Jasusi Honda ndani ya mpango wa Congo

Imetulia
Riwaya : Mpango wa Congo

Sehemu ya tatu


Alitamani kukisoma kile kikaratasi,ila akajionya kutokufanya kosa lolote katika wakati kama ule ambao hajui wapi anapelekwa.
*****

Gari ilizidi kuacha mji wa Ivuba na haikufuata barabara kuu ya Julius Nyerere kuelekea katikati ya Mji wa Kinshasa au barabara ya Nailogi kuelekea kituo kikuu cha polisi Ivuba,badala yake ikawa inaelekea katikati ya mji unaokaliwa na waasi wa ADF(Allied Democratic Forces) hiki ni kikosi cha waasi kinachoshambulia mara kwa mara nchi ya Congo japo hujipambanua kama kikosi kinachompinga Rais wa Uganda.

Karandinga lilizidi kuiacha Ivuba na Kinshasa na sasa uelekeo wake ulikuwa ni kaskazini mwa Congo katika Jimbo la Kivu.

Safari ilikuwa ni ya mwendo kasi sana na muda wote watu wale walikuwa kimya kabisa.

Wakiwa wameanza kutoka kwenye makazi ya watu mara gari ikasimama gafla na haraka Sajini Kebu akateremka kisha akaja nyuma ya karandinga lile,hakusema kitu akatoa ishara fulani na mmoja kati ya askari akashuka chini na kwenda kumsikiliza Sajini.

Honda alikuwa akiwatizama kwa makini sana na aliona wakiteta jambo huku wakimtizama kwa macho ya wizi wizi.
Macho yao na maongezi yao yakamtia shaka ila akajipa muda wa maamuzi kwa sababu hadi muda huo hakujua nini alitakiwa afanye na pia hakujua kwa nini mauaji yamewaandama katika ofisi yao,hivyo alihitaji kujua zaidi ila alikwamishwa na aina ya watu waliomzunguka.
Sajini Kebu aliendelea kuteta na yule askari aliemuita huku kila mara wakiendelea kumtazama Honda.
Baada ya mazungumzo yao kuisha ndani ya dakika tano,Sajini Kebu na yule askari wajongea kwenye lile karandinga na walipolifikia,tofauti na matarajio ya Honda kuwa Sajini arudi kuvunja kishoka kule mbele na safari iendelee,ilikuwa tofauti badala yake wote wawili wakaja hadi nyuma ya karandinga na kisha wakapeana ishara na wale waliokuwa ndani ya karandinga lile kisha wakateremka wote wanne waliokuwa wamesalia na hapo ndipo Honda akachezesha akili yake kuona lipi rahisi kulifanya kwa wakati huo na akapata wazo moja tu,kukisoma kikaratasi alichokichukua kwa marehemu Bulembo.
Akakisoma ila hakuelewa kilichoandikwa kwa uharaka ule,akakariri kilichoandikwa mana hakutaka kuamini kilikuwa kimeandikwa bahati mbaya,na kama ni bahati mbaya inamaana gani kufichwa kwenye unyayo wa miguu na kufunikwa na soksi?
Mana ipo!!
Akarudia tena kukisoma.

“142BOULEVARD DU JUIN
B. P. 1612
KINSHASA CONGO (81).”

Alipohakikisha kilichokuwa kimeandikwa kimemkaa kichwani,akakitafuna haraka sana kile kikaratasi na kukimeza.
Kitendo hiki kilifanyika ndani ya nusu dakika tu kiasi kwamba hata wale askari licha ya kuendelea kumtazama hawakufanikiwa kuona uharaka wa kitendo kile.

