Jamani CCM waongo....nyinyi sikieni tu

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Nov 25, 2010
6,135
17,802
Leo kulikuwa na Kongamano la kusindikiza Maadhimisho ya Miaka 51 ya Uhuru wa Tanganyika.Maadhimisho hayo yaliyoratibiwa na Jumuiya ya Wanazuoni wa UDSM-UDASA,yalifanyika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika Ukumbi wa Nkrumah. Wachokoza hoja na Wachangiaji walikuwa wengi.Lakini nilikuwa 'bias'.Niliwafuatilia kwa ukaribu wa kutoka chama tawala-CCM hasa Deo Filikunjombe na January Makamba.

Makamba alijinadi kwa hoja mbili: kwanza, urais wa 2015 uende kwa aliyezaliwa baada ya 1961.Na pili, elimu bure inawezekana. January,kabla ya kuwa Mbunge wa Bumbuli, alikuwa Mwandishi wa Hotuba wa Rais Kikwete kwa muhula wote wa 2005-2010 akisaidiana na Prof. Mukandala wa UDSM. Ni yeye aliyekuwa akipamba hotuba za Kikwete wakati wa kampeni za 2010 kukejeli hoja za CHADEMA kuwa elimu bure inawezekana na Kikwete,aliyezaliwa miaka 11 kabla ya uhuru,ni chaguo sahihi kwa watanzania. Leo akisema hivi,tumueleweje? Si muongo,mzandiki na mnafiki huyu?

Deo naye kasema Tanzania si mali ya CCM....ni mali ya watanzania wote. Mbona yeye ni mwimbaji mzuri wa kidumu chama cha mapinduzi na wa kuwaaminisha watanzania kuwa bila CCM hakuna Tanzania na 'vice versa is true'? Alitaka aeleweke vipi Deo? Si muongo huyu kwakuwa bado yupo ndani ya CCM na mtawanyaji mzuri wa ujumbe wa kifisadi kuwa Tanzania ni mali ya CCM?

Niliondoka mapema kwakuwa waliniudhi sana.Wana bahati kulikuwa na ulinzi.Pia,nililinda heshima yangu.Humchukia sana mtu mnafiki hasa anapokuwa karibu yangu!
 
Ulikuwa umevaa miwani ya chama gani wakati ukiwatazama hawa vijana wawili? Halafu naona kama umewashambulia watu na si hoja zao. Mwenye dhambi akitubu na kusamehewa Mungu hazikumbuki dhambi zake. Labda wazungumzaji hawa wawili wametubu dhambi zao na wapo katika mchakato wa kuziacha kwa kuhakikisha wanavua gamba. Hivyo naomba tuwape mda kama watazuacha dhambi zao. Kama watatubu na kushidwa kuziacha amin amin nakwambia damu yao na iwe juu ya vichwa vyao.
Leo kulikuwa na Kongamano la kusindikiza Maadhimisho ya Miaka 51 ya Uhuru wa Tanganyika.Maadhimisho hayo yaliyoratibiwa na Jumuiya ya Wanazuono wa UDSM-UDASA,yalifanyika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika Ukumbi wa Nkrumah. Wachokoza hoja na Wachangiaji walikuwa wengi.Lakini nilikuwa 'bias'.Niliwafuatilia kwa ukaribu wa kutoka chama tawala-CCM hasa Deo Filikunjombe na January Makamba.

Makamba alijinadi kwa hoja mbili: kwanza, urais wa 2015 uende kwa aliyezaliwa baada ya 1961.Na pili, elimu bure inawezekana. January,kabla ya kuwa Mbunge wa Bumbuli, alikuwa Mwandishi wa Hotuba wa Rais Kikwete kwa muhula wote wa 2005-2010 akisaidiana na Prof. Mukandala wa UDSM. Ni yeye aliyekuwa akipamba hotuba za Kikwete wakati wa kampeni za 2010 kukejeli hoja za CHADEMA kuwa elimu bure inawezekana na Kikwete,aliyezaliwa miaka 11 kabla ya uhuru,ni chaguo sahihi kwa watanzania. Leo akisema hivi,tumueleweje? Si muongo,mzandiki na mnafiki huyu?

