DuaZaMama
JF-Expert Member
- Jun 2, 2025
- 1,882
- 4,129
Mwenyekiti wa Ngome ya Wanawake wa ACT Wazalendo Janeth Rithe, amewaambia wakazi wa Jimbo la Tunduru Kusini Wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma, kuwa wasitegemee kupata huduma bora za afya kwakuwa Chama Cha Mapinduzi hakijali matatizo ya wananchi hivyo dawa pekee ya kuboresha huduma zote za kijamii ni kukiweka Chama hicho pembeni na kukichagua Chama cha ACT Wazalendo kama suluhisho la matatizo yote ya wananchi hasa wenye kipato cha chini.