hawafahamu kuwa kutazama ponografia husababisha uraibu mkubwa zaidi ya ule wa dawa za kulevya.
Kibaolojia binadamu kama viumbe wengine hupata msukumo wa kuzaliana lakini mfumo wa hamasa na zawadi wa mwili (dopamineโreward based system) haujui kutenganisha kati ya mwanadamu halisi na picha ya mwanamke aliye uchi anayeonekana kupitia skrini ya luninga au simu.
Sitii chumvi nikikwambia kuwa vijana wengi hapa Tanzania ni waraibu wakubwa wa ponografia. Kundi kubwa kati yao hawajui kuwa ni waathirika wa uraibu huo kwakuwa hawajawahi kufanya juhudi ya kuacha kutazama.
Kutokana na maendeleo ya TEHAMA maudhui ya kiponografia yamekuwa yakienezwa kirahisi kupitia mtandao wa intaneti. Hapo awali ilikuwa ni mwiko mkubwa kueneza maudhui ya ponografia.
Miaka ya 90 hadi 2000 kulikuwa na maeneo machacheโ hasa mabanda ya sinema ambapo ponografia zilioneshwa kwa malipo maalumu kwa watu wazima pekee. Kwa wanaokumbuka, ponografia ziliitwa "pilau" na mara zote zilioneshwa kwa siri tena usiku.
Miaka ya hivi karibuni umezuka mtindo miongoni mwa vijana wa Tanzania wa kusambaza video za utupu za watu mashuhuri wanazoziita "๐ฐ๐ผ๐ป๐ป๐ฒ๐ฐ๐๐ถ๐ผ๐ป".
Bila kufahamu athari zake au kwa sababu ya uraibu vijana wa kike na wakiume hujitokeza mitandaoni kuomba watumiwe video hizo.
Baadhi hutambua kuwa jambo hilo halifai, ndio utakuta wanaomba kwakutumia misemo kama; "๐๐๐ด๐ฎ๐๐ฎ๐ป๐ฒ ๐ฑ๐ต๐ฎ๐บ๐ฏ๐ถ."
Katika bandiko hili litakalojadili athari za ponografia nitaegemea zaidi utafiti uliofanywa na Taasisi ya maendeleo ya Mwanadamu ya Max Plank (Max Plank Institute for Human Development) ya jijini Berlin nchini Ujerumani (2014) na utafiti wa Kituo cha Uraibu wa Ponografia ya Mtandao (Neuroscience of Internet Pornography Addiction) [2015]
Utafiti wa Max Plank uliohusisha watafitiwa 64, uligundua uhusiano kati ya kiasi cha ponografia watafitiwa walichotazama (dosage) na mabadiliko kwenye bongo zao katika maeneo ya ubongo yanayohusika na ufanyaji maamuzi, tabia na motisha.
Utafiti uligundua kuwa matumizi ya ponografia ya mara kwa mara husababisha mabadiliko mabaya ya kimuundo na utendaji wa ubongo, yaani: 1.Kupungua eneo la kijivu (reduced gray matter)
2.Muunganisho mdogo wa utendaji kati ya mfumo wa hamasa na gamba la mbele la ubongo (prefrontal cortex) na mabadiliko mengine.
Kwa hivyo, utafiti huu ulionyesha kuwa watumiaji sugu wa ponografia na wale kawaida wana mifumo duni ya hamasa ikilinganishwa na wale wasiotumia.
Aidha ilionekana kupitia kipimo cha MRI kuwa eneo la ubongo linahusika na hamasa (Striatum) husinyaa kila mtu anapotazama ponografia. Vilevile ilionekana kuharibika muunganisho kati ya Striatum na eneo la mbele la ubongo (prefrontal cortex) linalohusika na tabia na kufanya maamuzi.
Matokeo ya utafiti yalipendekeza kwamba; "watu walio na matumizi makubwa ya ponografia huhitaji msukumo mkubwa zaidi ili kufikia kiwango sawa cha hamasa na hawana uwezo wa kufanya maamuzi sahihi."