Deo naye kasema Tanzania si mali ya CCM....ni mali ya watanzania wote. Mbona yeye ni mwimbwji mzuri wa kidumu chama cha mapinduzi na wa kuwaaminisha watanzania kuwa bila CCM hakuna Tanzania na 'vice versa is true'? Alitaka aeleweke vipi Deo? Si muongo huyu kwakuwa bado yupo ndani ya CCM na mtawanyaji mzuri wa ujumbe wa kifisadi kuwa Tanzania ni mali ya CCM?

Niliondoka mapema kwakuwa waliniudhi sana.Wana bahati kulikuwa na ulinzi.Pia,nililinda heshima yangu.Humchukia sana mtu mnafiki hasa anapokuwa karibu yangu!
 
Leo kulikuwa na Kongamano la kusindikiza Maadhimisho ya Miaka 51 ya Uhuru wa Tanganyika.Maadhimisho hayo yaliyoratibiwa na Jumuiya ya Wanazuono wa UDSM-UDASA,yalifanyika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika Ukumbi wa Nkrumah. Wachokoza hoja na Wachangiaji walikuwa wengi.Lakini nilikuwa 'bias'.Niliwafuatilia kwa ukaribu wa kutoka chama tawala-CCM hasa Deo Filikunjombe na January Makamba.

Makamba alijinadi kwa hoja mbili: kwanza, urais wa 2015 uende kwa aliyezaliwa baada ya 1961.Na pili, elimu bure inawezekana. January,kabla ya kuwa Mbunge wa Bumbuli, alikuwa Mwandishi wa Hotuba wa Rais Kikwete kwa muhula wote wa 2005-2010 akisaidiana na Prof. Mukandala wa UDSM. Ni yeye aliyekuwa akipamba hotuba za Kikwete wakati wa kampeni za 2010 kukejeli hoja za CHADEMA kuwa elimu bure inawezekana na Kikwete,aliyezaliwa miaka 11 kabla ya uhuru,ni chaguo sahihi kwa watanzania. Leo akisema hivi,tumueleweje? Si muongo,mzandiki na mnafiki huyu?

Deo naye kasema Tanzania si mali ya CCM....ni mali ya watanzania wote. Mbona yeye ni mwimbwji mzuri wa kidumu chama cha mapinduzi na wa kuwaaminisha watanzania kuwa bila CCM hakuna Tanzania na 'vice versa is true'? Alitaka aeleweke vipi Deo? Si muongo huyu kwakuwa bado yupo ndani ya CCM na mtawanyaji mzuri wa ujumbe wa kifisadi kuwa Tanzania ni mali ya CCM?

Niliondoka mapema kwakuwa waliniudhi sana.Wana bahati kulikuwa na ulinzi.Pia,nililinda heshima yangu.Humchukia sana mtu mnafiki hasa anapokuwa karibu yangu!

kweli Mkuu Hawa jamaa ni waongo sana. Wanachoongea siku zote hakiendani na matendo yao.

Hawa jamaa ni viwanda vya kuzalisha uongo. Kwao kusema uongo ni moja ya sera zao.

Hata humu jf ukisoma tu thread unajua imeletwa na nani. Thread za magamba ni za uzushi, uongo na mipasho. Lumumba wameajiri watu kwa ajili ya kutunga Na kusema uongo. Wanaitwa kitengo Cha propaganda.
 
kauli ya Deo si mbaya , tanzania si mali ya ccm lakini huyu mwingine ni kuvaa mlegezo tu hana uwezo wowote maana alikula hela ya wahisani pale ikulu na kujifanya yeye ndiyo kila kitu
 
ccm bila uongo inakufa kwani imewageuza watz wote kama mademu zao,
ukimtongoza demu ukamwambia ukweli halisi jinsi ulivyo, ANAKUKATAA. ila ukimdanganya ANAKUKUBALI.
 
