Jarida la The Economist ladai uchumi wa Tanzania unaporomoka, lahamasisha Rais Magufuli adhibitiwe kwa vikwazo kiuchumi

Nipe jina la kiongozi hata mmoja aliyefanikiwa kwa kwenda against western countries
 
How? wanaomba misaada kwetu? Wana nini wanachokikosa wakiachana na sisi? Jiulize wakisusia dhahabu kuna wa kuzinunua? Remember, Diamonds are forever!
Hawaombi misaada kwetu kwa sababu wanatuibia...WAMESHIKWA VIBAYA MNO NA MAGUFULI....
Possibly hata huyo mwandishi wa HILI GAZETI INAWEZEKKANA KAHONGWA HATA NA ACCACIA
 
Me nadhan issue c kukanusha kwenye vyombo vya habari ila kuangalia wapi tumekosea km taifa tusonge mbele
Mkuu. Hivi unadhani hawa jamaa wanatupenda saaaana! kiasi kwamba wanajisikia uchungu uchumi wetu unaposhuka?
Think twice. Kwangu moja ya indicator kuonesha Rais wetu yupo kwenye mstari sahihi ni hizi kelele zao za maumivu kana kwamba wanatujali saaaana!
 
Et real 100% ...may be real on lies by 100%
 
Acha upuuzi Hawaombi misaada kwetu kwa sababu wanatuibia...WAMESHIKWA VIBAYA MNO NA MAGUFULI....
Possibly hata huyo mwandishi wa HILI GAZETI INAWEZEKKANA KAHONGWA HATA NA ACCACIA
Kusema wanatuibia nadhani sio sahihi maana tumesaini mikataba ambayo ipo kisheria na sisi kuingia nao ubia tena wanalipa kodi na tozo mbalimbali serikalini sasa utasemaje wanatuibia wakati wanafanya kazi kihalali au maana ya wizi imebadilika mkuu?

Tatizo lipo kwa viongozi wetu tuliowapa nafasi ya kuzisimamia rasilimali zetu hawa ndio sio waaminifu wapo kwa ajili ya maslahi yao binafsi na sio ya nchi

Ndio maana wanaingia mikataba ambayo hainufaishi nchi ila wao na ndio hiyo unasema wanatuibia lkn sio ni mikataba mibovu iliyoingiwa na wenzetu kwa ajili ya kujinufaisha ila ni mikataba halali kabisa
 
Paskali, lazima wasomaji wenzangu tuache papala! Mpangilio wa jarida lazima tuufahamu. Huwa kuna taarifa rasmi za kiuchumi, zinazotokana na uchunguzi wa jarida. Pia kuna taarifa zinazoandikwa na waandishi binafsi kwa mtazamo wao na maomni yao, yaani columnist. Taarifa hii ya Magufuli siyo ya Jarida ni ya columnist. Unaweza ukampuuza tu!

Ukisoma taarifa hii kwa ufahamu, utagundua mwandishi anajaribu kufaidika na uzembe wa wasomaji. Kuna wasomaji wazembe kama unavyoona meseji au maoni ya wasomaji wa JF, wanaoona nafuu kwa kusaidiwa kueleza ubaya wa rais! Taarifa kama hizi huandikwa na watanzania na kuzitoa kwenye majarida kama haya.

Ukiangalia kichwa cha habari kinamzungumzia rais Magufuli na uchumi wa TZ. Lakini ukiangalia baadhi ya mambo mabaya yanayoandikwa ndani ya taarifa hii ni yale ya zamani yasiyomuhusu Magufuli. Lakini kwa msomaji mzembe mwenye kupenda kusikia ubaya wa magufuli, hataweza kuona mchezo na upuuzi wa mwandishi.

Hili ni jarida la uchumi halistahili kupima ubora wa mipango ya serikali kwa kuangalia investors walioingia nchini au walioondoka bila kusema faida gani ilipatikana kwa nchi. Investors ktk nchi hizi ni wale wanaokuja kuchota na mara zote ukiwadhibiti wanaondoka. Eti hilo nalo ndo jambo la kuandikwa na kutumwa the economist. Binafsi naona ni juhudi inayoendelea ili kiongozi atishike na alegeze baadhi ya mambo ya kipuuzi yaliyofanyika miaka ya nyuma yaendelee.

Wale munaoshabikia, nasikitika kuwaambia Ulaya au Amerika hakuna mjomba wa kukupa maendeleo, eti leo hii anasikitika kwamba unakosa njia safi ya kuendelea. Ukikenua meno kwamba umetetewa, baadaye ni mtego wa kukulawiti.
 

Hahaaaaaaaaaaaaaaaaaaa!
Wengine neema hatujaiona,labda weye uliyejikoni!
Vipi Makinikia bado ziko Bandarini kwenye Makontaina??
Vipi Yale matrilioni?

Yako mazuri ya Raisi wa awamu ya Tano kiuchumi lakini mguvu kubwa isiyoakisi hali halisi ya mambo ni njia mmoja kuelekea Njiapanda Kiuchumi. Hili halihitaji Mchumi kuliona. Maneno huumba,na imeandikwa Ombeni nanyi mtapewa! Haikuandikwa muombe mazuri tu!
 
Tupe source ya hii taarifa then tuanzie hapo. Besides that mnapaswa muelewe wazungu tumewashika pabaya...kilichobaki ni kutaka kutuvuruga kupitia machagadema. Mungu yupo upande wetu na kamwe hatuvurugiki. Tunazo taarifa za vikao vyao na tundu lisu huko ubelgiji....hahaha endeleeni kujitekenya tu. Mbona hawaongelei demokrasia ya China?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…