Jamani mimi sijielewi!!

Jamani mimi sijielewi!!

Una ndege wewe,,, chakufanya achana na mapenzi,,,
Mbona na mi mpole lakn nmega kama kawa!!!!!
 
Wako yupo anakuja na she is da best,chakufanya tulia acha kuanzisha mahusiano na watu moyo wako haujaridhia,badala yake sali sana umuombe Mungu atakujbu wakati umpendezao ukifika
 
Kama umesha jitambua hivyo inabidi uwe makini sana.Huenda kuta hujui jinsi ya kuongea na mwanamke ili umvute vizuri awe karibu nawe na hata mwishoe mpendane yani kila mmoja ampende mwenzie.

Inawezekana..!!
 
Kutongoza ni fani inayowashinda wengi....
 
labda unatongoza viwango visivyokuwa vyako na kwa papara..wanapoenda kuwaelezea rafk zao, marafk wanavutiwa na kuwazunguka wenzao. Fanya mambo yako kama kobe kaka, kama kafika vile kumbe anafkria njia.
 
Tatizo lako unachagua matawi ambayo siyo yako. Wewe uwezo wako Escudo Unaenda Kuchagua Prado. Huoni kuwa unavaa viatu visivyokutosha?

mweleze huyo dau lake la mia ataka elfu mbili inahuuuuuuuuuuuuuu
 
Kufunga na kuomba ni vema sana ila unatakiwa pia uombewe na mtu ambaye unadhani imani yako iko juu ambaye wewe ukiombewa naye unaaamini utafunguka pia labda kuna tabia fulani unazo ambazo huwa haziwapendezi kina dada usikate tamaa ujue siku moja itafika tu hayo yataisha unajua kwenye maisha hakuna kitu kinadumu ee yote mapito tu take it easy najua ni ngumu lkn jua one day Yes
 
wape darasa!!! Hawajui kuzeveza vijana!!

Hahaha...wanaume wengi wanadhani kuzeveza ni kumsumbua sumbua mwanamke...hawajui kuwa if you can build a castle inside woman's heart, basi unakuwa umemaliza zaidi ya 80% ya tongozo lol
 
habarini wana mmu.

Katika kujitafiti nimegundua nina tatizo ambalo silielewi. Tatizo lenyewe ni hili:
Kila mwanamke ninayemtongoza simpati anaishia kunitolea nje. Na kama tulikua na urafiki wa kawaida na wenyewe unakufa. Hata hivyo mwisho wa siku bila kuelewa imekuaje kuaje najikuta nina mpenzi ambaye sijamtongoza.
Katika hao ambao nawapata bila kuwatongoza wengi wao ni marafiki wa wale watongozwa. Yaani shabaha inamkosa mhusika na asiyehusika najikuta tu nipo naye.
Wakati nafikiria labda ni hisia zangu tu kwamba ninayemtaka simpati, mwaka jana nilikutana na dada mmoja skype na sijui ilikuwaje kuwaje hadi akawepo kwenye list ya friends wangu. Tulikuwa tukichat sana hadi akiniaga nasikitika. Baadae tulikuja kukutana millenium tower. Tukaongea sana na kucheka cheka kama machizi. Mwisho wa siku nikaingizia mada ya uhusiano nayo ikaua urafiki hadi leo. Kwa kweli iliniuma sana maana sio siri nilimpenda hadi basi. Mpaka leo siamini kweli kama imetokea. Japo nina mpenzi mwingine ki ukweli haipiti siku bila kumuwaza. Naangalia picha zake alizowahi kunitumia whatsap na facebook..nabaki kuumia tu moyoni.
Huyu ni habari ya siku za usoni, lakini nyuma yake kwa vipindi tofauti imekuwa ikitokea hivi hivi..ninayempenda kweli kweli simpati. Na hao wengineo imekuwa ni migogoro tuu kwa kuwa upendo ule wa dhati nakuwa sina..ila huwa najipa moyo kwamba mbele ya safari nitafall deeply kitu ambacho hakitokei.
Jamani nifanyeje? Hii ni my real personal life.
mi naona kama utulie na uache zinaa kwa muda wkt unajitafakari labda ukirudi utakuwa mpya na utapendwa
 
Back
Top Bottom