- Thread starter
- #41
Mkuu miongoni mwa watu wenye akili na wewe umo, atakaesema umefanya makosa kuondoka na yeye ni akili zake.
Mwanaume unatakiwa kuwa mvumilivu lakini pia kuna uvumilivu wa kijinga.
Kwa maelezo yako hukuondoka nyumbani kwa kukwepa majukumu la ila kwa kuinusulu ndoa na familia yako pia kupuka manyanyaso ya akili na roho.
Kwa nionavyo mimi ulifanya jambo la busara kwani usingeondoka ambalo lilikuwa linajili ni kutengana na kugawana mali yenu hali ambayo ingewaweka watoto katika mazingira magumu sana.
Ushauri wangu ni kwamba endelea kuwasiliana na mkeo wasalimie watoto kila siku hata ikibidi wadanganye unafanya kazi na ukipata chochote wakumbuke uwatumie zawadi na mahitajio mengine.
Ila wakati huo ukiwa unatafuta kazi popote pale, mungu hamtupi mja wake utapata iwe arusha au hata huko Dar, baada ya kupata kazi rudi nyumbani.
nathani wewe umenielewa vizuri sana ...couz kuna watu wananishambulia hapa kua nmekwepa majukum ..sjakwepa majukum mimi nmeepusha shari maana ningekomaa pale home na wakati huo sina kitu yangeweza tokea makubwa thanks men