๐๐๐ต๐ฎ๐ฟ๐ถ ๐๐ฎ ๐ท๐๐บ๐น๐ฎ ๐๐ฎ ๐ธ๐๐๐ฎ๐๐ฎ๐บ๐ฎ ๐ฝ๐ผ๐ป๐ผ๐ด๐ฟ๐ฎ๐ณ๐ถ๐ฎ ๐ธ๐๐ฒ๐ป๐๐ฒ ๐๐ฏ๐ผ๐ป๐ด๐ผ ๐๐ฎ๐ธ๐ผ
Zifuatazo ni athari za kutazama ponografia ziazojitokeza kwenye ubongo wako:
1.๐๐๐๐ฎ๐๐ฎ๐บ๐ฎ ๐ฝ๐ผ๐ป๐ผ๐ด๐ฟ๐ฎ๐ณ๐ถ๐ฎ ๐ต๐๐ฑ๐ฎ๐ป๐ด๐ฎ๐ป๐๐ฎ ๐๐ฏ๐ผ๐ป๐ด๐ผ ๐๐ฎ๐ธ๐ผ ๐ป๐ฎ ๐ธ๐๐ธ๐๐ณ๐ฎ๐ป๐๐ฎ ๐บ๐ฟ๐ฎ๐ถ๐ฏ๐ ๐๐ฎ ๐ธ๐๐ฝ๐ถ๐ป๐ฑ๐๐ธ๐ถ๐ฎ
Katika ubongo wako kuna eneo liitwalo kwa kimombo "reward center" ambalo husaidia kujenga tabia. Eneo hili pia huhusika na uzalishaji wa kemikali iitwayo ๐๐๐๐๐๐๐๐ ambayo huunganisha kati ya matendo na shauku ya kuyatenda matendo hayo.
๐๐๐ฎ ๐๐ถ๐ฝ๐ถ ๐ฝ๐ผ๐ป๐ผ๐ด๐ฟ๐ฎ๐ณ๐ถ๐ฎ ๐ต๐๐ฎ๐๐ต๐ถ๐ฟ๐ถ ๐ฑ๐ผ๐ฝ๐ฎ๐บ๐ถ๐ป๐ฒ?
Dopamine ni kemikali inayomfanya mtu ajisikie vizuri. Shughuli kama vile mazoezi, kula chakula kitamu na ngono husababisha kuzalishwa kemikali hii.
Hata hivyo, uzalishaji wa dopamine wakati wa kutazama ponografia huwa tofauti na ule wa shughuli nyingine kama kukimbia, kula au kufanya mapenzi. Kwa tabia nyingi za kila siku, ubongo una swichi ya "kuzima" ambayo huzuia kutolewa kwa dopamine mara tu shauku inapofika kikomo.
Kinyume chake, ponografia huathiri ubongo kwa kuzalisha kiwango kikubwa cha dopamine mchakato ambao pia hutokea kwa mtumiaji wa dawa za kulevya.
Baada ya muda, ubongo hujenga uwezo wa kustahimili dopamine ya ziada hivyo huhitaji kiwango kikubwa cha maudhui ili kufikia kiwango cha furaha kinachohitajikaโhali hii ndio humfanya mtu kuwa mraibu sugu.
Ripoti ya utafiti ya Kituo cha Uraibu wa Ponografia ya Mtandao (Neuroscience of Internet Pornography Addiction) inaonyesha kuwa kutazama ponografia hupunguza kwa kiasi kikubwa hamasa kwenye ubongo na kumfanya mtumiaji kuwa mraibu sugu.
2. ๐๐๐๐ฎ๐๐ฎ๐บ๐ฎ ๐ฝ๐ผ๐ป๐ผ๐ด๐ฟ๐ฎ๐ณ๐ถ๐ฎ ๐ต๐๐ต๐ฎ๐ฟ๐ถ๐ฏ๐ ๐บ๐๐๐ป๐ด๐ฎ๐ป๐ผ ๐๐ฎ ๐๐ฒ๐ต๐ฒ๐บ๐ ๐๐ฎ ๐๐ฏ๐ผ๐ป๐ด๐ผ ๐๐ฎ๐ธ๐ผ
Wakati "reward center" ya ubongo wako inapochochea kutolewa kwa "dopamine" pia hutoa protini iitwayo "๐ท๐๐๐ก๐๐น๐๐ ๐ต" ambayo hutumika kama "kichocheo."
