Jangwani: Lissu amenisikitisha!

Jangwani: Lissu amenisikitisha!

Nilikuwa nasikiliza hotuba za vyama vilivyoungana dhidi ya chama tawala sasa hivi lakini imebidi nizime radio na kuelekea kwenye kanywaji, kwa vile sikuweza kuvumilia derogatory language ya huyu Mh. Tundu Lissu.

Katika kueleza mchakato wa yale yaliyojiri alikuwa akitamka, tena bila aibu, staha wala ustaarabu kuwa amekuwa akiongea na miCCM, maCCM na kwa ujumla kwa kutmia lugha isiyostahili kwa mtu msomi, tena aliyeheshimiwa kupewa dhamana ya kuingia bungeni kwawakilisha wananchi kwa kupitia jimbo lake la uchaguzi.

Pengine Msajili wa Vyama inabidi amkumbushe huyu jamaa kuwa derogatory language haijengi na yule uliyemkusudia akiamua kurudisha matusi basi amani inaweza kuwekwa rehani.

Kwa mtaji huu , Lissu anaingia katika wanasiasa wasio na ustaarabu wa kuelezea yale yaliyo moyoni bila kutumia dharau, matusi n.k.

No wonder humu JF , si ajabu yeye ni mmoja wa wanaoutumia matusi kujieleza.
Nawasilisha.

ulitaka ayaiteje haya makitu? including you.
 
Mamndenyi,hata wewe unatumia KIROBA?JINA ZURI LA CCM NI MAGAMBA!
 
Lissu is very logic kaka. Hawezi kuisifu ccm hata kidogo. Nimeipenda Sana logical presentation yake.
 
Hili na lile la serukamba bungeni tena wakati luninga na redio zinarusha live hewani lipi la kusikitisha?
 
Nyeusi iitwe nyeusi,let a spade be called a spade!Ulitaka waitwe nini au hukumbuki wanaKigoma walivyosema...CDM ni chama cha wakristo,...CUF ni chama cha waislamu..CCM ni chama cha SHETANI.Tundu amewapa haki yao ingawaje ni chungu kumeza lakini inatibu...leave pi as pi.
 
Nilikuwa nasikiliza hotuba za vyama vilivyoungana dhidi ya chama tawala sasa hivi lakini imebidi nizime radio na kuelekea kwenye kanywaji, kwa vile sikuweza kuvumilia derogatory language ya huyu Mh. Tundu Lissu.

Katika kueleza mchakato wa yale yaliyojiri alikuwa akitamka, tena bila aibu, staha wala ustaarabu kuwa amekuwa akiongea na miCCM, maCCM na kwa ujumla kwa kutmia lugha isiyostahili kwa mtu msomi, tena aliyeheshimiwa kupewa dhamana ya kuingia bungeni kwawakilisha wananchi kwa kupitia jimbo lake la uchaguzi.

Pengine Msajili wa Vyama inabidi amkumbushe huyu jamaa kuwa derogatory language haijengi na yule uliyemkusudia akiamua kurudisha matusi basi amani inaweza kuwekwa rehani.

Kwa mtaji huu , Lissu anaingia katika wanasiasa wasio na ustaarabu wa kuelezea yale yaliyo moyoni bila kutumia dharau, matusi n.k.

No wonder humu JF , si ajabu yeye ni mmoja wa wanaoutumia matusi kujieleza.
Nawasilisha.

Kitu kibaya ni kibaya tu hata ukikipamba vipi, CCM ni chama kibaya kinasimamia ufisadi, rushwa, ukatili dhidi ya raia, kufilisi raslimali za taifa, dawa za kulevya, kuua Tembo wetu nk nk. Lissu yuko sahihi kuwaita MiCCM na MaCCM. Kwa hiyo disapointment yako iko misplaced! Pole
 
maccm hayastahili lugha ya staha hata kidogo! Kwanza TL katumia lugha ya staha sana... Maccm yanastahili matusi tena ya nguoni
 
Tundu Lissu hana nidhamu kabisa.
Acha aseme hivyo. Ukweli CCM wanaudhi sana hasa wanapotaka kuteka kwa wazi mchakato wa katiba na huku tayari tumejua ile wanayotaka inafananaje! Hawatutakii mema Watanzania!!
 
Kuna tusi zaidi ya kumwita kiongozi wenzako "waongo, wanafiki na wazandiki hadharani" ? MiCCM na MaCCM ni lugha ya kuonyesha kuwa ni watu wasiopenda kubadilika kama CHUMA. Big up Lissu
 
sasa hapo kuna tusi? wewe uliona wapi lissu akiwaita ccm? yeye utumia maccm hata mie nawaita maccm hakuna kosa hapok

Ta Ruttashoborolwa ninkwikiliza na mimi nayaita the same way MASISIEM,MISISIEM,GASISIEM!!!
Kuna haja gani ya kuyastahi magamba,mwosha huoshwa.
 
Tunajadili nini hapa wakati LiCCM Lililoleta hoja limesema limeenda kilabuni....!
 
Pole sana, kama matusi ya wabunge wa utawala wanavyorusha matus dhid upande mwingine na huyaoni badala yake neno ma ccm ndo limekufanya uzime redio. Na kwa hali hiyo utoe kabisa betri kwenye redio ili ubaki hivyohivyo ulivyo

Aliona kwenye redio hafaidi vizuri akaamua kwenda kilabuni kudoea tv huku akikamua Rider..!
 
Dung'unyi tumemchoka Tundu Lissu, hakuna maendeleo aliyotuletea mpaka sasa zaidi ya kumzuia ndugu na aliyekuwa mpinzani wake kuunganisha huduma ya umeme kwenye shule za kata Dung'unyi. Hata Kanisa Katoloki Parokia ya Dun'unyi wamemchoka. Ile ladha ya kujifanya anatuhadaa na kesi za vitalu vya madini kwenye kiwanja cha Kanisa imeshaisha. Lissu sio mdini bali ni mtumia dini kuhadaa wanyampaa. Nawaambia atakiona 2015, labda aje na usanii mwingine tofauti na kutuma watoto wa chekechea kuchana picha za Njau.
labda atakoa kura yako tu!
 
Back
Top Bottom