Jamani, katika hili JK apongezwe!!

Jamani, katika hili JK apongezwe!!

Unajua kuna watu kazi yao kukosoa tu,rais ana majuku mazito ya kuliongoza taifa hili,ndio maana kuna amani,hivi mtanapotoa lawama rais kafanya hiki mara kile mnapata nini,unajua mtu yeyote asiye nashukrani ukifuatilia utaona ana matatizo lukuki,nakushukuru uliyeleta hii thread hapa javini,na kumpongeza raisi wetu.

Wewe unayeona rais hafai ondoka nenda kaishi nchi nyingine utakapo mpata rais anayefaa zaidi ya huyu tuliyenaye.

Watanzania lazima tubadilike tufanye kazi tuache kutoa lama kila kukicha,hii ni dalili ya uvivu wa kufikiri.

Kikwete ni rais bora,huo ndio ukweli wa mambo.
 
Ni Tanzania pekee ambapo mtu akitimiza wajibu wake anatakiwa KUPONGEZWA.
Alafu mtoa mada usikute ni KADA wa CCM anausake UDC AU URC maana JK ukimegea sifa hakutupi!
 
nadhani mganga njaa ni wewe unaepost humu ili kulipwa pale Lumumba
kama hujaelewa usikurupuke
tunachojadii hapa ni uhalali wa kukatishwa kwa safari ya JK siku ya pili na pongezi feki
safari hukatishwa kwa kuahirisha dinner au unaacha kufanya kilichokupeleka na kurudi unapotakiwa mapema? kama taarifa aliipata j2 angerudi siki hiyo hiyo ndio tungesema kakatiza safari
na sio kesho yake siku alitakiwa kumaliza ziara yake
tatizo la maCCM hayatumii ubongo kufikiri
hata yakiambiwa leo unguza nyumba yako yataunguza tu kwa vile washazoea kufanya jambo bila kufikiri

Nyie waganga njaa hamkosi cha kusema; kwani tatizo lilikuwa wapi? Serikali yote ilikuwepo Arusha na wote walitekeleza majukumu yao chini ya maelekezo ya Raisi mlitaka ajigeuze upepo?
Chama
Gongo la. Mboto DSM
 
Sina hakika kama unakijua unachokisema. Mgomo wa madaktari ulitokea katika kipindi cha awamu ya nne na Rais ni huyu huyu pia ndiye huyu huyu alikwenda ziara ya nje wakati watu wakiendelea kufa kutokana na mgomo huo. Watu waliopoteza maisha katika kipindi hicho ni wengi zaidi KULIKO WA WA TUKIO LA aRUSHA. Sijui unataka kutuambia kuwa sasa hivi Raisi amekuwa mzalendo baada kukosa uzalendo siku za nyuma au unataka kutuambia ana huruma zaidi na wakristo? Maana walioathirika na mgomo wa madaktari walikuwemo waislam, wakristo hata wapagani au ni kama kawaida yake kuzuga
Ndg wanajamvi,

Kama ulivyo usemi wa wahenga wetu kuwa "mnyonge mnyongeni lakini haki take mpeni" Nijuzi baada ya mlipuko wa bomu kanisani huko Arusha, Rais Kikwete alikuwa ziarani nje ya nchi kama kawaida yake ya kutotulia nchini kwake lakini baada ya kutaarifiwa janga hilo la bomu, aliamua kukatisha ziara yake na kuacha malengo yake yote ya ziara hiyo na kurudi nyumbani kushirikiana na wananchi wake katika mkasa huo.

Kweli huo ni uzalendo na ninashauri vyombo vya habari viliweke wazi jambo hilo kwa watanzania kama vilivyokuwa vinaweka wazi pale marais waliomtangulia JK walipokuwa wanaendelea na mambo yao nje ya nchi wakati watanzania wanumia bila msaada. Mfano wakati wa mgomo wa madaktari muhimbili na wakati huo Raisi yuko majuu miaka ileeeeee!!!!
 