Wajanja walikutana na mjanja!!.
Dakika mbili badae askari watatu walipanda kwenye karandinga na bila kumsemesha wawili wakamfuata na kunyanyua juu kimabavu,nusura wambwage chini kisha kwa mbwembwe wakamsukuma nje ya karandinga nae akatua chini kwa mbwembwe zile zile bila kuumia na ilikuwa rahisi kwake mana walikuwa hawajafanya jitihada zozote kumfunga.
Kitendo chake cha kutoanguka kikawa kama kimewatia hasira,wale wawili waliokuwa wamebaki chini wakampokea kwa kipigo kizito bila kujali anakwepa au la.
Kipigo alichopewa Honda ndani ya dakika tano kilitosha kumuacha bila nguvu za kusimama na hapo ndipo akagundua alikuwa anapigwa na askari wote watano isipokuwa Sajini Kebu,ambae muda wote alikuwa kimya akishuhudia vijana wake wakimsulubu mfanyakazi yule wa ubalozi wa Tanzania nchini Congo.

Sajini Kebu alipiga hatua moja na kufika pale alipokuwa Honda akitweta kwa maumivu,akamwinamia na kumshika ukosi wa shati lake kisha akamvuta kwa nguvu na kufanya nyuso zao zitazamane kwa karibu zaidi na bila kusema kitu Sajini Kebu akamshushia kichwa kizito Honda na kumuacha akiwa na nundu kwenye paji la uso huku akijibwaga chini kama mzigo ulioozesha matunda.

Honda alipoanguka akafanya jitihada za kunyanyuka na hapo akaona Sajini Kebu anamfuata tena kwa gadhabu na bila kusema kitu akawahi kuushika mkoba uliokuwa ukininginia shingoni Honda.
Honda hakutaka kukubali kizembe,nae akajitutumua kumdhibiti Sajini Kebu asichukue ule mkoba.
Dhamira yake ya kuulinda ule mkoba ukagonga mwamba bada ya mmoja wa askari wale kumchapa teke la kifua na kumyanyua juu kisha kubwagwa chini kwa uzito wa teke lile na hapo askari mwingine akaudaka ule mkoba na kuutoa shingoni kwa Honda.
Honda hakuwa na la kufanya akabaki akitweta kwa maumivu huku akipanga namna ya kuwadhibiti watu wale ambao tayari walionekana si wema kabisa.

Baada ya Sajini Kebu na wenzie kuona wamemdhibiti Honda; akauchukua mkoba ule na kuanza kuukagua kwa umakini sana
 
Hello Kudo
Nimekumiss
Tafadhali tuwekee hata sehemu moja ili nafsi yangu ipate tulia
 
Tafadhali ndugu uwe unakuwa na busara kidogo, wote si wakaa vijiweni, tuna mishe zingine pia, lakini kikubwa ukiona unacheleweshewa unaeza kuacha kufuatilia.

Mana naona tangu imeanza riwaya hii unatoa lugha za ajabu tu, kuwa muungwana tafadhali
Usinitishe kama huweki tulia huko kuku pori ww

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Punguza jazba kiongozi, pamoja na kuwa arosto inatupelekesha ila tusimuudhi na kumkatisha tamaa mwasilishaji wetu.
Akitaka aache hakuna aliyemlazimisha kupost humu. Wakati mwingine hawa waandishi wanapost hadithi zao kama sehemu ya matangazo ya biashara zao sasa wanataka mpaka tuwapigie magoti ili waendelee kupost.

Wakitaka ni bora wawe wanatoa taarifa mapema kama ni kwaajili ya matangazo...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Akitaka aache hakuna aliyemlazimisha kupost humu. Wakati mwingine hawa waandishi wanapost hadithi zao kama sehemu ya matangazo ya biashara zao sasa wanataka mpaka tuwapigie magoti ili waendelee kupost.

Wakitaka ni bora wawe wanatoa taarifa mapema kama ni kwaajili ya matangazo...

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwel mkuu waache kutufanya sisi kama wahuni mbona Steve Molel watu hawamtukani anasema kwel kuwa hapa haitoisha Ila ntauza tunamuelewa sasa huyu cjui mwandishi uchwara anatutisha akalale huko bumbavu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Akitaka aache hakuna aliyemlazimisha kupost humu. Wakati mwingine hawa waandishi wanapost hadithi zao kama sehemu ya matangazo ya biashara zao sasa wanataka mpaka tuwapigie magoti ili waendelee kupost.