Hongereni UDSM kwa kuwa mna muda wa kuongea na kina Filikunjombe na Makamba wakilazimisha kuwahukumu watu wakose civil and political right just because of age...why? Napata shida kujua aina ya viongozi wanaotoka UDSM kwa miaka ya karibuni. Wakati UDSM wakipiga soga za urais,Mwenyekiti wa jukwaa la katiba,Deus Kibamba alikuwa SAUT-Mwanza kuongea na vijana kuhusu mchakato wa kupata katiba mpya ulipofikia na haja ya vijana kufuatilia,kuelewa,kutathmini na kupima mazingira ya kuunda katiba itakayowaongoza miaka mingi ijayo.Sitashangaa kusikia wamepigiwa makofi na kushangiliwa hao kina Fillikunjombe na January kwa sababu wasomi wa siku hizi siyo wale aliowatarajia Mwl.Nyerere na Karume. Changamoto inayolikumba taifa ni ajira,nishati,usalama,ufisadi,miundombinu ya usafiri wa anga na majini n.k Ninaposikia watu wanaojiita viongozi wakiwa wanaongea na wana-UDSM eti wanajadili kuzaliwa kabla au baada ya 1961 kama kigezo cha urais,vinahusiana vipi na changamoto?
 
Hongereni UDSM kwa kuwa mna muda wa kuongea na kina Filikunjombe na Makamba wakilazimisha kuwahukumu watu wakose civil and political right just because of age...why? Napata shida kujua aina ya viongozi wanaotoka UDSM kwa miaka ya karibuni. Wakati UDSM wakipiga soga za urais,Mwenyekiti wa jukwaa la katiba,Deus Kibamba alikuwa SAUT-Mwanza kuongea na vijana kuhusu mchakato wa kupata katiba mpya ulipofikia na haja ya vijana kufuatilia,kuelewa,kutathmini na kupima mazingira ya kuunda katiba itakayowaongoza miaka mingi ijayo.Sitashangaa kusikia wamepigiwa makofi na kushangiliwa hao kina Fillikunjombe na January kwa sababu wasomi wa siku hizi siyo wale aliowatarajia Mwl.Nyerere na Karume. Changamoto inayolikumba taifa ni ajira,nishati,usalama,ufisadi,miundombinu ya usafiri wa anga na majini n.k Ninaposikia watu wanaojiita viongozi wakiwa wanaongea na wana-UDSM eti wanajadili kuzaliwa kabla au baada ya 1961 kama kigezo cha urais,vinahusiana vipi na changamoto?

Wehuu!
 
Hongereni UDSM kwa kuwa mna muda wa kuongea na kina Filikunjombe na Makamba wakilazimisha kuwahukumu watu wakose civil and political right just because of age...why? Napata shida kujua aina ya viongozi wanaotoka UDSM kwa miaka ya karibuni. Wakati UDSM wakipiga soga za urais,Mwenyekiti wa jukwaa la katiba,Deus Kibamba alikuwa SAUT-Mwanza kuongea na vijana kuhusu mchakato wa kupata katiba mpya ulipofikia na haja ya vijana kufuatilia,kuelewa,kutathmini na kupima mazingira ya kuunda katiba itakayowaongoza miaka mingi ijayo.Sitashangaa kusikia wamepigiwa makofi na kushangiliwa hao kina Fillikunjombe na January kwa sababu wasomi wa siku hizi siyo wale aliowatarajia Mwl.Nyerere na Karume. Changamoto inayolikumba taifa ni ajira,nishati,usalama,ufisadi,miundombinu ya usafiri wa anga na majini n.k Ninaposikia watu wanaojiita viongozi wakiwa wanaongea na wana-UDSM eti wanajadili kuzaliwa kabla au baada ya 1961 kama kigezo cha urais,vinahusiana vipi na changamoto?