Katika Tanzania hii kila mtu ana majukumu yake muhimu kwake na kwa Taifa lake. Kukaa na kuishi nchini Tanzania sio hisani ni haki ya kila raia awe na cheo au bila cheo. Mawazo ya kusema kama hutaki kumsifia Rais uhame nchini, ukatafute mahali pengine pa kuishi sijui unayapata wapi. Kinachomfanya mtu aishi nchini Tanzania sio kumsifia Rais ni uraia wa mtu. Watu wanaomkosoa Rais wanafanya kazi nzuri amabayo wewe huwezi kuifanya kwa hulka zako tu. Raisi akijirekebisha kama alivyofanya sasa kuahirisha ziara kwa sababu nchini kwake kuna tatizo ni matokeo ya wakosoaji wake. Walimkosoa alipoondoka kwenda Brazil wakati wa mgomo wa madaktari, wakosoaji walifanya kazi yao, leo amejirekebisha. Kumsifia mfalme kuwa amevaa vizuri wakati kiukweli yuko uchi ni kufedhehesha mfalme wako.
Unajua kuna watu kazi yao kukosoa tu,rais ana majuku mazito ya kuliongoza taifa hili,ndio maana kuna amani,hivi mtanapotoa lawama rais kafanya hiki mara kile mnapata nini,unajua mtu yeyote asiye nashukrani ukifuatilia utaona ana matatizo lukuki,nakushukuru uliyeleta hii thread hapa javini,na kumpongeza raisi wetu.

Wewe unayeona rais hafai ondoka nenda kaishi nchi nyingine utakapo mpata rais anayefaa zaidi ya huyu tuliyenaye.

Watanzania lazima tubadilike tufanye kazi tuache kutoa lama kila kukicha,hii ni dalili ya uvivu wa kufikiri.

Kikwete ni rais bora,huo ndio ukweli wa mambo.
 
Lokissa
Wewe ni veteran wa waganga njaaa humu JF unafahamika sana; huna jipya wala huninyimi usingizi; Kikwete mtamuota sana hamkosi la kusema hata sishangazwi sana na hilo hiyo ndiyo ajira yako; leo umevuta ngapi mpaka dk hii?
Chama
Gongo la mboto DSM
 
Last edited by a moderator:
Kwa hapo alijitahidi. Hivyo ndivyo kiongozi anavyo takiwa kuwa. Sio watu wako wanapata shida unaendelea kucheza disco.
 
Kilichomrudisha nyumbani siyo bomu kutupwa Kanisani na kusababisha vifo na kujeruhi watu kadhaa, kilichomrudisha ni alipoambiwa kuwa wahusika wakuu ni raia wa Saudia, ilimlazimu kurudi haraka kufunika mambo, ndiyo maana hadi sasa majina na picha za hao Wasaudia hazionyeshwi wala majina yao hayatajwi.
 
labda wewe ndio unanifahamu
sina chama cha siasa
na wala silipwi na mtu yoyote
huwa nakosoa au kupongeza panapofaa iwe ni CCM au Upinzani.
ni mtu mdanganyika atakaepongeza kitu bila kufikiri kama wewe.
lumumba team tunawajua
upeo wako unadhihirisha ukilaza wako.
Lokissa
Wewe ni veteran wa waganga njaaa humu JF unafahamika sana; huna jipya wala huninyimi usingizi; Kikwete mtamuota sana hamkosi la kusema hata sishangazwi sana na hilo hiyo ndiyo ajira yako; leo umevuta ngapi mpaka dk hii?
Chama
Gongo la mboto DSM
 
kurudi nchini kwa sababu ya janga ni jambo ambalo Maraisi wote wenye busara duniani hufanya wala siyo kitu special sana cha kutufanya tumsifie Kikwete.
Ishu ni kwamba haya matukio yamepaliliwa na sera za udini za chama tawala.
 
Lokissa
Unaikana chadema utakula wapi? Kila siku mkielezwa ukweli utetezi wenu mkubwa ni eti mimi sina chama; huo sio ungo dhahiri kama wewe huna chama unakesha kufanya nini JF? Hebu niwekee post moja uliyoisifia CCM au mh. Kikwete. Mkuu sema nayo njaa yako vinginevyo itakupeleka pabaya
Chama
Gongo la mboto DSM
 
Last edited by a moderator:
sina njaa ndugu wala sijawahi kuishi kwa mgongo wa mtu au chama
sina haja ya kukuwekea post nilizosifia serikali
we are not in court and Im not ablidged to so.
kazi yangu hainiruhusu kuwa mwanasiasa
lakini hainikatazi kukosoa maovu ya CCM au Chadema.
na hainizuii kutoa maoni.
kwa hili sitaweza kuwa mnafiki kumpngeza JK,ingekua ndivo kama angerudi j2 ile ile
karibu Ngaramtoni uone kilimo kwanza sio kupiga debe hapo dar ili uwahi Lumumba.
 