Protini hii, huunda njia za neva ili kuunganisha kile mtu anachofanya na jinsi anavyohisiโkatika hali hii, mtu anapotazama ponografia mara kwa mara "DeltaFosB" huunganisha kwa nguvu furaha na kitendo cha kutazama ponografia.
Muunganisho wa namna hii husababisha mahitaji makubwa ya maudhui ya ponografia hivyo kumfanya mtu kurejea kutazama mara kwa mara.
Kwa mujibu wa Ripoti ya Neuroscience of Internet Pornography Addiction, ikiwa protini hii itaongezeka, inaweza kusababisha mabadiliko ya kudumu kwenye ubongo wako ambayo hukuachia uraibu mkubwa zaidi ya ule wa dawa za kulevya.
Njia za neva zinapounganisha "reward center" ya ubongo wako na kitu kinachodhuru kama ponografia, huharibu imani iliyojengwa awali kuhusu mambo yanayofaa na yasiyofaa na kukufanya ufikiri kwamba mambo yasiyo ya kimaadili ni ya kawaida.
Utafiti mmoja uligundua kuwa watu watazamao ponografia mara kwa mara hudhani kuwa matendo kama vile ubakaji na kishambuliwa wanawake ni mambo ya kawaida tu.
3. ๐๐๐๐ฎ๐๐ฎ๐บ๐ฎ ๐ฝ๐ผ๐ป๐ผ๐ด๐ฟ๐ฎ๐ณ๐ถ๐ฎ ๐ต๐๐ฎ๐๐ต๐ถ๐ฟ๐ถ ๐บ๐ฎ๐ต๐๐๐ถ๐ฎ๐ป๐ผ ๐๐ฎ๐ธ๐ผ
Kutazama ponografia husababisha uharibifu wa kudumu kwa vijana kuwa na mahusiano mazuri.
Kwa mfano, tafiti zinaonyesha kuwa kutazama ponografia ngumu (hard-core porn) huweza kubadilisha mitazamo kuhusu wanawake. Aghalabu wanaume wanaotazama ponografia mara kwa mara wana uwezekano mkubwa wa kuwadhania vibaya wanawake na kuwa na mitazamo ya chuki dhidi yao.
Kwa kuwa ponografia ndio chanzo cha taarifa zihusuzo ngono kwa vijana wadogo wa siku hizi, huchangia kuunda mawazo yaliyopotoka kuhusu wanawake.
Uchokozi wa kingono (sexual aggressiveness) ni ujumbe mkuu unaoonyeshwa katika ponografia ya kisasa, na utafiti mmoja wa video za ponografia uligundua kwamba 9 kati ya 10, mwanamke alikuwa akipigwa, kupayukiwa, au kudhuriwa kwa kupigwa makofi n.k. Hivyo kijana atakayeiga mfumo wa mahusiano ya kiponografia atajikuta anavuruga mahusiano yake.
๐จ๐๐ต๐ฎ๐๐ฟ๐ถ ๐ธ๐๐ฎ ๐๐ฎ๐ฟ๐ฎ๐ถ๐ฏ๐ ๐๐ฎ ๐ฝ๐ผ๐ป๐ผ๐ด๐ฟ๐ฎ๐ณ๐ถ๐ฎ
Bila shaka tabia ya kutazama ponografia umeijenga kwa miaka mingi, kama sio miongo. Hivyo haitakuwa rahisi kuivunja.
Utakapojaribu kuacha kuangalia ponografia utapata wakati mgumu hasa majuma mawili ya mwanzo kisha taratibu tabia hii hatarishi itaanza kufutika.
Haijalishi mara ngapi umeanguka kwa kurejea kutazama ponografia, unatakiwa ujitie hima kuacha kabisa.
Tambua kuwa hakuna mtu anayeweza kukulazimisha kuacha tabia hiyo bali ni wewe mwenyewe kuamua sasa.
Kama inakuwia vigumu kuacha, nakushauri ugoogle "nofap" โni jumuiya ya mtandaoni inayopambana na ponografia na kujichua (masturbation).
Humo utakutana na watu wanaohamasishana kuacha matumizi ya ponografia hasa katika kipindi kigumu cha uraibu.
Ndimi mwalimu wenu;
Longino, A.R
Morogoro
Tanzania
2023
adolfrafael.ar@gmail.com