Jamani, katika hili JK apongezwe!!

Jamani, katika hili JK apongezwe!!

Tiger One

JF-Expert Member
Joined
Apr 11, 2012
Posts
568
Reaction score
312
Ndg wanajamvi,

Kama ulivyo usemi wa wahenga wetu kuwa "mnyonge mnyongeni lakini haki take mpeni" Nijuzi baada ya mlipuko wa bomu kanisani huko Arusha, Rais Kikwete alikuwa ziarani nje ya nchi kama kawaida yake ya kutotulia nchini kwake lakini baada ya kutaarifiwa janga hilo la bomu, aliamua kukatisha ziara yake na kuacha malengo yake yote ya ziara hiyo na kurudi nyumbani kushirikiana na wananchi wake katika mkasa huo.

Kweli huo ni uzalendo na ninashauri vyombo vya habari viliweke wazi jambo hilo kwa watanzania kama vilivyokuwa vinaweka wazi pale marais waliomtangulia JK walipokuwa wanaendelea na mambo yao nje ya nchi wakati watanzania wanumia bila msaada. Mfano wakati wa mgomo wa madaktari muhimbili na wakati huo Raisi yuko majuu miaka ileeeeee!!!!
 
Ndg wanajamvi,
kama ulivyo usemi wa wahenga wetu kuwa "mnyonge mnyongeni lakini haki take mpeni"
Nijuzi baada ya mlipuko wa bomu kanisani huko Arusha, Rais Kikwete alikuwa ziarani nje ya nchi kama kawaida yake ya kutotulia nchini kwake lakini baada ya kutaarifiwa janga hilo la bomu, aliamua kukatisha ziara yake na kuacha malengo yake yote ya ziara hiyo na kurudi nyumbani kushirikiana na wananchi wake katika mkasa huo.
Kweli huo ni uzalendo na ninashauri vyombo vya habari viliweke wazi jambo hilo kwa watanzania kama vilivyokuwa vinaweka wazi pale marais waliomtangulia JK walipokuwa wanaendelea na mambo yao nje ya nchi wakati watanzania wanumia bila msaada. Mfano wakati wa mgomo wa madaktari muhimbili na wakati huo Raisi yuko majuu miaka ileeeeee!!!!

Wacha urongo,

JK alikuwa na ziara ya siku 2 kuanzia jumapili hadi jumatatu. JK aliondoka nchini jumapili asubuhi, na huku nyuma bomu likalipuka. Ina maana wakati JK anatua Kuwait, Jumapili mchana alikuwa na taarifa. JK aliendelea na ziara yake hadi Jumatatu mchana ndipo akarudi. Kumbuka masaa ya Kuwait yapo sambamba na ya bongo... angekuwa anajali saana angegeuza ile ile jumapili...
 
Ndg wanajamvi,
kama ulivyo usemi wa wahenga wetu kuwa "mnyonge mnyongeni lakini haki take mpeni"
Nijuzi baada ya mlipuko wa bomu kanisani huko Arusha, Rais Kikwete alikuwa ziarani nje ya nchi kama kawaida yake ya kutotulia nchini kwake lakini baada ya kutaarifiwa janga hilo la bomu, aliamua kukatisha ziara yake na kuacha malengo yake yote ya ziara hiyo na kurudi nyumbani kushirikiana na wananchi wake katika mkasa huo.
Kweli huo ni uzalendo na ninashauri vyombo vya habari viliweke wazi jambo hilo kwa watanzania kama vilivyokuwa vinaweka wazi pale marais waliomtangulia JK walipokuwa wanaendelea na mambo yao nje ya nchi wakati watanzania wanumia bila msaada. Mfano wakati wa mgomo wa madaktari muhimbili na wakati huo Raisi yuko majuu miaka ileeeeee!!!!

Mkuu!

Sema unatafuta kujua hisia za waTanzania katika hili. Hivi unakubaliana na wanao sema aliahirisha ziara yake? Ki diplomasia/ protokali nini maana ya ziara ya siku mbili nje ya nchi? Hata kama ulifika nchi ile saa moja jioni, ile ni siku ya kwanza.

Na unaye mpongeza alitumia MA-USIKU MAWILI (2 NIGHTS) ambazo tayari ni siku mbili hata angeondoka asubuhi ya saa kumi na mbili. Ili mradi alihitaji kupewa huduma zote za kiitifaki na kidiplomasia.

Na kwa taarifa ya ofisi yake, tuali tangaziwa kwamba ni ziara ya siku mbili. Hivyo huko mnaoita kuahirisha kunatoka wapi? Au ndio ule muendelezo kwamba "NYUMBA YA MUONGO HAIISHI VITUKO?"
 