Wakitaka ni bora wawe wanatoa taarifa mapema kama ni kwaajili ya matangazo...

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwel mkuu waache kutufanya sisi kama wahuni mbona Steve Molel watu hawamtukani anasema kwel kuwa hapa haitoisha Ila ntauza tunamuelewa sasa huyu cjui mwandishi uchwara anatutisha akalale huko bumbavu

Sent using Jamii Forums mobile app
Nadhani nyinyi ndo muache kufuatilia nyuzi zangu wakuu mana hamjalazimishwa kufuata riwaya ninazo weka,

Wanaonifahamu na riwaya zangu nilizowekaga hapa wanajua utaratibu Wangu, riwaya ikiaanza lazima iishe, inayouzwa inatangazwa kabla haiujarushwa hapa...

Lakini ninyi ambao hamfahamu au mnafahamu lakini ni ustarabu tu mmekosa, ndio mnaotukana na kutoa kauli zisizo na mashiko, mnyonge wa hali ya chini ,nadhani sio mara ya kwanza kusoma riwaya zangu na nimesikitika kuona unashambulia tu pasipo kujua sijui kwanin umeingia kwenye mkumbo wa hivyo ndugu.

kuku mweusi tangu siku ya kwanza unatukana tu bila sababu ya msingi na sijui nilikukosea nini hadi nistahili lugha kali unayonishambulia nayo.

Lakini lilokubwa ni kuwa kama unaona hupati ulichotarajia, kwanini usiache kufungua uzi huo ili usikwazike? Ya nini kutukana, kukashifu? Kitu ambacho unajua kabisa hakikuongezei chochote ukisoma au usiposoma?
Tafadhalini jamani namimi nin shuguli zingine za kufanya mbali na kuwa humu Jf!

Nitapost ila ni kila nipatapo Muda ila si kila nyie mkitaka, anatakae taka tutakuwa pamoja hadi kikomo ila asiependa basi ni vyema asifungue kabisa uzi huu mana ni riwaya ndefu sana hivyo unaeza kukwazika mara nyingi pia..
 
Riwaya :Mpango wa Congo

Sehemu ya tano




Mtega Nyoka!!
Ndio alikuwa ni Mtega Nyoka, Nyoka wanaomwinda Mzee Kinyonga!!

Ila kama alijua ni kazi rahisi kumlinda Kinyonga mbele ya nyoka wakaao pangoni, yaezekana alikosea kufikiri vema.
****
Katika mitaa ya Igoma, jirani na Ndama Hotel, msichana wa kadri ya miaka minne alikuwa amesimama kwenye kituo cha kungojea daladala.
Hakuna aliejua safari yake ilikuwa ni kuelekea Kishiri ama aliamua tu kupumzika pale huku akishuhudia magari ya upande wa pili yanayotoka Kishiri na Igoma yakielekea katikati ya mji, na pia akishuhudia magari ya upande wake yakishusha abiria zaidi kuliko kuwabeba.

Alivaa mawani ya jua,na hakuna aliejua kama anatazama kitu ama alikuwa anahamsini zake.

Kama angekuwa ameamkia sehemu safi na yenye hadhi, basi wakati huu angelikuwa ananukia uturi wa kisasa.
Lakini kama ungelimtizama kwa makini basi ungeligundua huyu binti hajapata lau hata nusu maji katika mwili wake kwa siku kadhaa.
Nae hakuonekana kujali uchafu wa mwili wake, pengine kwa kuwa alikuwa mweusi wa ngozi na uchafu haukuwa kigezo kwake tena.

Macho yake yakiwa yamefichwa nyuma ya mawani ila bado yalipepesa eneo lile alilokuwa amesimama na kuna kitu alikuwa anahakikisha upande wa pili wa barabara, kulikokuwa na kituo cha kuoshea magari na pikipiki.

Akatabasamu huku akitaka kuvuta hatua ili avuke barabara.

