Mtambuzi mimi nataka matokeo! Ulikula au hukula? Samahani nilichelewa kuona thread hii kwani nilikuwa nafuturu chakula fulani nakulaga mimi PakaJimmy na LiverpoolFC, kinaitwa nyagi. Haya nipe taarifa!
Kulaaaaaaaaa!!!!!!!!. Kiingiacho haramu..........
Fanyeni fasta basi, nile au nisile, mwenzenu nasubiriwa kikaoni hivoo................
Mh, una hatari wewe.............
Wakuu, niko huku Masaki Chole Road karibu na tpsf, nina kikao na kampuni moja ya Wachina, sasa huyu binti wa kichina kaniandalia Chai ya kichina yaani imeungwa na tu vijani tubichi na kaniletea tuvitu flani tumekaa kama tambi lakini kama tuna vijicho halafu vikavu ananiambia ni bites za kichina na kuna tuvitu flani vimefanana na tende lakini mwe navifananisha na mende hivi.....
Mh, mwenzenu hapa nimepatikana....
Niko chooni hivi sasa naweka hii post nasubiri mnijibu kabla sijarudi kwenye kikao, yaani muafrika niko peke yangu halafu nimezungukwa na Wachina watano.
Wakuu, niko huku Masaki Chole Road karibu na tpsf, nina kikao na kampuni moja ya Wachina, sasa huyu binti wa kichina kaniandalia Chai ya kichina yaani imeungwa na tu vijani tubichi na kaniletea tuvitu flani tumekaa kama tambi lakini kama tuna vijicho halafu vikavu ananiambia ni bites za kichina na kuna tuvitu flani vimefanana na tende lakini mwe navifananisha na mende hivi.....
Mh, mwenzenu hapa nimepatikana....
Niko chooni hivi sasa naweka hii post nasubiri mnijibu kabla sijarudi kwenye kikao, yaani muafrika niko peke yangu halafu nimezungukwa na Wachina watano.
Hebu gfsonwin, watu8, Asprin, snowhite, nivea, Lisa, Eiyer, cacico, Ruttashobolwa, madamu B, Paloma, KakaKiiza, Fidel80, Filipo, Kaizer, marejesho, amu, Mungi, Preta, sweetlady, FirstLady, nyumba kubwa, BADILI TABIA, Mwita Maranya, Nyamayao lara 1 na wale wanaojua menu za kichina waje hapa kunipa maushauri kabla sijala kharamu..............