Mmmmmh!
Apongezwe?
Mie ninavyojua ni wajibu wake!!
Kwa hiyo kila anayetekeleza wajibu wake apongezwe?
 
Huwa nawashangaa sana wanaume wengine na huwa najiuliza hivi wakifunga zipu wanafungia nini humo ndani
Si kila anayevaa suruwali ni Mwanaume, na kuna tofauti kubwa kati ya Mwanamume na mtoto wa Kiume.
 
ndg wanajamvi,

kama ulivyo usemi wa wahenga wetu kuwa "mnyonge mnyongeni lakini haki take mpeni" nijuzi baada ya mlipuko wa bomu kanisani huko arusha, rais kikwete alikuwa ziarani nje ya nchi kama kawaida yake ya kutotulia nchini kwake lakini baada ya kutaarifiwa janga hilo la bomu, aliamua kukatisha ziara yake na kuacha malengo yake yote ya ziara hiyo na kurudi nyumbani kushirikiana na wananchi wake katika mkasa huo.

Kweli huo ni uzalendo na ninashauri vyombo vya habari viliweke wazi jambo hilo kwa watanzania kama vilivyokuwa vinaweka wazi pale marais waliomtangulia jk walipokuwa wanaendelea na mambo yao nje ya nchi wakati watanzania wanumia bila msaada. Mfano wakati wa mgomo wa madaktari muhimbili na wakati huo raisi yuko majuu miaka ileeeeee!!!!


huko majuu huwa nakwenda kufanya nini wajameni ? Mbona haji kwetu kasulu ? Kwani tulimchaguza kutembea majuu
 
Last edited by a moderator:
Ndg wanajamvi,

Kama ulivyo usemi wa wahenga wetu kuwa "mnyonge mnyongeni lakini haki take mpeni" Nijuzi baada ya mlipuko wa bomu kanisani huko Arusha, Rais Kikwete alikuwa ziarani nje ya nchi kama kawaida yake ya kutotulia nchini kwake lakini baada ya kutaarifiwa janga hilo la bomu, aliamua kukatisha ziara yake na kuacha malengo yake yote ya ziara hiyo na kurudi nyumbani kushirikiana na wananchi wake katika mkasa huo.

Kweli huo ni uzalendo na ninashauri vyombo vya habari viliweke wazi jambo hilo kwa watanzania kama vilivyokuwa vinaweka wazi pale marais waliomtangulia JK walipokuwa wanaendelea na mambo yao nje ya nchi wakati watanzania wanumia bila msaada. Mfano wakati wa mgomo wa madaktari muhimbili na wakati huo Raisi yuko majuu miaka ileeeeee!!!!

Hebu fikiria wewe ni Baba wa familia, ukawa uko safarini mkoa au nje ya nchi. Ukapata taarifa kuwa nyumba yako imeungua au bahati mbaya mwanao amefariki. Kama utaachana na safari yako na kurudi nyumbani, utapongezwa kwa kuijali familia yako au utakuwa unatekeleza wajibu wako ulioahidi siku unafunga ndoa ?
 
Ndg wanajamvi,

Kama ulivyo usemi wa wahenga wetu kuwa "mnyonge mnyongeni lakini haki take mpeni" Nijuzi baada ya mlipuko wa bomu kanisani huko Arusha, Rais Kikwete alikuwa ziarani nje ya nchi kama kawaida yake ya kutotulia nchini kwake lakini baada ya kutaarifiwa janga hilo la bomu, aliamua kukatisha ziara yake na kuacha malengo yake yote ya ziara hiyo na kurudi nyumbani kushirikiana na wananchi wake katika mkasa huo.

Kweli huo ni uzalendo na ninashauri vyombo vya habari viliweke wazi jambo hilo kwa watanzania kama vilivyokuwa vinaweka wazi pale marais waliomtangulia JK walipokuwa wanaendelea na mambo yao nje ya nchi wakati watanzania wanumia bila msaada. Mfano wakati wa mgomo wa madaktari muhimbili na wakati huo Raisi yuko majuu miaka ileeeeee!!!!

Unampongeza kwa kukatisha ziara yake au ni wajibu wake? Unajua hiyo ni safari ya mia ngapi?? Nafikiri ungempongeza kwa kuzuia uharifu sasa juzi amempa Saidi mwema na Kova nishanio ya utumishi wa jeshi lapolisi iliyotukuka,leo muulize hizo nishani zilikuwa za nini???:help:
 
Teundelee kupongezana jamani ila nchi inaangamia naona tunaelekea kuwa kuwa kama nchi zilizoshindwa kama vile Nigeria, Pakistani na Somalia ila tunaendelea kupongezana tu.Ninachokiona itafika mahali tutaona aibu kujitambulisha kama sisi ni Watanzania huko nje ya nchi.Waambie waliokutuma nchi inaangamia tuko nyuma ya Rwanda pamoja na rasilimali zote tulizonazo.Waambie pia kimataifa hatuna tena cha kujivunia.
 
alikatisha dinner, huo ndio uzalendo unaotaka tumpongeze nao?
bado una akili za panzi.
ziara ya JK ilikuwa ya siku 2 kuanzia tarehe 5 hadi 6, alirudi tarehe 6, sasa alikatiza wapi zaidi ya dinner?
 