mdau nakupongeza kwa hoja za kisiasa imara na zenye muono wa haki ya kizalendo.haiji kichwani kuzungumzia uraisi na miaka ya baada ya siti au kabla kama kigezo cha urais, ni upotofu mkubwa, na hili ndo ombwe la kupata wazalendo halisia wanaoipenda nchi yao na kutoa kipaumbele cha matazamio ya kweli ya watanzania walio wengi wanyonge.Tanzania ya leo tukianza kujadili matabaka ya ya namna hii kama kigezo , nataraji tutakuja kupata raisi mwendawazimu, sababu kipaumbele cha majukumu na vipaumbele vya watanzania kwa dhati havitazingatiwa.Ni upotofu wa wazi unajitokeza sasa hasa kwa vijana kutamani madaraka , kwa nia ya kujitajirisha kupitia siasa ,na si kuwatumikia wananchi wanyonge
 
Ni kweli hawa watu si wasafi wala wakweli, Mtu mkweli hutembelea maneno yake. Kama walipiga vita Sera za CHADEMA kwamba elimu bure haiwezekani, kwamba hiyo sera haitekelezeki na wakashika bango kwa watu kwamba wasiwasikilize CHADEMA, leo inakuwaje wameanza kutekeleza hizo sera kimya kimya na kuzifanya za ccm?

Ni kwlei katika maisha watu hufanya makosa na kurekebisha hapa na pale. Lakini tunachohitaji sasa ni wao kuwa wakweli na wawazi kwamba walikosea kuponda Sera za CHADEMA. Na kwamba baada ya kufunguka macho wamegundua kwamba CHADEMA walikuwa sahihi na sera zake ni sahihi kabisa kwa maendeleo ya nchi na ndiyo maana sasa wameanza kuzitekeleza. Kuzitekeleza kinyemela na kutaka zionekane ni zao ni wizi na ulaghai. Wakionnyesha kua acknowledge, hakuna mtu atawalaumu na tutawaponngeza kwa uungwana ingawa watabaki na changamoto kwamba ni "Slow learners, myopic & not proactive.

Vinginevyo, their malicious approaches can not flatter Tanzanians who are tired with endless lies and ever increasing life difficulties.
 
Hongereni UDSM kwa kuwa mna muda wa kuongea na kina Filikunjombe na Makamba wakilazimisha kuwahukumu watu wakose civil and political right just because of age...why? Napata shida kujua aina ya viongozi wanaotoka UDSM kwa miaka ya karibuni. Wakati UDSM wakipiga soga za urais,Mwenyekiti wa jukwaa la katiba,Deus Kibamba alikuwa SAUT-Mwanza kuongea na vijana kuhusu mchakato wa kupata katiba mpya ulipofikia na haja ya vijana kufuatilia,kuelewa,kutathmini na kupima mazingira ya kuunda katiba itakayowaongoza miaka mingi ijayo.Sitashangaa kusikia wamepigiwa makofi na kushangiliwa hao kina Fillikunjombe na January kwa sababu wasomi wa siku hizi siyo wale aliowatarajia Mwl.Nyerere na Karume. Changamoto inayolikumba taifa ni ajira,nishati,usalama,ufisadi,miundombinu ya usafiri wa anga na majini n.k Ninaposikia watu wanaojiita viongozi wakiwa wanaongea na wana-UDSM eti wanajadili kuzaliwa kabla au baada ya 1961 kama kigezo cha urais,vinahusiana vipi na changamoto?

Zimbabwe wanaongozwa na Kibabu Mugabe lakini hawamo katika nchi 48 masikini sana Duniani, uongozi sio Umri ni Hekima na Kujali wananchi wako.
 
