Ng'wanza Madaso
JF-Expert Member
- Oct 21, 2008
- 2,268
- 333
Wakati huo huo Kamati ya Bunge inayoshughulikia Nishati na Madini imelazimika kuanza kazi mapema kutokana na makali ya mgao wa umeme.
Akizungumza na waandishi wa habari kwenye moja ya ofisi za Bunge mjini Dodoma jana, Mwenyekiti wa Kamati hiyo January Makamba alisema lengo ni kubaini kwa haraka sababu za kukosekana kwa umeme nchini.
Makamba ambaye ni Mbunge wa Bumbuli kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), alisema kesho wajumbe wa kamati hiyo watakwenda Mtera kutizama hali halisi ya uzalishaji umeme kutoka kwenye chanzo hicho.
Akizungumzia safari hiyo alisema imegharamiwa na ofisi za Bunge ingawa awali ziara za namna hiyo zilikuwa zikigharamiwa na serikali kupitia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO).
January alisema baada ya kupitia taarifa zilizopita za kamati hiyo, aligundua kuwepo kwa bahasha za mlo wa mchana kwa kila mjumbe wa kamati ambazo ndani yake kunakuwa na shilingi milioni moja hivyo aliwaomba wajumbe wa kamati yake kuzikataa.
"Baada ya kupitia taarifa zile tumeona kuwa wajumbe wa kamati walikuwa wakienda kwenye ziara kama hivyo hupewa bahasha za ‘lunch' ambazo ndani yake kunakuwa na sh milioni moja sasa nimewaomba wajumbe wenzangu tusizikubali… safari hii tutagharamiwa na Ofisi ya Bunge," alisema January.
Kwa habari kamili soma hapa: http://www.freemedia.co.tz/daima/habari.php?id=23734
Akizungumza na waandishi wa habari kwenye moja ya ofisi za Bunge mjini Dodoma jana, Mwenyekiti wa Kamati hiyo January Makamba alisema lengo ni kubaini kwa haraka sababu za kukosekana kwa umeme nchini.
Makamba ambaye ni Mbunge wa Bumbuli kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), alisema kesho wajumbe wa kamati hiyo watakwenda Mtera kutizama hali halisi ya uzalishaji umeme kutoka kwenye chanzo hicho.
Akizungumzia safari hiyo alisema imegharamiwa na ofisi za Bunge ingawa awali ziara za namna hiyo zilikuwa zikigharamiwa na serikali kupitia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO).
January alisema baada ya kupitia taarifa zilizopita za kamati hiyo, aligundua kuwepo kwa bahasha za mlo wa mchana kwa kila mjumbe wa kamati ambazo ndani yake kunakuwa na shilingi milioni moja hivyo aliwaomba wajumbe wa kamati yake kuzikataa.
"Baada ya kupitia taarifa zile tumeona kuwa wajumbe wa kamati walikuwa wakienda kwenye ziara kama hivyo hupewa bahasha za ‘lunch' ambazo ndani yake kunakuwa na sh milioni moja sasa nimewaomba wajumbe wenzangu tusizikubali… safari hii tutagharamiwa na Ofisi ya Bunge," alisema January.
Kwa habari kamili soma hapa: http://www.freemedia.co.tz/daima/habari.php?id=23734