Akasita gafla huku tabasamu lake likififia na hofu ikauvaa mwili wake.
Haraka akatoa kofia aliokuwa ameishika kwenye mkono wake wa kulia na kupachika kichwani, kisha kama anaekimbia na nusu kutembea kutoka mbali na eneo lile.

Mtega nyoka nae alikuwa pale amekaa huku akiwa na mawazo lukuki, hasa baada ya kulala na kuamka bila kupiga hatua yoyote ile.

Akiwa ametulia tu, huku akiwaza wapi pa kuanzia ahsubuh ile, mara macho yake yakatua kwa mwanadada mrefu mweusi mwenye asili ya kitutsi akiwa amevaa miwani na kofia mkononi huku mgongoni akiwa na kibegi kidogo ambacho hakikuonekana kubeba nguo yoyote.

Kama ilivyo kwa wanaume wengi;nae Akaanz kumthaminisha binti yule huku akisahau mawazo yaliomfikisha pale.

Mbali ya tathimini yake, ila hakukawia kujua uchafu uliokuwa kwenye mavazi ya binti yule ambae hadi wakati huo hakuwa amefanya tashititi yoyote ile kumuangalia yeye ama yeyote aliekuwa nyuma yake.

Ilikuwa ni rahisi kwa mtu wa kawaida kuhisi binti yule anamatatizo ya akili ama kaibiwa siku chache nyuma, ama katoroka kwao na kafika mjini pasi na ramani ya kumfanya uzuri wake ubaki katika thamani yake. Lakini ilikuwa tofauti kidogo kwa Mtega nyoka ambae aligundua kitu kingine kabisa.
Kwa mtazamo wa haraka kulingana wajihi wa binti yule, aligundua yaezakuwa si mkazi wa jiji la Mwanza na Tanzania kiujumla.
“Mnyarwanda huyu binti” alijisemea Mtega nyoka huku akiamua kuacha kumtazama binti yule ambae aliamini tayari amekutana na wajanja wa mjini kulingana na hali aliokuwa nayo binti yule.

Mtega nyoka aliamua kuendelea kuwaza hili na lile na sasa alipata wazo moja tu,nalo ni kumtafuta msanifu wa majengo aliekuwa anafanya kazi binafsi.
Mbali ya kupata orodha kamili ya watu wanaofanya kazi na msanifu huyo; lakini pia angepata mwanga kidogo ni kwanini wafanyakazi wa msanifu huyo wa majengo walikuwa wanakufa vifo vya ajabu kiasi kile huku yeye akiwa nae akiwa amepewa kazi na serikali yake kuhakikisha wasaidizi wa msanifu mkuu wanafanywa ilivyotakiwa kufanywa ili kulinda itifaki.

Ni wakati akianza kujiinua kutoka alipokuwa amekaa, ndipo alipoona jambo lingine lililomsitua zaidi,yule binti alikuwa anaharakisha kuondoka pale kwa mwendo wa nusu kukimbia na nusu kutembea.
Ingelikuwa macho ya kawaida ungeona ni haraka tu za yule dada,lakini macho ya Mtega nyoka, yaligundua hofu na mashaka kwenye mwendo wa binti yule.

Kwa nini!! Hakujua.

Mawazo yake yakamtuma amfuate yule binti lakini akajikuta hana sababu ya kumfuata.
Akapuuza.

Yule binti alizidi kukata mitaa kuelekea Igoma katikati huku kila mara akigeuka na kuhakikisha usalama wake,alikokuwa akielekea hakupajua, japo aliamini aelekeako atapata mawazo mapya kuhusu maswahibu yanayompata na namna ya kukabiliana nayo japo aliamini kupona ni miujiza ya mwenyezi Mungu.
Roho mkononi!
Lakini kuna kitu kilichomchanganya akili zaidi ni kile alichokiona.

Aliemhitaji alimwona ni baada ya kumtafuta ndani ya mji wa Mwanza karibuni siku tatu. Lakini aliekuwa anamkimbia alimwona pale kwa mtu aliekuwa anamtafuta kwa udi na uvumba.