Jamani, waacheni hawa watu wajikaange kwa mafuta yao wenyewe. Huyo mwezi wa kwanza hana la kutudanganya. Kama kweli yeye ni mzalendo wa kweli amwambie kwanza baba yake maka-amba arudishe fedha zetu alizoiba na amwambie atuombe radhi wa-Tanzania kwa kuwa mstari wa mbele kutupa serikali lege lege na iliyojaa wezi na majambazi wa rasilimali za nchi. Vinginevyo akae tu kimya maana yeye mwenyewe ni mwizi tu kama baba yake na rais wake aliyemtumikia kabla ya kuzawadiwa ubunge.
 
Leo kulikuwa na Kongamano la kusindikiza Maadhimisho ya Miaka 51 ya Uhuru wa Tanganyika.Maadhimisho hayo yaliyoratibiwa na Jumuiya ya Wanazuoni wa UDSM-UDASA,yalifanyika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika Ukumbi wa Nkrumah. Wachokoza hoja na Wachangiaji walikuwa wengi.Lakini nilikuwa 'bias'.Niliwafuatilia kwa ukaribu wa kutoka chama tawala-CCM hasa Deo Filikunjombe na January Makamba.

Makamba alijinadi kwa hoja mbili: kwanza, urais wa 2015 uende kwa aliyezaliwa baada ya 1961.Na pili, elimu bure inawezekana. January,kabla ya kuwa Mbunge wa Bumbuli, alikuwa Mwandishi wa Hotuba wa Rais Kikwete kwa muhula wote wa 2005-2010 akisaidiana na Prof. Mukandala wa UDSM. Ni yeye aliyekuwa akipamba hotuba za Kikwete wakati wa kampeni za 2010 kukejeli hoja za CHADEMA kuwa elimu bure inawezekana na Kikwete,aliyezaliwa miaka 11 kabla ya uhuru,ni chaguo sahihi kwa watanzania. Leo akisema hivi,tumueleweje? Si muongo,mzandiki na mnafiki huyu?

Deo naye kasema Tanzania si mali ya CCM....ni mali ya watanzania wote. Mbona yeye ni mwimbaji mzuri wa kidumu chama cha mapinduzi na wa kuwaaminisha watanzania kuwa bila CCM hakuna Tanzania na 'vice versa is true'? Alitaka aeleweke vipi Deo? Si muongo huyu kwakuwa bado yupo ndani ya CCM na mtawanyaji mzuri wa ujumbe wa kifisadi kuwa Tanzania ni mali ya CCM?

Niliondoka mapema kwakuwa waliniudhi sana.Wana bahati kulikuwa na ulinzi.Pia,nililinda heshima yangu.Humchukia sana mtu mnafiki hasa anapokuwa karibu yangu!

- Sasa Bro hawa ni waongo na wanafiki kuliko huko Chadema? Are you serious au unafurahisha genge tu, sasa untaka tuanze kuweka uongo na unafiki wa huko Chadema hapa? Please!!

Es!
 
Ulikuwa umevaa miwani ya chama gani wakati ukiwatazama hawa vijana wawili? Halafu naona kama umewashambulia watu na si hoja zao. Mwenye dhambi akitubu na kusamehewa Mungu hazikumbuki dhambi zake. Labda wazungumzaji hawa wawili wametubu dhambi zao na wapo katika mchakato wa kuziacha kwa kuhakikisha wanavua gamba. Hivyo naomba tuwape mda kama watazuacha dhambi zao. Kama watatubu na kushidwa kuziacha amin amin nakwambia damu yao na iwe juu ya vichwa vyao.
Ukishakula nyama ya mtu ni vigumu kuacha - JKN
 
