Jangwani: Lissu amenisikitisha!

Jangwani: Lissu amenisikitisha!

Nilikuwa nasikiliza hotuba za vyama vilivyoungana dhidi ya chama tawala sasa hivi lakini imebidi nizime radio na kuelekea kwenye kanywaji, kwa vile sikuweza kuvumilia derogatory language ya huyu Mh. Tundu Lissu.

Katika kueleza mchakato wa yale yaliyojiri alikuwa akitamka, tena bila aibu, staha wala ustaarabu kuwa amekuwa akiongea na miCCM, maCCM na kwa ujumla kwa kutmia lugha isiyostahili kwa mtu msomi, tena aliyeheshimiwa kupewa dhamana ya kuingia bungeni kwawakilisha wananchi kwa kupitia jimbo lake la uchaguzi.

Pengine Msajili wa Vyama inabidi amkumbushe huyu jamaa kuwa derogatory language haijengi na yule uliyemkusudia akiamua kurudisha matusi basi amani inaweza kuwekwa rehani.

Kwa mtaji huu , Lissu anaingia katika wanasiasa wasio na ustaarabu wa kuelezea yale yaliyo moyoni bila kutumia dharau, matusi n.k.

No wonder humu JF , si ajabu yeye ni mmoja wa wanaoutumia matusi kujieleza.
Nawasilisha.

Na mimi naendela kukuambia ni ujinga kuendelea kuyashabikia maCCM, ebu naomba nikuulize pale mwigulu alipotamka kuwa haongei na Mbwa anaongea na Mfuga Mbwa, na isitoshe huyohuyo Mwigulu wakati ule Kafumu ametangazwa kushinda ubunge kule Igunga alitamka hadharani kuwa CCM wamepiga Mbwa na Mfuga Mbwa na baada ya hapo akaenda Iramba akamvesha Mbwa Bendera ya CHADEMA katika matukio haya wewe unayejifanya kuguswa sana na kauli zisizo za Kistaarabu kuna chochote ulichangia kupinga haya aliyoyafanya Mwigulu?
 
Dung'unyi tumemchoka Tundu Lissu, hakuna maendeleo aliyotuletea mpaka sasa zaidi ya kumzuia ndugu na aliyekuwa mpinzani wake kuunganisha huduma ya umeme kwenye shule za kata Dung'unyi. Hata Kanisa Katoloki Parokia ya Dun'unyi wamemchoka. Ile ladha ya kujifanya anatuhadaa na kesi za vitalu vya madini kwenye kiwanja cha Kanisa imeshaisha. Lissu sio mdini bali ni mtumia dini kuhadaa wanyampaa. Nawaambia atakiona 2015, labda aje na usanii mwingine tofauti na kutuma watoto wa chekechea kuchana picha za Njau.

Jimboni kwetu huku kwa mwingula tunamtamani sana dah lazima tumpe jimbo
 
Pole sana, kama matusi ya wabunge wa utawala wanavyorusha matus dhid upande mwingine na huyaoni badala yake neno ma ccm ndo limekufanya uzime redio. Na kwa hali hiyo utoe kabisa betri kwenye redio ili ubaki hivyohivyo ulivyo
 
Umeishia kukandia pasipokueleza baya alilofanya
 
Nimehuzunika sana. Ninawaonea huruma wananchi wa jimbo lake.
 
maandamano vipi?.au ilikuwa ni nguvu ya viroba.
 
Ona huyu nae, ccm ni maadui wa watanzania, unataka tuwaite kwa jina lipi...tuite lovely ccm?, bandiko lako halina mashiko, hapa unalalamika tu...ni maccm bana, usituchaguliwe namna ya kuwaiteni kama mmeshajichafua, kama mnatufanya maskini,fukara, wajinga, mnabakiza watanzania kesi, mnatulipua mabomu, manatumwagia tindikali, mnauza mdini yetu, manafanya ujangili na kuuza mihadarati sasa tuwaiteje?...


Kuitwa hivo inawapa fulsa ya kujitathimini sifa na weledi wenu kwa watanzania kwa sasa..
 
Nimehuzunika sana. Ninawaonea huruma wananchi wa jimbo lake.
Pale wamentambulisha kama mtaalam na mwanasheria wa katiba, lakini sikuona utaalam wala uanasheria.
Ni kama Sugu tu na si vinginevyo.
 
Ona huyu nae, ccm ni maadui wa watanzania, unataka tuwaite kwa jina lipi...tuite lovely ccm?, bandiko lako halina mashiko, hapa unalalamika tu...ni maccm bana, usituchaguliwe namna ya kuwaiteni kama mmeshajichafua, kama mnatufanya maskini,fukara, wajinga, mnabakiza watanzania kesi, mnatulipua mabomu, manatumwagia tindikali, mnauza mdini yetu, manafanya ujangili na kuuza mihadarati sasa tuwaiteje?...


Kuitwa hivo inawapa fulsa ya kujitathimini sifa na weledi wenu kwa watanzania kwa sasa..

bado hamjalijua somo la DEMOKRASIA. hoja yenye nguvu haiitaji kejeli. namna utavyo ijenga itatosha kueleweka.
 
Dah! Nilikuwa nasoma hili bandiko kwa hofu mno nikiwa na udadisi wa makosa ya lissu. Kumbe ni kuhusu maccm? Hofu imeisha
 
Back
Top Bottom