Return Of Undertaker
JF-Expert Member
- Jun 12, 2012
- 4,572
- 26,868
Jaji Joseph Warioba amesema vita dhidi ya rushwa na ufisadi inayoendelea nchini inawagusa wafanyabiashara na watumishi pekee, lakini inawazunguka viongozi.
Jaji Warioba, ambaye alikuwa mwenyekiti wa Tume ya Kuchunguza Kero ya Rushwa iliyoundwa Januari 17, 1996 na Rais Benjamin Mkapa, alisema hayo katika mahojiano maalumu na Mwananchi kuhusu miaka 20 baada ya kifo cha muasisi wake, Julius Nyerere.
Nyerere anaonekana kuwa kioo cha viongozi ambao hawakupenda rushwa na ambaye aliasisi Azimio la Arusha ambalo kwa kiasi kikubwa lilidhibiti viongozi kujiingiza kwenye uovu huo.
Pamoja na msimamo huo wa Nyerere na mikakati yake, Jaji Warioba anasema rushwa ilikuwepo, lakini anaona Serikali ya sasa imejikita kupambana nayo ila imesahau viongozi.
“Kwa upande wa rushwa kama kuna kitu kinanifanya nishabikie Serikali hii ni kupiga vita rushwa, ufisadi, kurudisha uadilifu, kurudisha nidhamu na kulinda rasilimali za Taifa,” alisema Jaji warioba ambaye alikuwa Waziri Mkuu kati ya mwaka 1985 na 1990.
“Sasa naona jitihada zinazofanywa za kupiga vita rushwa na ufisadi. Ni jitihada nzuri, lakini bado hazitoshi.
“Haya mambo huwezi kuondoa nafasi ya uongozi kama unapambana na rushwa. Na mpaka sasa, hii vita inaonekana inapita pembeni, ina deal (inashughulika) na wafanyabiashara na watumishi wa umma. Inaonekana kama viongozi hawahusiki ni wasafi, mimi siamini.
“Huwezi kuwa na nchi ambayo kuna rushwa na ufisadi, lakini viongozi wake wote ni wasafi na itafika mahali kama kweli tuko serious (makini) tuone tunapambana na rushwa na ufisadi ndani ya uongozi.”
Tangu Serikali ya awamu ya Tano iingie madarakani imejikita katika kupambana na ufisadi, wakwepa kodi, watakatishaji fedha na wahujumu uchumi.
Vita hiyo imekumba watumishi waandamizi wa serikali na wafanyabiashara, huku viongozi wakiadhibiwa kwa kutumbuliwa au kutakiwa kujiuzulu pale panapoonekana udhaifu katika majukumu yao.
Lakini Jaji warioba anaona bado vita hiyo haijashika vizuri.
“Kenya inatoa dalili nzuri kwamba hata wakubwa wanashughulikiwa,” alisema Jaji Warioba.
“Sasa hapa bado. Katika mfumo wetu wa siasa na hasa za uchaguzi kuna rushwa nyingi tu.”
Chanzo: Mwananchi
Jaji Warioba, ambaye alikuwa mwenyekiti wa Tume ya Kuchunguza Kero ya Rushwa iliyoundwa Januari 17, 1996 na Rais Benjamin Mkapa, alisema hayo katika mahojiano maalumu na Mwananchi kuhusu miaka 20 baada ya kifo cha muasisi wake, Julius Nyerere.
Nyerere anaonekana kuwa kioo cha viongozi ambao hawakupenda rushwa na ambaye aliasisi Azimio la Arusha ambalo kwa kiasi kikubwa lilidhibiti viongozi kujiingiza kwenye uovu huo.
Pamoja na msimamo huo wa Nyerere na mikakati yake, Jaji Warioba anasema rushwa ilikuwepo, lakini anaona Serikali ya sasa imejikita kupambana nayo ila imesahau viongozi.
“Kwa upande wa rushwa kama kuna kitu kinanifanya nishabikie Serikali hii ni kupiga vita rushwa, ufisadi, kurudisha uadilifu, kurudisha nidhamu na kulinda rasilimali za Taifa,” alisema Jaji warioba ambaye alikuwa Waziri Mkuu kati ya mwaka 1985 na 1990.
“Sasa naona jitihada zinazofanywa za kupiga vita rushwa na ufisadi. Ni jitihada nzuri, lakini bado hazitoshi.
“Haya mambo huwezi kuondoa nafasi ya uongozi kama unapambana na rushwa. Na mpaka sasa, hii vita inaonekana inapita pembeni, ina deal (inashughulika) na wafanyabiashara na watumishi wa umma. Inaonekana kama viongozi hawahusiki ni wasafi, mimi siamini.
“Huwezi kuwa na nchi ambayo kuna rushwa na ufisadi, lakini viongozi wake wote ni wasafi na itafika mahali kama kweli tuko serious (makini) tuone tunapambana na rushwa na ufisadi ndani ya uongozi.”
Tangu Serikali ya awamu ya Tano iingie madarakani imejikita katika kupambana na ufisadi, wakwepa kodi, watakatishaji fedha na wahujumu uchumi.
Vita hiyo imekumba watumishi waandamizi wa serikali na wafanyabiashara, huku viongozi wakiadhibiwa kwa kutumbuliwa au kutakiwa kujiuzulu pale panapoonekana udhaifu katika majukumu yao.
Lakini Jaji warioba anaona bado vita hiyo haijashika vizuri.
“Kenya inatoa dalili nzuri kwamba hata wakubwa wanashughulikiwa,” alisema Jaji Warioba.
“Sasa hapa bado. Katika mfumo wetu wa siasa na hasa za uchaguzi kuna rushwa nyingi tu.”
Chanzo: Mwananchi