January Makamba: amegawa simu, anakula matapishi yake

January Makamba: amegawa simu, anakula matapishi yake

Makamba mwivi, 96,600,000/= kwa hali ya kuvuja jasho huwezi kuzirusha sandakalawe, kwa kazi gani anayoifanya!!!???!??!!!
 
Bestee habari za siku bwana.
Hebu nielimishe hapo tafadhali...kuna wakuu wa wilaya walioteuliwa na chadema? Manake nilidhani rais wangu mpendwa ndo anachagua hawa watu 'muhimu'?
-

- Kumbe Ukuu wako wa Wilaya umeupata kwa kujipendekeza huko Chadema? ha1 ha! ha!

Le Mutuz
 
TOTALY DISQUALIFICATIONS AND IT DISCOURIAGE THE MEANS FUTURE OF "ENERGITIC YOUNG CLEAN EDUCATED FOR FUTURE LEADERSHIP"MLIMAU HAUWEZI KUTOA EMBE,we laymans where? to go now!where? is our prosperities & destiny
 
Mimi huwa sipendi majungu, udaku na pia hii dhana ya kwamba kila tajiri nchini Tanzania ni mwizi na fisadi lakini vile vile Matajiri nao wangewatendea haki watu kama mimi kwa kuwa wawazi katika kazi, biashara na utajiri wao.

Wazungu wanaposema "There ain't no such thing as a free lunch" wanakuwa na maana nzito. Kama kweli Mh. Makamba Jn anasimama kwenye dhana ya ukweli na uwazi basi ni lazima AUFUTE usemi huo kwa kuwaeleza wananchi ni kina nani walifanikisha hii kitu anayoita 'Kaharambee kadogo' pale aliposema,


"kaharambee kadogo" ka kupatikana kama inavyodai simu zipatazo 138 zenye dhamani ya Ths 96,600,000 siyo kadogo kwa macho ya wananchi wengi ambao ni walalahoi nchini. Inahitaji maelezo na pia siyo kitu cha kuficha kama waliofanikisha "kaharambee kadogo" ni watu halali na wametoa kwa uhalali ndani ya moyo kama wa masaritan wa enzi za biblia walivyokuwa wanafanya kule Samaria.

Nje ya hivyo, tutaendelea kujiuliza maswali mengi yenye sintofahamu zenye mitazamo hasi kulingana na nafasi yake katika jamii na serikali.

Kuna tatizo la kimfumo Tanzania ya namna ya viongozi kujitenganisha na mgongano wa kimaslahi na hii ni hatari kwa usalama wa nchi na ustawi wa jamii pana. Lowasa anachangia pesa lukuki kwenye harambe mbalimbali makanisani, watu wakihoji hizo pesa anazitoa wapi yeye anasema ni msaada kutoka kwa marafiki zake na kwamba yeye ana watu wengine wana vitu. Makamba junior na yeye ameanza, makampuni ya simu yaliyo chini ya wizara yake yanampa ofa kabambe yeye anadai ni kaharambe kadogo kutoka makada wenzake. Haiingii akilini! Viongozi wataitumbukiza nchi hii kwenye giza kwa tamaa ya utajiri na madaraka.
 
W.J Malecela, watu hawahoji juu ya simu, hela za kukunulia simu hizo kapata wapi? maana kutoa 105 Million, lazima uwe na ziada, maana hiyo tun-assume ni 10% ya ulichonacho! sasa huoni sisi wengine masikini, tusiojua hata kesho tutakula nini ndio tunashaaanga?

- Ungonyesha alipoiba hizo simu ungekwua na hoja nzito, otheerwise ni majungu kama kawaida yenu umri wa Januari hauruhusu kugombea urais, yaani huna facts wala dataz poleni sana!!!

Le Mutuz
 
le mutuz unajidhalilisha mtu wangu!! Kuwa muwaz tu unafiki hautakusaidia, MAKAMBA AMETOA WAP MIL 105!
 
Mi kinachonishangaza ni kubisha ili kujionesha wewe umezaliwa ukazikuta pesa home, ila hujui uchungu wa kutafta coz baba(mzee malecela) ashakutafutia, come to the point, 105 tsh milioni unasema umefanya "kaharambee kadogo"? Come to think ameipata wapi? Kama anafanya kazi halali
 
- Yaaap tumejionea kweli jinsi Mkurugenzi wa kampuni ya kigeni nchini kama vodacom anavyotakiwa kuishi, sio kama mkulima wa kijijini halafu next time lete picha za nyumbani kwa MWenyekiti wa Chadema na Katibu Mkuu wa Chadema tuone kama wanafanana na wananchi wanaodai wanataka kuwakomboa!!