“alijuaje nitafika kwa Mwasu?” alijisemea binti yule.
“mh” akaguna na kusita kuendelea kupiga hatua zaidi.

“Mungu wangu!!” akasema kwa hamaki baada ya kuhisi jambo baya linaweza kumtokea Mwasu, au Mama Ujazo kama walivyopenda kumuita wateja wa chakula chake.
Binti yule akapiga hatua ndefu zaidi kurudi kule alikomwona Mwasu,huku dhahiri shahiri akionekana kupagawa kwa alilokuwa ameliwaza.

Dakika sita baadae alikuwa anatazamana na binti wa miaka kama kumi na sita hivi; aliekuwa anahudumia wateja kwenye mgahawa ule wa maturubai.

“kuna wali maharage;ugali dagaa..” alitaja vyakula vilivyokuwa vinapatikana pale mgahawani kwake.

“sihitaji chakula mdogo wangu” alijibu binti aliefika pale.
Ikawa mshangao kwa binti anaehudumia.
Lafudhi!!
Msukuma yule anaehudumia kwenye mgahawa wa Mama ujazo,alibaki anashangaa lafudhi ya mgeni wake yule,haikuwa lafudhi ya Kitanzania,lakini kubwa lafudhi ile inaufanano kwa mbali na lafudhi ya Mwasu.
Akashangaa!!
Licha ya kushangaa, ila hakutaka fikira zake zimuibulie maswali.
Akabaki kimya kumsikiliza msichana mwenzie alimzidi kimo cha urefu na weusi wa kung’aa.

“Namuulizia Mwasu!” alisema binti mweusi huku akimtizama Msukuma wa Bariadi.

Msukuma wa Bariadi akagundua kitu kingine tena.
Ustarabu!
Binti aliekuwa mbele yake, hakuwa na ustarabu wa Kitanzania,Mtanzania yeyote akitaka kuuliza lazima aanze na neno ‘Samahani’ila huyu huo ustarabu hakua nao kabisa.
“Sio Mtanzania huyu” alijiwazia Msukuma.

“mmh hilo jina silifahamu dada” Binti wa kisukuma akajibu huku bado akiwa amemkodolea macho binti mgeni.

Binti mgeni akalikumbuka jina maarufu aliloambiwa na Mwasu siku kadhaa nyuma, jina hilo lilimeza jina lake la kuzaliwa.

Mama ujazo!!

“mh nimekumbuka, anaitwa Mama ujazo” alisema binti mgeni huku akitabasamu ili kumtoa kwenye udadisi mwenyeji wake.

“aah sawa;katoka hapa punde tu na Kaka yake!”

“kaka yake!!?”

“ndio amesema ni kaka yake, na wameenda kwake”

Akili ya binti mgeni ikapiga kite cha hofu baada ya kuhisi huyo kaka alieondoka na Mwasu ni yule aliemkimbia dakika chache zilizopita.

Binti mgeni akasikia tumbo likiunguruma kwa woga,akaangaza kushoto na kulia kuona kama kuna choo maeneo yale,hakukiona.
Jasho la hofu likatanda mwilini mwake,kichwa kikamwasha mithili ya mtu mwenye mba sugu.

“my God! Mwasu hastahili kufa” akajiwazia haraka akataka kutoka mle mgahawani.
Akakumbuka cha muhimu.

“aah anaishi wapi kwani” aliuliza.

“anapoishi sipafahamu; ila ni huko Nyakato Meko” alijibu binti wa kisukuma.

“shiiit” akang’aka kwa fadhaa.
Binti mgeni akaanza kutoka kwa pupa akadakwa mkono.

“Hebu ngoja kwanza; kwani wewe ni nani yake?” aliuliza Msukuma.

“mdogo wake” alijibu Binti mgeni.

“unaitwa nani?”

Binti mgeni akafikiria kidogo kisha akajibu.

