Mtego wa Noti
JF-Expert Member
- Nov 27, 2010
- 2,591
- 1,599
Msanii wa kizazi kipya kutoka Arusha maarufu kwa jina la JCB amewaomba msamaha waislamu wote kutokana na kutunga wimbo wenye baadhi ya mistari ya Quran. Kitendo hicho kiliwaudhi waislamu na kusababisha kuwafanya wamtafute popote alipo kwa kuwatumia polisi. Baada ya kusikia ivo, msanii huyo aliamua kujipeleka mwenyewe msikitini na kukutana na viongozi wa dini hiyo ambayo walimuonya na kumtaka amulete mtu aliyemshirikisha kwenye wimbo huo ambaye ndiye aliyeweka hiyo mistari ya quran.
anasema alipompleleka huyo msanii mwenzake, waislamu walimtaka atangaze wimbo huo kuwa ni batili na ni dhambi kuendelea kuusikiliza huo wimbo na ni kinyume na dini ya kiislam.
Kupitia east african radio, msanii huyo amewaomba watu wote wenye huo wimbo waufute na usipigwe popote pale redioni. Pia amewaomba hata watu wenye huo wimbo kwenye simu zao waufute kabisa na wasiuzikilize tena!!!!
Bahati mbaya wimbo wenyewe umefutwa hata kabla mimi sijaupata kwa hiyo hata sijawah kuusikiliza.
Labda wenye wimbihuo wauweke hapa jamvini ili tuuage rasmi.
Source ni East African Radio....Zembwela na Baruti!!!
anasema alipompleleka huyo msanii mwenzake, waislamu walimtaka atangaze wimbo huo kuwa ni batili na ni dhambi kuendelea kuusikiliza huo wimbo na ni kinyume na dini ya kiislam.
Kupitia east african radio, msanii huyo amewaomba watu wote wenye huo wimbo waufute na usipigwe popote pale redioni. Pia amewaomba hata watu wenye huo wimbo kwenye simu zao waufute kabisa na wasiuzikilize tena!!!!
Bahati mbaya wimbo wenyewe umefutwa hata kabla mimi sijaupata kwa hiyo hata sijawah kuusikiliza.
Labda wenye wimbihuo wauweke hapa jamvini ili tuuage rasmi.
Source ni East African Radio....Zembwela na Baruti!!!