Jakaya Kikwete: Mjanja, nguli na gwiji wa diplomasia za kimataifa

comrade igwe

JF-Expert Member
Jan 12, 2015
7,295
3,939
jakaya-kikwete-1.jpg


Jina lake ni Jakaya Mrisho Kikwete,ni Mh Rais mstaafu wa awamu ya nne katika serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, mwanajeshi mstaafu kwa cheo cha Luteni kanali, mwanadiplomasia mahiri mno mwenye macho ya kung'amua yatayotokea katika diplomasia mbalimbali kidunia.

Miongoni mwa Rais waliohudumu na kudumu mno katika Wizara ya mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa akiwa waziri wa wizara hiyo, hivyo kumuwezesha kusoma diplomasia za kimataifa zaidi na zaidi, ujanja wa diplomasia za uchumi na ulinzi duniani kwa umakini sana, aidha, ni moja ya viongozi walioiangalia jumuiya ya Afrika Mashariki kwa makini mno akitumia uzoefu wake kijeshi na kidiplomasia kusoma nchi wanachama na janja zao katika diplomasia ya kiuchumi na kiulinzi.Hongera Jakaya Kikwete Mungu akupe nguvu zaidi.

Jakaya Kikwete ni Mtanzania pekee kiongozi mkuu aliejumuishwa katika mikakati ya Helsinki kuhusu utandawazi na demokrasia duniani, kwa kutambua umuhimu wa diplomasia na amani Jakaya Kikwete mnamo tarehe 26/5/2013 alieleza kwenye kikao cha umoja wa nchi za Afrika kwamba ili nchi ya Kongo iwe na amani ya kudumu ni vyema kabisa Rais wa Uganda, Rais wa Rwanda na Rais wa Kongo- Kinshasa wakae chini na vikosi vya waasi kama vile Allied for Democratic Force For Liberation of Uganda na Democratic Forces for Liberation of Rwanda kwa kifupi ADF wamalize tofauti zao kuhusu Kongo, ni msukumo wake wa diplomasia ya amani ambayo haikuwapendeza baadhi ya viongozi husika.

Mawazo yake yangefanyiwa kazi basi amani ya Kongo ingetengemaa kabisa, Aidha, kwa kutambua umuhimu wa amani Maziwa makuu Mh Jakaya Kikwete alifikiria na kuruhusu vikosi vyetu vya majeshi vikalinde amani nchini Kongo na kwa umahiri wa majeshi yetu kikundi cha M-23 kilifurumishwa na kusambaratishwa vibaya sana. Hongera Jakaya Kikwete.


Baadhi ya mafanikio ya Mh Jakaya Kikwete katika anga la diplomasia ya kimataifa yalikua hivi:-
Mwaka 2007 alitunukiwa nishani ya amani ‘Most Excellent Order of the Pearl of Africa’ nchini Uganda.

Mwaka 2009 alitunukiwa nishani ya amani ‘Order of the Green Crescent of Comoros’ nchini Comoro



    • Alishirikiana na rais wastaafu Mh Benjamin Mkapa na Katibu Mkuu wa umoja wa Mataifa wa wakati huo Mh Koffi Annan kunusuru malumbano makubwa ya serikali ya Kenya yalisababishwa na matokeo tata ya uchaguzi wa mwaka 2007 hivyo kufanikiwa kushawishi kuundwa kwa serikali ya pamoja kati ya Rais Mwai kibaki na Raila Odinga.



 
alichotufanyia bwana huyu sina hamu naye, ila mwenyezi mungu ampe umri mrefu ashuhudie huu mnyoosho maana tulikuwa tunamkebehi sana. Kweli nimeamini malipo ni hapahapa duniani maana mzee alivubilia sana kebehi wakati buldoza linaanza kazi mwanzoni....
 
Dr. JK,
Alikuwa anachekacheka humo ndani ya nchi.

Ila nilimpenda kwa jambo kuu moja ambalo ni hili.
"Katu hakuchekacheka inapokuja kwenye jambo linalo husu usalama, amani ya Taifa Letu hasa kwa kuambatana na vikaragosi wa nchi jirani"

Nitarudi tena...
 
Inchi hovyo sana lkulu ikawa geto tukashuhudia mapedejee mgosha anafanya kaz nzuri ktk mazingira magumu Mke wangu kajifungua bure Hanna chakununua vifaa wala mini tens kijijini
 
Dr. JK,
Alikuwa anachekacheka humo ndani ya nchi.

Ila nilimpenda kwa jambo kuu moja ambalo ni hili.
"Katu hakuchekacheka inapokuja kwenye jambo linalo husu usalama, amani ya Taifa Letu hasa kwa kuambatana na vikaragosi wa nchi jirani"

Nitarudi tena...

Alikuwa anawajua hao Jirani zetu ni watu wa aina gani,ila huyu jamaa yao haelewi ameingi choo cha shimo tena kibovu
 
Kila mtu an mabaya na mazuri yake ila Magu....... mungu anakuona

Ni Nadra sana Duniani kumpata Kiongozi ambae ni Mwanajeshi Mstaafu Halafu ukute ni Mwanadiplomasia kwa kuwa kihistoria wanajeshi ni Watemi na Wababe

Ukiambiwa Jakaya alikuwa ndio Mwanajeshi na Magufuli sio Mwanajeshi huwezi kuamini kwa kuwa Style Yao ya Uongozi ingepaswa kuwa Tofauti


Sifa Kubwa ya Jakaya ambayo naiona exception ni kuweza Kufanya urafiki kwa ukaribu na Mataifa makubwa mawili Duniani ambayo ni Marekani na China kwa wakati Mmoja
 
Huko jeshini wr
Ni Nadra sana Duniani kumpata Kiongozi ambae ni Mwanajeshi Mstaafu Halafu ukute ni Mwanadiplomasia kwa kuwa kihistoria wanajeshi ni Watemi na Wababe

Ukiambiwa Jakaya alikuwa ndio Mwanajeshi na Magufuli sio Mwanajeshi huwezi kuamini kwa kuwa Style Yao ya Uongozi ingepaswa kuwa Tofauti


Sifa Kubwa ya Jakaya ambayo naiona exception ni kuweza Kufanya urafiki kwa ukaribu na Mataifa makubwa mawili Duniani ambayo ni Marekani na China kwa wakati Mmoja
wengine jeshini wapishi wengine walimu wa siasa kipindi cha nyuma sio wrote wapiganaji mpiganaji ana hulka tofauti
 
Back
Top Bottom