Fidel80
JF-Expert Member
- May 3, 2008
- 21,947
- 4,444
Na Charles Mwakipesile, Ileje
WASAIDIZI wa Rais Jakaya Kikwete jana walinurika kufa katika ajali Mbaya baada ya gari walilokuwa wakisafiria kupasuka gurudumu la nyuma kushoto na gari hilo kuacha njia na kuserereka kwenye korongo.
Ajali hiyo ilitokea saa tano asubuhi katika kijiji cha Ikinga, Wilaya ya Ileje wakati msafara huo ukitoka Kyela kuelekea Shule ya sekondari ya Isange, mahali ambapo Rais Kikwete alitarajia kupokea taarifa ya wilaya na kuweka jiwe la msingi kwenye sekondari hiyo.
Gari hilo Toyota Landcruser lenye namba za usajili STK 3264 likiendeshwa na dereva Peter Makwale, liliacha njia likiwa katika mwendo mkali na kutumbua kwenye korongo lililokuwa jirani na makazi ya watu lakini hata hivyo halikupata madhara na lilisimama kama vile lipo barabarani.
Wasaidizi hao wa Rais wakiongozwa na January Makamba,walitoka salama bila majeraha yoyote na kuendelea na safari baada ya kupatiwa gari lingine Toyota Land Cruser namba STK 4744.
Akizungumza baada ya ajali hiyo, Makamba alimshukuru Mungu kwa kuwanusuru kwenye balaa hilo na kusema bila huruma zake, hali ingekuwa mbaya .
Naye dereva Makwale, alisema alijitahidi kuhakikisha analimudu gari hilo lakini kutokana na vumbi lililotanda barabarani na kupasuka gurudumu, alishangaa kujikuta amepaa na kutua kwenye korongo kubwa.
Kamanda wa Polisi mkoani Mbeya, Zelotte Steven alithibitisha kutokea kwa ajali hiyo ambayo hata hivyo, alisema wasaidizi hao wote walitoka salama na kuendelea na safari.
WASAIDIZI wa Rais Jakaya Kikwete jana walinurika kufa katika ajali Mbaya baada ya gari walilokuwa wakisafiria kupasuka gurudumu la nyuma kushoto na gari hilo kuacha njia na kuserereka kwenye korongo.
Ajali hiyo ilitokea saa tano asubuhi katika kijiji cha Ikinga, Wilaya ya Ileje wakati msafara huo ukitoka Kyela kuelekea Shule ya sekondari ya Isange, mahali ambapo Rais Kikwete alitarajia kupokea taarifa ya wilaya na kuweka jiwe la msingi kwenye sekondari hiyo.
Gari hilo Toyota Landcruser lenye namba za usajili STK 3264 likiendeshwa na dereva Peter Makwale, liliacha njia likiwa katika mwendo mkali na kutumbua kwenye korongo lililokuwa jirani na makazi ya watu lakini hata hivyo halikupata madhara na lilisimama kama vile lipo barabarani.
Wasaidizi hao wa Rais wakiongozwa na January Makamba,walitoka salama bila majeraha yoyote na kuendelea na safari baada ya kupatiwa gari lingine Toyota Land Cruser namba STK 4744.
Akizungumza baada ya ajali hiyo, Makamba alimshukuru Mungu kwa kuwanusuru kwenye balaa hilo na kusema bila huruma zake, hali ingekuwa mbaya .
Naye dereva Makwale, alisema alijitahidi kuhakikisha analimudu gari hilo lakini kutokana na vumbi lililotanda barabarani na kupasuka gurudumu, alishangaa kujikuta amepaa na kutua kwenye korongo kubwa.
Kamanda wa Polisi mkoani Mbeya, Zelotte Steven alithibitisha kutokea kwa ajali hiyo ambayo hata hivyo, alisema wasaidizi hao wote walitoka salama na kuendelea na safari.