“Naitwa Remi”

“ooh, sasa nenda Buzuruga plaza,pale kuna ofisi za Kasuku contractors,hapo kuna mchumba wake anaitwa Malima,yeye anaeza kukufikisha kwake kirahisi,mana hapa harudi tena na mimi sina simu dada angu” alieleza kwa kirefu binti Msukuma.

Remi alishukuru kwa ukarimu wa aina ile kutoka kwa Msukuma. Akaaga na kuondoka kwa haraka ya ajabu huku akimwacha Msukuma akimwangalia bila kujiuliza haraka zile za nini.
Watanzania hatuna udadisi,amani imetujaa!!

***
Nusu saa badae,Remi alikuwa anashuka kwenye daladala huku tumbo la kukata lilomkumba gafla kule mgahawani kwa Mwasu,lilianza tena kukata huku jasho likianza kutoka tena.
Hali ile ilimkuta kwa sababu hakuwa na hakika na kumpata Mwasu.
Akatazama jengo lile lilivyopendeza huku watu wakiendelea na shughuli zao kama kawaida. Macho yake yalikuwa yanapepesa kila kona ili apate kuona kibao cha Kasuku Contractors.

Alikiona.

Akapiga hatua za tahadhari huku mapigo ya moyo yakiongezeka kama ya mkimbia marathon.
Alizidi kufuata ulekeo kama kibao kilivyoelekeza.

Alibaki akitazamana mlango wa mapokezi. Mapigo ya moyo yalizidi kwenda kasi ya zaidi.
Akapumua kwa nguvu kujipa ahueni kidogo.
Hatimae akausukuma mlango na kuingia ndani.
Akakaribishwa na mandhari nzuri za ofisi ile ya ujenzi na uhandisi wa majengo,lakini pia ilikuwa na watalaamu wa kusanifu majengo.
Ilimchukua dakika nzima kushangaa na kujaribu kuyazoea mazingira ya ofisi ile.

“Karibu dada!” ilisema sauti ya kike.
Remi alipiga hatua za woga kusogea pale alipokuwa dada aliemkaribisha,ambae hakuwa peke yake,kulikuwa na mtu mwingine mwenye jinsia ya kiume na kimtazamo tu nae alionekana kuwa ni mgeni ofisini pale.

Alieyekuwa pale mapokezi alikuwa ni Mtega nyoka.alifika pale kumuulizia Msanifu mkuu wa majengo wa kampuni ile inayomilikiwa na vijana wa kitanzania.
Akiwa ndo kwanza ameanza kusikilizwa mara akaingia mwanadada ambae yule yule ambae alimwona pale Igoma saa moja iliopita.
Akapigwa butwaa!

Remi hakujali uwepo wa mtu mwingine pale. Alikuwa anataka kuwahi kuonana na Mwasu.

“Nauliza ilipo ofisi ya Malima” aliuliza Remi.

Dada aliekuwa mapokezi akamtazama kisha akainama chini na alipoinuka alikuwa anadaftari na kalamu.

“Andika hapo majina yako na namba yako ya simu” akaeleza dada wa mapokezi.

“Sijui kuandika wala kusoma”

Ajabu hii.

Si dada wa mapokezi alieshangaa jibu la Remi; hata Mtega nyoka hakutaka kuamini kirahisi vile eti katika Dunia hii kuna mtu mwenye uzuri na sura ile hajui kusoma.
Hata!!

“Basi kama ndivyo hutaweza kusikilizwa” alisema dada wa mapokezi huku akionekana kukereka baada ya kuhisi amedharauliwa na mwanamke mwenzie.

“Ni muhimu,tafadhali nielekeze” alisema Remi.

Huku akibinua midomo na kuendelea kuwa bize na Tarakilishi iliokuwa mezani kwake akasema.

“Binafsi au kikazi?”

“Binafsi dada” Remi alijibu.

Muda wote huo Mtega nyoka alikuwa kimya kabisa.

“kwa hiyo Malima ndo huwa anakutana na wasiojua kusoma?” aliuliza dada wa mapokezi.