sina njaa ndugu wala sijawahi kuishi kwa mgongo wa mtu au chama
sina haja ya kukuwekea post nilizosifia serikali
we are not in court and Im not ablidged to so.
kazi yangu hainiruhusu kuwa mwanasiasa
lakini hainikatazi kukosoa maovu ya CCM au Chadema.
na hainizuii kutoa maoni.
kwa hili sitaweza kuwa mnafiki kumpngeza JK,ingekua ndivo kama angerudi j2 ile ile
karibu Ngaramtoni uone kilimo kwanza sio kupiga debe hapo dar ili uwahi Lumumba.
Mkuu unaendelea kujichanganya hapa tunajadili siasa; kazi unafanya mpaka ushindwe kujihusiha na siasa? Siku mapadri; mashekhe wote tunao kwenye siasa; mkuu njaa yako sema nayo
Chama
Gongo la mboto DSM
 
Nyie waganga njaa hamkosi cha kusema; kwani tatizo lilikuwa wapi? Serikali yote ilikuwepo Arusha na wote walitekeleza majukumu yao chini ya maelekezo ya Raisi mlitaka ajigeuze upepo?
Chama
Gongo la. Mboto DSM

Soma vizuri mawazo ya wachangiaji.kinachopingwa hapa siyo kutofika kwake haraka arusha,ila ni ile kutuhadaa eti alikatisha safari wakati siku 2 za ziara yake ziliku wa zimeisha hatudanganyiki!
 
Wana jamvi naomba tuwe watu wa kufikiri,
hivi ni nani kati yenu ambaye mtoto wake akiwa mla unga wa mda mrefu na baadae akaamua kucha asimpongeze?
Je mtoto akiwa mwizi na akaamua kuacha humpongezi?
Marais wa nchi hii hawakuwahi kufanya tendo alofanya JK la kurudi home kabla ya kukamilisha ratiba yake Kuwait, hata kama aliwahi lisaa limoja tu, bado ni element ya utafauti na watangulizi wake (isipokuwa Mwalimu) na kuonyesha mabadiriko kidogo.
Naomba nitambulike wazi kuwa mie sio muumini wa JK na wala hakuipata kura yangu na wala siutarajii u DC!!!

Kama ukijua mtoto wako ni mwizi inabidi umfikishe kwenye vyombo vya sheria siyo kusubiri aache eti umpongeze!!! No wonder ujangiri unaongezeka Bongo kwa vile tuna wazazi kama nyinyi mnaowaficha wahalifu mkisubiri waache wenyewe!!
 
Soma vizuri mawazo ya wachangiaji.kinachopingwa hapa siyo kutofika kwake haraka arusha,ila ni ile kutuhadaa eti alikatisha safari wakati siku 2 za ziara yake ziliku wa zimeisha hatudanganyiki!
Kama aliondoka saa 12 asubuhi badala ya saa 2 usiku atakuwa amekatisha ziara kuna hafla nyingi angezifanya
Chama
Gongo la mboto DSM
 
Hebu fikiria wewe ni Baba wa familia, ukawa uko safarini mkoa au nje ya nchi. Ukapata taarifa kuwa nyumba yako imeungua au bahati mbaya mwanao amefariki. Kama utaachana na safari yako na kurudi nyumbani, utapongezwa kwa kuijali familia yako au utakuwa unatekeleza wajibu wako ulioahidi siku unafunga ndoa ?
Hakika huu ni mfano mfu, yaani unadhani uchungu wa JK kwa wale waliokufa kwenye mlipuko wa bomu ni sawa na angefiwa na Riz1? Angekufa Riz1 hiyo ndege ingepiga riverse angani..! Utakuwa umesahau kuwa ''Damu ni nzito kuliko Maji''
 
Kama aliondoka saa 12 asubuhi badala ya saa 2 usiku atakuwa amekatisha ziara kuna hafla nyingi angezifanya
Chama
Gongo la mboto DSM

mkuu chama kama unaweza kupitia nusanusa ya lumumba ebu tupia program ya hiyo siku ya pili ili tuone hizo hafla kama zilikuwa na tija.tunaombea next trip to singapore isikatizwe
 
Kilichonifuraisha kwenye mada hii ni kuwa wachangiaji wanabishana kwa hoja si matusi. Tofauti na id moja tu ya Isalia, waliobaki hongereni kwa michango mizuri kuanzia mleta mada. Hata kama hoja haikupendezi,kutukana si njia sahihi. Hongereni.
 
Back
Top Bottom