Blood of Jesus
JF-Expert Member
- Sep 19, 2016
- 2,955
- 5,877
Kama kichwa cha habari kinavyojieleza. Mimi kwa uzoefu wangu mdogo wa kusoma maandiko matakatifu kwa habari ya mambo ya rohoni, nimekutana na visa kadhaa vya watu ambao shetani alitaka/alitamani kuwaangamiza kwa sababu shetani aliona watu hao wakiwa wamebeba kusudi kubwa la Mungu, hivyo ibilisi huwa anataka kulifutilia mbali kusudi la Mungu.
Kwa uchache niwataje wachache.
YUSUFU - huyu shetani aliwatumia ndugu zake na Yusufu kutaka kumwangamiza. Lakini kwa vile Yusufu alikuwa amelibeba kusudi la Mungu, ndugu zake hawakufanikiwa kumuua, waliishia kumuuza Misri ambapo baadaye alikuja kuwa mtu mkubwa sana na kufanyika msaada mkubwa si kwa ndugu zake tu, bali kwa taifa zima la Israeli kwa ujumla. Huyu ndiye alieendeleza ma-Agano kati ya Mungu na Ibrahimu, Isaka na Yakobo.
MUSA - Huyu alipozaliwa tu, shetani alimuwinda amuue kupitia mfalme wa Misri (Farao). Shetani aliandaa mpango mzima wa kumuangamiza Musa kwa kutangaza kuuawa kwa watoto wote wa kiume wa Kiebrania, lakini kwa muujiza mkuu Musa alipona na kupata hifadhi katika Kasri la mfalme na akakulia kwa waliotaka kumuua. Huu ni muujiza wa Mungu. Ndiye baadaye aliyekabidhiwa Torati, na pia alipewa na Mungu jukumu la kuwatoa wana-Israeli utumwani Misri.
YESU MNAZARETI - Mara tu baada ya Yesu kuzaliwa huko Bethlehemu, shetani kama kawaida yake alitaka amwangamize Yesu kabla mpango wa Mungu juu yake kutimia. Ibilisi alimtumia Herode na akatangaza kuwaua watoto wote wa kiume wa chini ya miaka miwili. Lengo likiwa ni kumwangamiza Yesu. Jaribio hili pia lilishindikana kwa kuwa shetani hana uwezo wa kulizuia kusudi la Mungu. Na hivyo mpango wa Mungu wa kumleta Yesu ulitimia, na ulipotimia ndipo akaondoka zake.
UKIONA MTU ANAKOSWAKOSWA KUUAWA KATIKA HALI YA KUMIMINIWA RISASI NYINGI VILE UJUE SHETANI AMESHINDWA KUTIMIZA KUSUDI LAKE LA KUTAKA KUPINGANA NA KUSUDI LA MUNGU. MIPANGO YA MUNGU NI ZAIDI YA MIPANGO YA SHETANI. Ibilisi ni wa kushindwa tu siku zote.
Kwa uchache niwataje wachache.
YUSUFU - huyu shetani aliwatumia ndugu zake na Yusufu kutaka kumwangamiza. Lakini kwa vile Yusufu alikuwa amelibeba kusudi la Mungu, ndugu zake hawakufanikiwa kumuua, waliishia kumuuza Misri ambapo baadaye alikuja kuwa mtu mkubwa sana na kufanyika msaada mkubwa si kwa ndugu zake tu, bali kwa taifa zima la Israeli kwa ujumla. Huyu ndiye alieendeleza ma-Agano kati ya Mungu na Ibrahimu, Isaka na Yakobo.
MUSA - Huyu alipozaliwa tu, shetani alimuwinda amuue kupitia mfalme wa Misri (Farao). Shetani aliandaa mpango mzima wa kumuangamiza Musa kwa kutangaza kuuawa kwa watoto wote wa kiume wa Kiebrania, lakini kwa muujiza mkuu Musa alipona na kupata hifadhi katika Kasri la mfalme na akakulia kwa waliotaka kumuua. Huu ni muujiza wa Mungu. Ndiye baadaye aliyekabidhiwa Torati, na pia alipewa na Mungu jukumu la kuwatoa wana-Israeli utumwani Misri.
YESU MNAZARETI - Mara tu baada ya Yesu kuzaliwa huko Bethlehemu, shetani kama kawaida yake alitaka amwangamize Yesu kabla mpango wa Mungu juu yake kutimia. Ibilisi alimtumia Herode na akatangaza kuwaua watoto wote wa kiume wa chini ya miaka miwili. Lengo likiwa ni kumwangamiza Yesu. Jaribio hili pia lilishindikana kwa kuwa shetani hana uwezo wa kulizuia kusudi la Mungu. Na hivyo mpango wa Mungu wa kumleta Yesu ulitimia, na ulipotimia ndipo akaondoka zake.
UKIONA MTU ANAKOSWAKOSWA KUUAWA KATIKA HALI YA KUMIMINIWA RISASI NYINGI VILE UJUE SHETANI AMESHINDWA KUTIMIZA KUSUDI LAKE LA KUTAKA KUPINGANA NA KUSUDI LA MUNGU. MIPANGO YA MUNGU NI ZAIDI YA MIPANGO YA SHETANI. Ibilisi ni wa kushindwa tu siku zote.