Tofauti na mawazo yao kwamba yule mgeni asiejua kusoma na kuandika ataendelea kubembeleza; haikuwa hivyo.
Remi akapiga hatua ndefu na kuanza kuondoka ofisini pale huku dhahiri akionekana kupagawa.

Dada wa mapokezi alimwita ila Remi hakugeuka wala kusimama aliendelea kuendea mlango.

“kwani huyo Malima yupo?” Hatimae Mtega nyoka akauliza,na kwa gadhabu dada wa mapokezi akajibu.

“Wameenda kuzika wahandisi wa kampuni waliokufa juzi”

Mtega nyoka hakustuka kwa vifo vya wahandisi hao mana alishuhudia miili yao ikiwa haina uhai usiku wa jana japo akiefanya vile hakumjua.

Mtega nyoka akaona kuna kitu kipo kati ya dada asiejua kusoma na huyo Malima ambae nae alikuwa na shida nae. Mtega nyoka akapiga hatua kumwahi yule dada kabla hajatoka kwenye viunga vya Buzuruga Plaza.

Remi hakuwa mjinga wa kutoka pale bila kujua au kuonana na Malima.

Kabla hajaingia pale ofisini ,pembeni yake aliona saluni ya kike kubwa na kwa tabia za wanaume na wanawake alijua kabisa mmoja ya wahudumu pale saluni atakuwa anajuana na Malima ama la anamawasiliano yake.
Akauendea ule mlango wa saluni.

***
Mtega nyoka alibaki amezubaa kwenye valanda pana iliotenganisha milango ya ofisi zilizokuwa pale.
Hakumuona aliemtaka.
.haraka akakimbia nje ya lango la kuingilia pale Plaza huko nako hakumuona.
Akili yake haikukubali yule dada ametoka ndani kwa haraka kiasi kile.
Akarudi tena kule ndani.
Wakati yeye anaingia akapishana na Remi akitoka huku akiweka kitu kwenye matiti yake.
Mtega nyoka akamwacha apite kisha awe nyuma yake.
Mtega nyoka hakujua sababu gani aliamua kumfuatilia yule dada, ila alijikuta tu anamfuatilia.

Remi aliendelea na safari yake huku akiwa na jambo moja tu,kutafuta simu na kuzipiga namba za Malima alizopewa na mmoja ya wahudumu wa saluni.
Kitu kimoja ambacho hakujua ni kuwa wakati wote wa harakati zake kulikuwa na mtu mmoja zaidi aliyekuwa nae bega kwa bega na sasa alikuwa amepokea amri ya kumchukua mzima ama mfu na kumpeleka kusiko julikana na kazi hiyo ilitakiwa kufanywa wakati Remi akitoka Buzuruga Plaza.

Remi hakujua hesabu anazopogiwa na watu wawili kwa wakati mmoja huku miongoni mwao akiwepo mwenye nia ya kujua sababu ya kumtafuta Malima na mwingine akiwa na sababu ya zaidi kuua.

Hatimae Remi akaanza kuambaa na kuifuata Barabara mara mbele yake akakutana na mtu ambae hakutarajia kumuona pale.
Mtekaji!!
Remi akataka kugeuka na kurudi alikotoka.
Alichelewa!

Mikono imara ikamdaka bega lake na kumvuta kwa nguvu,kisha kikafuatia kibao kikali kilichotua sawia mgongoni mwa Remi huku kikimtoa kelele ya uchungu.

Remi alipepesuka na kutaka kuanguka chini,lakini akajikuta akijaa mikononi mwa mtu mwingine aliekuwa nyuma yake.
Alinguka mikononi mwa Mtega nyoka!

Mtekaji akabaha baada ya kuona kasi iliotumika kumdaka Remi.

“ugomvi huu haukuhusu braza, nipe huyo binti niende nae zangu” alisema mtekaji.

Mtega nyoka alikuwa akitazamana na mtu mrefu mwembamba lakini alionekana kuwa imara sana.
Mbali na mwonekano huo, lakini pia Mtega nyoka aligundua lafudhi ya mtekaji na mtekwaji zinafanana lakini pia hata sura na mwonekano ni watu wa jamii moja.

