Gharama ya taasisi kama CHADEMA kuhamia Dodoma ni zaidi ya pango la ofisi. Dar es Salaam ni Ngome ya CHADEMA kwa sababu zifuatazo
1. CHADEMA ina mtandao mkubwa unaojumuisha mikoa ya Dar es Salaam na pwani. Ngome za mikoa ya Arusha na Manyara zimeteteleka.
2. Ina majimbo matatu ya ubunge mkoa wa Dar es Salaam ambayo yamekaa kimkakati
3. Inaongoza halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam na baadhi ya manispaa
4. “Political visibility” yake ni kubwa Jiji la Dar es Salaam lenye idadi kubwa ya watu kuzidi majiji mengine
5. CHADEMA kuhamia Dodoma hakuna “political competitive advantage” kwani Dodoma ni ngome ya CCM. Ngome ya vita ya CHADEMA itakuwa ndani ya ngome ya vita ya CCM.