Siyo mbaya kutoa mtazamo wako
kwa hiyo wewe umeona anastahili pongezi?
Ndg wanajamvi,

Kama ulivyo usemi wa wahenga wetu kuwa "mnyonge mnyongeni lakini haki take mpeni" Nijuzi baada ya mlipuko wa bomu kanisani huko Arusha, Rais Kikwete alikuwa ziarani nje ya nchi kama kawaida yake ya kutotulia nchini kwake lakini baada ya kutaarifiwa janga hilo la bomu, aliamua kukatisha ziara yake na kuacha malengo yake yote ya ziara hiyo na kurudi nyumbani kushirikiana na wananchi wake katika mkasa huo.

Kweli huo ni uzalendo na ninashauri vyombo vya habari viliweke wazi jambo hilo kwa watanzania kama vilivyokuwa vinaweka wazi pale marais waliomtangulia JK walipokuwa wanaendelea na mambo yao nje ya nchi wakati watanzania wanumia bila msaada. Mfano wakati wa mgomo wa madaktari muhimbili na wakati huo Raisi yuko majuu miaka ileeeeee!!!!
 
Jamii forum is in TRANSITION PERIOD. THERE IS A CONTRARY BETWEEN RESPONSIBILITY AND VOLUNTEERING THIS IS HIS RESPONSIBILITY AND HE CANT DESERVED THAT CONGRATS.



"WHEN I DO GOOD I FEEL GOOD AND WHEN I DO BAD IFEEL BAD AND THAT IS MY RELIGION" ABRAHAM LINCOLN.
 
Kwa sasa hivi, binafsi focus yangu iko kwa akina nani mahakama itawakuta na hatia na hukumu itakayotolewa baada ya hapo! Kuna kesi nyingi sana za aina hii ziko mahakamani na hakuna mtu aliyewahi kukutwa na hatia. Niwaulize swali, tangu vurugu za kidini zianze na majengo ya ibada kuchomwa na baadhi ya viongozi wa dini kuuwawa, ni nani aliyewahi kukutwa na hatia na akahukumiwa? Wizi mtupu!!!

Kwa sasa hizi porojo za nilikuwa safarini nikaahirisha safari, sijui tumekamata victor wakati majina mengine yamefichwa hizo ni siasa tu ambazo mimi kama mtanzania hazinisaidii lolote.

Tunataka kuona serikali ikikamata wahusika na kuwaadhibu ili iwe fundisho kwao na kwa wengine ambao wamepanga kufanya mambo mabaya na maovu ya namna hii. Vingenevyo, nitaendelea kutokuwaamini viongozi na uongozi ulioko madarakani.
 
Wana jamvi naomba tuwe watu wa kufikiri,
hivi ni nani kati yenu ambaye mtoto wake akiwa mla unga wa mda mrefu na baadae akaamua kucha asimpongeze?
Je mtoto akiwa mwizi na akaamua kuacha humpongezi?
Marais wa nchi hii hawakuwahi kufanya tendo alofanya JK la kurudi home kabla ya kukamilisha ratiba yake Kuwait, hata kama aliwahi lisaa limoja tu, bado ni element ya utafauti na watangulizi wake (isipokuwa Mwalimu) na kuonyesha mabadiriko kidogo.
Naomba nitambulike wazi kuwa mie sio muumini wa JK na wala hakuipata kura yangu na wala siutarajii u DC!!!
 
Wacha urongo,

JK alikuwa na ziara ya siku 2 kuanzia jumapili hadi jumatatu. JK aliondoka nchini jumapili asubuhi, na huku nyuma bomu likalipuka. Ina maana wakati JK anatua Kuwait, Jumapili mchana alikuwa na taarifa. JK aliendelea na ziara yake hadi Jumatatu mchana ndipo akarudi. Kumbuka masaa ya Kuwait yapo sambamba na ya bongo... angekuwa anajali saana angegeuza ile ile jumapili...

Tatizo lako chuki zinakusumbuwa inawezekana juu ya chama chake au dini yake au vyote viwili ila tumia akili sio kila kitu kupinga tu kama viongozi wako wa chama chako
 
Back
Top Bottom