Kuna nini! Hakujua na la muhimu zaidi ni kuomukoa kwanza binti kisha mengine yatajulikana badae.

Akamvutia nyuma na kuwa kinga yake.
Mchoro ukachorwa huku raia wakianza kujaa kushuhudia linalojiri.

****

KINSHASA CONGO

…kutoka pale alipokuwa Honda alibakiza hatua mbili tu afike kwenye ukingo wa daraja lililokuwa linapitisha maji kwa chini.
Na bado alikuwa amemkaba barabara Sajini Kebu.
Wale askari wengine walikuwa bado wanapiga hesabu za kumwokoa Sajini Kebu kwa kusuburi Honda afanye kosa lolote ambalo hadi wakati huo halikuwa limefanywa nae hivyo wakakosa la kufanya.

Lakini Honda mbali ya kuwa na hesabu za kutoroka bado alikuwa anawazia namna ya kuwatoroka ama kuzua varangati litakalo wafanya wasahau kuhusu mkoba na kile kidole pale chini.

Pale walipokuwa ilikuwa ni barabara isiopitisha magari kwa wingi.
Lakini kwa mbali masikio ya wote yalinasa sauti ya kuja kwa gari kubwa.

Honda alitabasamu huku watekaji wake wakiingiwa na mchecheto wa namna ya kumuokoa sajini Kebu kabla gari hakijafika.

Hesabu zilipigwa pande zote.

Dereva wa lori aliona tukio lililokuwa mbele yake. Kurudi nyuma akaona haiwezekani hivyo akaamua kuongeza mwendo ili avuke pale darajani kwa kasi huku woga ukiwa umemtamalaki na mkojo ukikaribia kugonga hodi kwenye kipamchulio.

Lori lilizidi kukaribia na Honda nae alizidi kujisogeza kwenye ukingo wa daraja huku akiwa bado amemtundika kabali matata Sajini Kebu.
Hatimae lori likafika na hapo ndipo lilitokea tukio ambalo yaezekana Sajini Kebu na wenzie hawatakuja kuliona likijirudia tena katika himaya za macho yao iwe akhera ama Duniani.
 
Nadhani nyinyi ndo muache kufuatilia nyuzi zangu wakuu mana hamjalazimishwa kufuata riwaya ninazo weka,

Wanaonifahamu na riwaya zangu nilizowekaga hapa wanajua utaratibu Wangu, riwaya ikiaanza lazima iishe, inayouzwa inatangazwa kabla haiujarushwa hapa...

Lakini ninyi ambao hamfahamu au mnafahamu lakini ni ustarabu tu mmekosa, ndio mnaotukana na kutoa kauli zisizo na mashiko, mnyonge wa hali ya chini ,nadhani sio mara ya kwanza kusoma riwaya zangu na nimesikitika kuona unashambulia tu pasipo kujua sijui kwanin umeingia kwenye mkumbo wa hivyo ndugu.

kuku mweusi tangu siku ya kwanza unatukana tu bila sababu ya msingi na sijui nilikukosea nini hadi nistahili lugha kali unayonishambulia nayo.

Lakini lilokubwa ni kuwa kama unaona hupati ulichotarajia, kwanini usiache kufungua uzi huo ili usikwazike? Ya nini kutukana, kukashifu? Kitu ambacho unajua kabisa hakikuongezei chochote ukisoma au usiposoma?
Tafadhalini jamani namimi nin shuguli zingine za kufanya mbali na kuwa humu Jf!

Nitapost ila ni kila nipatapo Muda ila si kila nyie mkitaka, anatakae taka tutakuwa pamoja hadi kikomo ila asiependa basi ni vyema asifungue kabisa uzi huu mana ni riwaya ndefu sana hivyo unaeza kukwazika mara nyingi pia..
Bora umekuwa muwazi kuwa itaisha ila usiwe unatukaliza mda mrefu kama unaona niaje tangaza tununue

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

20 Reactions
Reply
Back
Top Bottom