IROKOS
JF-Expert Member
- Aug 13, 2011
- 10,184
- 7,819
Wana JF muda mfupi uliopita nilikuwa naangalia EATV kuna kipindi kipya kaanzisha Salama Jabir (yule jaji wa bongo star reasch), nikaona anamuhoji dada mmoja mrembo na star wa bongo movie kama sikosei, anayeitwa Irene Uwoya. Wako saloon na wanahojiana mambo mbalimbali but kitu kimoja ndiyo kimenifanya niilete hii hoja hapa kwenye jamvi: Salama kamuuliza huyu star umeshawahi kulewa talalila?? naye akajibu hapana na akaendelea kwamba yeye anakunywa sana lakini cha ajabu huwa halewi, anaendelea kwamba yeye akiamka tu asubuhi cha kwanza pombe! maisha yake yote. Sasa naomba kujuzwa hivi huu ndiyo mvumo wa maisha wa hawa mastaa/wasanii wetu? Hivi ukiwa msanii (ambapo wenyewe wanapenda kusema ni kioo cha jamii) ni lazima pombe ukitawale kiasi kwamba unaigeuza kuwa chai au supu?? Mimi nimeshindwa kuamini nilichokuwa nakiona kwani mdada mwenyewe mrembo wa ukweli halafu cha pombe!!!!