Mfalme_wa_Nyika
JF-Expert Member
- May 24, 2023
- 391
- 859
Ukisikia kama kuna pepo la magonjwa linampango wa kukuandama nakukuangamiza nadhani ndio huku.....
Wakuu na madaktari wa jf nawapa heshima zenu wasalaam....niende kwenye mada...
Takribani wiki mbili zilizopita nimetoka kumaliza kutumia dawa za PEP hii ni baada yakufanya mapenzi na na binti ambaye baadae niligua ni muathirika wa ukimwi, Mungu anasaidia hii ni wiki takribani ya saba toka kile kitendo na nimepima majibu yangu ni NEGATIVE.
Kiukweli hakuna kipindi kigumu nilipitia kama kipindi hiko chakumeza ile midawa ya PEP na kipindi hiki kwa ujumla kujua hatma yangu stress level iko juu sana.
Nimekuwa nikiishi kwa hofu mno kipindi hiki cha takribani miezi miwili, sasa leo nilitaka kwenda kufanya kipimo cha full blood picture ila nilipoanza kupimwa tu pressure na uzito niliamua kuahirisha mengine nirudi nyumbani kutafakari.
Nimepimwa nimekutwa na pressure ya 140/90 na uzito umeongezeka toka kilo 68 mpaka kilo 79, kitu ambacho sio kawaida yangu, mara ya mwisho niliendaga hospitali takribani miezi mitatu na sikuwahi kuambiwa nina pressure na uzito wangu mara nyingi unacheza 68 ikizidi sana 70 kg.
Naombeni ushauri wenu naogopa kuwa mtu wa hypertension nifanyeje!? Ukiniona niko kawaida kabisa, mimi situmii pombe, sigara wala kusema kula chumvi sio kivile sana na nina miaka 33 tu, pia ni mtu sana wa mazoezi, ni kwamba baada yakupata janga la kufanya mapenzi muathirika maisha yangu yakawa shaghala bagala miezi ya hivi karibuni niko na hofu na mapigo ya moyo hayako vizuri.
Nawaza hii pressure ya 140 kwa 90 nimeitoa wapi!? Na je ninawezaje kuwa normal nifanyaje!? Daktari aliniambia hii sio issue sana ingawa ni hatua za awali kuwa naweza kuwa mtu wa pressure, kimoyomoyo nikasema ananipa moyo tu, mimi naogopa....
Nawaza nirudi nyumbani niague mizimu maana naona kams majanga yananifata, la ukimwi ndio hilo Mungu anapambania, sasa hili la pressure ndio linanipa pressure kabisa maana najuta kufahamu najuta kwenda hospitali kujua naona ndio nazidi kuwaza tatizo.
Naombeni ushauri na mawazo....
Asanteni
Wakuu na madaktari wa jf nawapa heshima zenu wasalaam....niende kwenye mada...
Takribani wiki mbili zilizopita nimetoka kumaliza kutumia dawa za PEP hii ni baada yakufanya mapenzi na na binti ambaye baadae niligua ni muathirika wa ukimwi, Mungu anasaidia hii ni wiki takribani ya saba toka kile kitendo na nimepima majibu yangu ni NEGATIVE.
Kiukweli hakuna kipindi kigumu nilipitia kama kipindi hiko chakumeza ile midawa ya PEP na kipindi hiki kwa ujumla kujua hatma yangu stress level iko juu sana.
Nimekuwa nikiishi kwa hofu mno kipindi hiki cha takribani miezi miwili, sasa leo nilitaka kwenda kufanya kipimo cha full blood picture ila nilipoanza kupimwa tu pressure na uzito niliamua kuahirisha mengine nirudi nyumbani kutafakari.
Nimepimwa nimekutwa na pressure ya 140/90 na uzito umeongezeka toka kilo 68 mpaka kilo 79, kitu ambacho sio kawaida yangu, mara ya mwisho niliendaga hospitali takribani miezi mitatu na sikuwahi kuambiwa nina pressure na uzito wangu mara nyingi unacheza 68 ikizidi sana 70 kg.
Naombeni ushauri wenu naogopa kuwa mtu wa hypertension nifanyeje!? Ukiniona niko kawaida kabisa, mimi situmii pombe, sigara wala kusema kula chumvi sio kivile sana na nina miaka 33 tu, pia ni mtu sana wa mazoezi, ni kwamba baada yakupata janga la kufanya mapenzi muathirika maisha yangu yakawa shaghala bagala miezi ya hivi karibuni niko na hofu na mapigo ya moyo hayako vizuri.
Nawaza hii pressure ya 140 kwa 90 nimeitoa wapi!? Na je ninawezaje kuwa normal nifanyaje!? Daktari aliniambia hii sio issue sana ingawa ni hatua za awali kuwa naweza kuwa mtu wa pressure, kimoyomoyo nikasema ananipa moyo tu, mimi naogopa....
Nawaza nirudi nyumbani niague mizimu maana naona kams majanga yananifata, la ukimwi ndio hilo Mungu anapambania, sasa hili la pressure ndio linanipa pressure kabisa maana najuta kufahamu najuta kwenda hospitali kujua naona ndio nazidi kuwaza tatizo.
Naombeni ushauri na mawazo....
Asanteni