Jamani upweke unauma acheni tu

Jamani upweke unauma acheni tu

Waoh!
Ndio nimejichanganya kutwa nzima sasa na sahivi i am very lonely.

Ukiweza jifunze meditation na elimu ya utambuzi
Usikubali kushawishiwa ukaondoa upweke kwa bangi sigara madawa ya kulevya wala kilevi cha aina yeyote ile kwakuwa badala ya kutibu tatizo ndio utalikuza
 
ukiweza jifunze meditation na elimu ya utambuzi
usikubali kushawishiwa ukaondoa upweke kwa bangi sigara madawa ya kulevya wala kilevi cha aina yeyote ile kwakuwa badala ya kutibu tatizo ndio utalikuza

huh..!! Pole kwa ushauri mbovu.
 
Upweke ni moja ya vitu vibaya sana, hasa kwa maisha ya sahivi
 
Kabla ya kulalamikia upweke kwanza jitazame wewe mwenyewe kwanini uwe mpweke....kwanini upo mbali na watu.....??
Kwanini watu wanakutenga na kujiweka mbali nawe....??

Je hali hiyo imezuka tu hivi karibuni au upo nayo tangu zamani..?Na kama ni hivi karibuni ni kwa sababu gani....??
Ukichunguza kwa umakini utakuta jumba la upweke tunalijenga sisi wenyewe kwa kuweka uzio baina yetu na wale wanaovutiwa nasi......uzio ambao

unafanya tujione kama tupo kwenye dunia ya peke yetu....lakini tunaweza kulibomoa jumba la upweke kwa kutokea nje ya box na kubadili mtazamo wako juu ya watu...tambua kwamba kila mtu anahitaji heshima...na hakuna mkamilifu ndani ya sayari na kukosea ni sehemu ya maisha.

Jambo la msingi na busara ni kuwa mvumilivu kwa hali zote.....saidia watu kwa kadri ya uwezo wako...cheka na kila mtu....jitokeze kwenye mijumuiko ya kijamii kama vile misiba na sherehe....jishushe...

Kumbuka dunia msongamano....
 
Pendael24,

Dunia ina watu takribani billion 5 na kama upo Tanzania, nayo ina takribani ya watu 45 million... katika mazingira kama haya, hutakiwi kuwa mpweke kwa sababu ni kweli upweke unauma! Look someone you can talk to, someone who'll be there for you... someone you can share with him/her this or that! Hapa, simaanishi mpenzi coz' kwa mpenzi; mwisho wa mapenzi ni upweke mwingine, tena zaidi ya ule wa awali, utakaokufanya ujisikie kana kwamba hauna bahati wakati sio!!
 
Hapo ulipo kwani hakuna binadamu wenzako? Au unaishi porini?

Binadamu wengine wanaweza kukuongezea matatizo tu, kama mimi huwa naona bora niwe alone kuliko kukaa na wapiga majungu!!

Mtoa mada inaonekana upo iddle sana, mi mwenyewe hiyo hali huwa inanikuta nisipokuwa busy!! Tafuta vitu vya kufanya hasa vile unavyovipenda, unaweza angalia documentaries za kurikirisha, ukasikiza good music au ukajifunza program mbalimbali katika technologia i.e programming, designing!!
 
Mpweke kwani wewe mbalamwezi ishindayo angani usiku pasipo rafiki?
 
upweke unatesa sana.... heri ushinde njaaa kwenye amani kuliko upweke
 
Tena upweke wa kutokua na mwenzi
Hamna anayekujulia hali asubuhi na jion si kwa text wala call...wala wakuja kukupa company
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom