kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 17,407
- 17,014
Siku zote nilikuwa nikijiuliza maswali mengi kichwani bila kupata majibu yake kuhusu ni kwa vipi nchi kama Burundi yenye migogoro mingi ya kiusalama inawezeje kutoa wanajeshi wake wengi kwenda kuzisaidia nchi nyingine kurejesha amani yao badala ya kusalia nchini mwao kuimarisha amani ya nchi yao kwanza?
Kumbe nchi hizi huwa zinafaidika sana kwa kupitia mishahara wanayolipwa wanajeshi wao na UN au EU. Serikali hizi zinalazimisha mishahara ya wanajeshi wao ilipwe kupitia serikali za nchi zao ili 'kuipiga panga' kwanza kabla haijawafikia walengwa.
Inasemekana UN na EU inawalipa wanajeshi wa kulinda amani takribani mara 26 zaidi ya mishahara ya Burundi kwa US dollar.
Baada ya UN na EU sasa kung'amua janja hii na kutaka kuwalipa wanajeshi wenyewe moja kwa moja mifukoni mwa, weeee!, jamaa sasa wanatishia kuwarudisha nyumbani wanajeshi wao kwakuwa haitakuwa na maana kwao tena.
Huu ni unyonyaji wa hali ya juu kwa watoto wa watu kugeuzwa kitega uchumi na wanasiasa.
Kumbe nchi hizi huwa zinafaidika sana kwa kupitia mishahara wanayolipwa wanajeshi wao na UN au EU. Serikali hizi zinalazimisha mishahara ya wanajeshi wao ilipwe kupitia serikali za nchi zao ili 'kuipiga panga' kwanza kabla haijawafikia walengwa.
Inasemekana UN na EU inawalipa wanajeshi wa kulinda amani takribani mara 26 zaidi ya mishahara ya Burundi kwa US dollar.
Baada ya UN na EU sasa kung'amua janja hii na kutaka kuwalipa wanajeshi wenyewe moja kwa moja mifukoni mwa, weeee!, jamaa sasa wanatishia kuwarudisha nyumbani wanajeshi wao kwakuwa haitakuwa na maana kwao tena.
Huu ni unyonyaji wa hali ya juu kwa watoto wa watu kugeuzwa kitega uchumi na wanasiasa.