Wametoa mawazo yao na msingi Deo ndo aliyetoa nn watanzania wengi wanakosea Kuhusu CCM, na Tanzania CCM ni Chama kinachopata ridhaa ipo siku inaweza kukosa ridhaaa hiyo na bado Taifa likaendelea miaka 30 iliyopita Kenya walidhani Kanu ndo Kenya na Unip ndo Zambia but Vipi leo? Au Kamuzu Banda Rais wa maisha but leo Malawi inaendelea bila yeye na chama chake so Ilikuiondoa CCM madarakni tunahitaji watu Honestly kama Deo wanaoweza Kuitenganisha nchi na CCM, akiwa ndani ya CCM Kumbuka taifa letu ni wagumu wakuelewa ktk Muktadha wa CCM na TAnzania
 
- sasa bro hawa ni waongo na wanafiki kuliko huko chadema? Are you serious au unafurahisha genge tu, sasa untaka tuanze kuweka uongo na unafiki wa huko chadema hapa? Please!!

Es!
mara nyingi huwa najiuliza kama una ubongo kichwani au vapour!!!si uweke huo uongo wa chadema!walisema elimi bure inawezekana mkatoa mapovu leo mnakubali
 
- Sasa Bro hawa ni waongo na wanafiki kuliko huko Chadema? Are you serious au unafurahisha genge tu, sasa untaka tuanze kuweka uongo na unafiki wa huko Chadema hapa? Please!!

Es!

Kajibu tuhuma zako za utapeli wa kuuzia watu ajira feki kwanza kabla hujajichafua zaidi kufagilia ufisadi.
 
Tukiacha suala la uongo, ngoja tujikite kwenye hoja. CCM hawana hati miliki ya nchi hii ni kweli hata wale wanaodai watatawala milele ni walevi ambao Machiavelli alisema wanakuwa - corrupted with power absolutely. Historia inatoa ushahidi huu kwa kuangalia Mobutu Kuku Wazabanga, Sadam Husen, Ghadafi, Mbaraka, nk.

Hivyo CCM inattoka tu madaRAKANI TENE KWA AIBU AMBAYO HAKUNA ANAYETEGEMEA. kWA NINI CCM INAELEKEA MWISHO? CCM ilikuwa chama cha wakulima na wafanyakazi hadi mwishoni mwa 1980. Baada ya hapo kakawa na ndoa ya mkeka kati ya mafisadi na viongozi wa CCM kule Zbar. (Zbar ni maarufu kwa ndoa hizo Rej mwafaka CUF-CCM). Kuanzia hapo CCM ikafa kilichobaki nikundi la mafisadi nawanasiasa wanaoganga nja kwa jina la CCM chama ambacho hakipo.

Kwa nini hakipo? Hakina wanachama mashinani na matawini kule kuna kundi la walalahoi wanaosubiri ubwabwa, kapelo, kanga, fulana, bukubuku wakati wa uchaguzi. Hakuna wanachama wala viongozi, hakuna vikao wala mikutano, hakuna itikadi wala falsafa, hakuna sera wala agenda. Siku watakapogundua wamedanganywa vya kutosha ndo mwisho wa genge linalojiita CCM.

Suala la urais haliwezi kuzungumzwa kwa mkabala wa umri tena na mtu anayejiita msomi. Hizo ni fikra uchwara tena mufilisi na zinahitaji kupata makazi kwenye pipa la taka. Urais sio mtu bali ni taasisi. Taasisi si mtu binafsi, taasisi haina umri ila waliomo ndani ya taasisi hiyo wana umri.

Ukiona mtu anazungumzia umri wa rais ujue ana mtizamo wa kiimla kwamba yeye akiwa rais basi ni kila kitu. Hata dhana ya mihimili ya dola haijui, huyo kalewa ukiritimba unaoendeshwa pale magogoni na ansahau tunafanya mabadiliko ya katiba kupunguza madaraka ya taasisi ya urais ili kuweka checks and balances. Hayo maoni apeleke kwenye tume ya Warioba. Baaahati mbaya sikumsikia alikuwa anatumia hoja gani kutetea hoja hiyo nyepesi ambayo hata mwanafunzi wa kidato cha kwanza hawezi kukubali.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom