Ni ukweli usiobishaniwa kuwa J.Kikwete ni baba wa katiba mpya hapa Tanzania.
Kama kweli katiba mpya itapatikana.
Kama kweli katiba mpya itapatikana kwa haki na amani.
Kama kweli katiba mpya itapatikana bila kuingiliwa na ushabiki na masilahi ya CCM.
Kama kweli katiba mpya haitakuwa na mapungufu yaleyale yaliyomo kwenye katiba ya sasa.
Kama kweli katiba mpya haitaingiza "udini" ndani ya katiba hiyo.
Kama kweli katiba mpya itapunguza madaraka ya kifalme ya raisi.
Kama kweli katiba mpya italiongezea nguvu BUNGE katika kuisimamia serikali.
Kama kweli katiba mpya itaiweka huru tume ya uchaguzi.
Kama kweli katiba mpa itapunguza viongozi wa kuteuliwa na raisi.
Kama kweli katiba mpya itampa madaraka makubwa zaidi ya kiuamuzi waziri mkuu.
Kama kweli katiba mpya itamuondoa raisi katika kuwateua majaji.
Kama kweli katiba mpya itamuondoa raisi katika kumteua katibu mkuu wa BUNGE.
Kama kweli katiba mpya itawafanya wakuu wa mikoa wachaguliwe na moja kwa moja na wananchi.
Kama kweli katiba mpya itapunguza baaraza la mawaziri ni kuweka idadi maalum.
Kama kweli katiba mpya itaondoa au kuweka kikomo cha ubunge kwa viti maalum.
Kama kweli katiba mpya itaweka bayana kikomo cha mtu kuwa mbunge.
Kama kweli katiba mpya itatoa mfumo sahihi wa Muungano wanaoupenda wananchi walio wengi, yaani serikali tatu.
Kama kweli katiba mpya itakuwa kweli ya imetoka kwa wananchi, na kwa masilahi mapana ya wananchi.
BASI KWELI: Jakaya Mrisho Kikwete atastahili kuitwa "BABA WA KATIBA MPYA" hapa Tanzania. Kama itakuwa hivyo, basi napendekeza ijengwe sanamu yake katika viunga vya BUNGE huko Dodoma akiwa ameshika kitabu cha KATIBA MPYA, ili iingie vizuri kwenye historia ya nchi hii vizazi kwa vizazi.
Kama kweli katiba mpya itapatikana.
Kama kweli katiba mpya itapatikana kwa haki na amani.
Kama kweli katiba mpya itapatikana bila kuingiliwa na ushabiki na masilahi ya CCM.
Kama kweli katiba mpya haitakuwa na mapungufu yaleyale yaliyomo kwenye katiba ya sasa.
Kama kweli katiba mpya haitaingiza "udini" ndani ya katiba hiyo.
Kama kweli katiba mpya itapunguza madaraka ya kifalme ya raisi.
Kama kweli katiba mpya italiongezea nguvu BUNGE katika kuisimamia serikali.
Kama kweli katiba mpya itaiweka huru tume ya uchaguzi.
Kama kweli katiba mpa itapunguza viongozi wa kuteuliwa na raisi.
Kama kweli katiba mpya itampa madaraka makubwa zaidi ya kiuamuzi waziri mkuu.
Kama kweli katiba mpya itamuondoa raisi katika kuwateua majaji.
Kama kweli katiba mpya itamuondoa raisi katika kumteua katibu mkuu wa BUNGE.
Kama kweli katiba mpya itawafanya wakuu wa mikoa wachaguliwe na moja kwa moja na wananchi.
Kama kweli katiba mpya itapunguza baaraza la mawaziri ni kuweka idadi maalum.
Kama kweli katiba mpya itaondoa au kuweka kikomo cha ubunge kwa viti maalum.
Kama kweli katiba mpya itaweka bayana kikomo cha mtu kuwa mbunge.
Kama kweli katiba mpya itatoa mfumo sahihi wa Muungano wanaoupenda wananchi walio wengi, yaani serikali tatu.
Kama kweli katiba mpya itakuwa kweli ya imetoka kwa wananchi, na kwa masilahi mapana ya wananchi.
BASI KWELI: Jakaya Mrisho Kikwete atastahili kuitwa "BABA WA KATIBA MPYA" hapa Tanzania. Kama itakuwa hivyo, basi napendekeza ijengwe sanamu yake katika viunga vya BUNGE huko Dodoma akiwa ameshika kitabu cha KATIBA MPYA, ili iingie vizuri kwenye historia ya nchi hii vizazi kwa vizazi.