JamiiForums Users Music Award..

JamiiForums Users Music Award..

Benny

JF-Expert Member
Joined
Jun 6, 2014
Posts
3,275
Reaction score
5,415
Habari wakuu!

Tanzania tulikua na Kili Music Award ambazo zimekua na changamoto nyingi ila bado ni tunzo ambazo ziliwatia moyo sana wanamuziki wa hapa nyumbani.

Nimepata wazo sisi kama jumuiko dogo la watumiaji wa Jamii Forum tunaweza kuanzisha jambo dogo pia hapa kwa lengo la kutoa heshima kwa wanamuziki na kazi za muziki zilizofanya vizuri "kila mwaka" hatuwezi kuandaa tamasha kubwa la utoaji tunzo ila kwa bandiko kama hili litabaki hapa milele na milele kuonyesha nani aliwahi kufanya vizuri mwaka flani na itakua heshima kwake na kwa kila aliyeshiriki kuandaa hili.

Kwa kuanza nakaribisha mawazo kwa kila mdau kama litapokelewa vizuri.

Tunaweza kuandaa vipengele vichache sana na kupigia kura hapa na kutangaza washindi wetu kwa muda usiozidi miezi miwili tu yaani siku 60.

Pia ili kuepusha mkanganyiko tunaweza kuangazia kazi zilizotolewa miezi kumi au tisa tu iliyopita na baada utaratibu wa upigaji kura (kama tutafika huko) kupata na kutangaza zilizo bora tutasubiri tena kuangazia zitakazotoka kwa miezi kumi inayofuata.

Binafsi sina maslahi wala lengo lolote lilijificha juu ya jambo hili bali tu nia njema tu na upenzi wangu mdogo wa burudani na maendeleo ya muziki wa hapo nyumbani.

Kwa kua jambo hili ni kwa ajili ya watumiaji wa mtandao huu litahususha wale tu watakaopenda kushiriki na pia tutaheshimu sana ambao hawatapenda kushiriki (sio wote wapenzi wa muziki)na litakapokubalika basi na libaki kuwa letu halitahusiahwa na maslahi ya mtu yoyote binafsi humu au kikundi kidogo cha watu.
 
Wazo zuri sana lkn tatizo litakuja kwny hizi timu maana wengine watakuwa wanapiga kura kukomoana
 
Ni wazo zuri Benny.

Kwa hiyo hapatakuwa na zawadi wala tuzo yoyote? Ni kupiga kura tu na kuorodhesha majina?
Karibu Boss

tunaanza hivyo bila zawadi tutatangaza washindi hapa kwa kuorodhesha mbeleni huko tunaweza kuwa na chochote
 
Wazo zuri sana lkn tatizo litakuja kwny hizi timu maana wengine watakuwa wanapiga kura kukomoana
tusisitize kwamba jambo
hili halina maslahi na mtu binafsi au kikundi kidogo cha watu
 
Karibu Boss

tunaanza hivyo bila zawadi tutatangaza washindi hapa kwa kuorodhesha mbeleni huko tunaweza kuwa na chochote
Ni vizuri kwangu naunga mkono. Japo kuna changamoto zake kama.

1. U-team
2. Kuhesabu kura
3. Kuharibiwa uzi wa tuzo. Mtu kwasababu ni ID fake tu anaamua kuleta stori zingine
4. Kuvuta crowd kubwa(hili ndilo kubwa bro)
 
Wazo zuri japo changamoto ni nyingi ila inawezekana tu...

Inabid upatikane mpango mzima na watu wakupushi.....

Ata hivyo kwa kuanz tunaeza generalize labda msanii bora wa kike/kiume, Nyimbora ya mwaka, Video bora ya Mwaka, producer bora ili vpengele viwe vichache na kazi iwe rais then mbele ya safari yatakua yamezaliwa mawazo mapya zaid....

Ata hivyo
 
Naunga mkono hoja
Ila ngeomba kama ingewezekana wale wasioshirik yan wasiopenda mzik wakapgwa ban

kutochangia huo uz
Maana wataletw story zao
Za wanaa? Na mwisho wa
Sku kuharbu uz

Shida n kuwatabua
 
Naweza pata fursa kwa mara ya kwanza kupigia kura kazi ya sanaa. Wazo zuri
 
Habari wakuu!

Tanzania tulikua na Kili Music Award ambazo zimekua na changamoto nyingi ila bado ni tunzo ambazo ziliwatia moyo sana wanamuziki wa hapa nyumbani.

Nimepata wazo sisi kama jumuiko dogo la watumiaji wa Jamii Forum tunaweza kuanzisha jambo dogo pia hapa kwa lengo la kutoa heshima kwa wanamuziki na kazi za muziki zilizofanya vizuri "kila mwaka" hatuwezi kuandaa tamasha kubwa la utoaji tunzo ila kwa bandiko kama hili litabaki hapa milele na milele kuonyesha nani aliwahi kufanya vizuri mwaka flani na itakua heshima kwake na kwa kila aliyeshiriki kuandaa hili.

Kwa kuanza nakaribisha mawazo kwa kila mdau kama litapokelewa vizuri.

Tunaweza kuandaa vipengele vichache sana na kupigia kura hapa na kutangaza washindi wetu kwa muda usiozidi miezi miwili tu yaani siku 60.

Pia ili kuepusha mkanganyiko tunaweza kuangazia kazi zilizotolewa miezi kumi au tisa tu iliyopita na baada utaratibu wa upigaji kura (kama tutafika huko) kupata na kutangaza zilizo bora tutasubiri tena kuangazia zitakazotoka kwa miezi kumi inayofuata.

Binafsi sina maslahi wala lengo lolote lilijificha juu ya jambo hili bali tu nia njema tu na upenzi wangu mdogo wa burudani na maendeleo ya muziki wa hapo nyumbani.

Kwa kua jambo hili ni kwa ajili ya watumiaji wa mtandao huu litahususha wale tu watakaopenda kushiriki na pia tutaheshimu sana ambao hawatapenda kushiriki (sio wote wapenzi wa muziki)na litakapokubalika basi na libaki kuwa letu halitahusiahwa na maslahi ya mtu yoyote binafsi humu au kikundi kidogo cha watu.
Tatizo linakuja kwa wale wenye multiple IDs kupiga kura
 
wakuu vyema nipo naangalia muitikio wa wadau...
 
Good idea japo uteam unaweza kua ni changamoto kubwa sana!! Lakin pia kuna wale wenye mizaha isiyokua na msingi nao hawatakosa kujitokeza
 
jambo zuri pia litaitangaza jf..

Nitapendelea hata wasanii/nyimbo za kitambo fulani hivi nazenyewe ziwe na kitengo chake ili kuwaenzi wasanii na nyimbo za kitambo,maana hivi sasa ni matunda yale yaliyopita so nayo pia yananafasi kubwa na inastahiri kuenziwa.
 
Back
Top Bottom