Le Mutuz
last time i checked CCM ni chama cha wakulima na wafanyakazi!
 
chuki Jina lako tu linasadifu haya uliyoyaandika humu,acha chuki binafsi ndugu yangu kuna tatizo gani mtu akitimiza ahadi aliyoahidi?
Anyway chuki binafsi haifai,mi nilitegemea ungekuja na hoja yakuwakumbusha viongozi wa chama chako wakatimize ahadi walizomwahidi mjane wa mwangosi.
 
Last edited by a moderator:
Watu tunahangaika na maisha ya wenzetu huku ndugu zetu wanakufa njaa.
 
Jina lako tu linasadifu haya uliyoyaandika humu,acha chuki binafsi ndugu yangu kuna tatizo gani mtu akitimiza ahadi aliyoahidi?
Anyway chuki binafsi haifai,mi nilitegemea ungekuja na hoja yakuwakumbusha viongozi wa chama chako wakatimize ahadi walizomwahidi mjane wa mwangosi.

Mama Mwigulu, kumbe hupo , umeshajifungua......?
 
Tanzania yetu na kila mwenye kupewa mamlaka ni lazima afanye dhihaka kama si matusi kwa wananchi anaowaongoza au waliomchagua.
 
- Ilishatihibitishwa siku nyingi sana kwamba hizi barua ni za uongo fake zimetengenezwa na watu, so ni batili na zinahusiana nini na kichwa cha mada hii?

Le Mutuz

Laiti kama Le Mutuz ungekuwa umeishi maisha ya yule mtoto wa kule Mtera kijijini haya maneno unayoyasema usingeyarudia hata kidogo. infact you stand for truth which is you belong to the life of Makambas and family and not poor and poorest Tanzania. Wala sikushituka ulipojitosha kutetea watu unaolingana nao kiitikadi na maisha. You cant be friend with poor nor defend them. Kwani hujaishi maisha kama hayo (umaskini). Umazaliwa ndani ya faraja na utakufia humo!! Kama Makamba kafanya hayo aliyoyafanya nje na msimamo wake na kile anachokiamini basi amepotoka..na huyo Dada wa Makamba i know her from long time..she is what she is!!
 
Atajuta huyo.hata jk angegombea angeshindwa itakuwa yeye?atunze hela yake ili imsaidie ccm itakapofurushwa madarakani kwa kura 2015
 
jina lako tu linasadifu haya uliyoyaandika humu,acha chuki binafsi ndugu yangu kuna tatizo gani mtu akitimiza ahadi aliyoahidi?
Anyway chuki binafsi haifai,mi nilitegemea ungekuja na hoja yakuwakumbusha viongozi wa chama chako wakatimize ahadi walizomwahidi mjane wa mwangosi.
mbona hujielewi?au ndo mtindikio wa mawazo unakutesa?nani kakwambia huyo ni mwanachama wa chama cha siasa?is that the best you can think?japo umesoma udsm lakini nahisi umekuwa kama ngombe aliyepita kwenye josho lisilo na dawa akatoka na kupe walewale.
 
Mzee W.J. Malecela, umeshaharibu mwelekeo wa hii mada, kwa kutetea ujinga!
 
Makamba January simuamini hata kidogo na hasa baba yake anapodai Lowassa ni jembe....----!
 
This issue is controversial tusimsulubu jm ilhali nchi nzima imejaa ufisadi,sioni penye nafuu.kama walala hoi wenyewe wanataka rushwa ili wakupe kura, wanatuchagulia viongozi wa aina gani,tafakari chukua tahadhari.
 
chuki - Ungonyesha alipoiba hizo simu ungekwua na hoja nzito, otheerwise ni majungu kama kawaida yenu umri wa Januari hauruhusu kugombea urais, yaani huna facts wala dataz poleni sana!!!

Le Mutuz

mkuu wewe ndio hauna fact.January makamba amezaliwa 28/01/74 hivyo mwaka 2015 atakuwa na umri wa miaka 41,kwa maana hiyo hata umri wa kugombea ukibaki kama ule wa zamani (40),au ukirudishwa nyuma letsay (35) bado ataweza kugombea.
I stand to be corrected
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom