Jaji Warioba: Siioni Katiba Mpya

Kama mimi ndiyo sielewi somo kabla hata hiyo rasimu hawajaipigia kura na kuipitisha nimeshaanza kampeni yangu ya mtu kwa mtu , mpaka 2016 nitakuwa nimeshakuwa na wafuasi maelfu wa kusema BIG NO KWA RASIMU YA KIFISADI YA BMK.
 
Kinachonishangaza ni kwa kwa mzee Warioba kuanza kutoa elimu kwa umma JUU ya rasimu yake sasa wakati alipewa pesa nyingi ili kuelimisha umma kwanini Tume yake ili andika rasimu kwa namna ile. Yote ingemsaidia Watu na wabunge kumuelewa. Alitumia muda mwingi kufafanua kwa nini anapendekeza kuuvunja muungano katika rasimu yake wakati akiiwasilisha bungeni ili kuhakikisha wananchi wa Pande mbili za muungano wanachukiana sana. Vitu vingine hata sisi wananchi tulikuwa hatuvijui . Sasa muda wake wa kuandika rasimu umekwisha kwa nini usitulie mzee Wangu upumzike baada ya kazi Ngumu? Kwanini unaona mawazo ya Tume yako pekee yanafaa ? Huoni wabunge wa bunge la katiba nao wanawawakilisha wananchi kwa mfano vijana, wanawake, wavuvi, wafugaji, wakulima, wafanyakazi, waajiri, wafanyabiashara, wanasiasa,NGO, wananchi kupitia wawakilishi majimboni. Je hayo makundi yote yaliyobaki bunge unaona mawazo yao waliyoyatumia kuboresha rasimu ya Tume hayana maslah kwa wananchi? Mi naomba mzee Wangu usitumike vibaya na kikundi kidogo cha wanasiasa na wafadhili wao ambao wana mipango yao ya 2015 wanajitahidi kuipigania kwa mgongo wako bila wewe kujua. Achana nao. Usipoteze nguvuzako waachie wanasiasa walumbane majukwaani na kwenye makongamano. Wananchi kwa mujibu wa sheria watapiga kura kufanya maamuzi. Hiyo ni katiba yao. Kazi yako umemaliza. Sitta kamaliza. Watanzania wataamua lini tumsubiri mwenye mamlaka aliyekuteua wewe na bunge la katiba atasema.
 
Kinachonishangaza ni kwa kwa mzee Warioba kuanza kutoa elimu kwa umma JUU ya rasimu yake sasa wakati alipewa pesa nyingi ili kuelimisha umma kwanini Tume yake ili andika rasimu kwa namna ile. Yote ingemsaidia Watu na wabunge kumuelewa. Alitumia muda mwingi kufafanua kwa nini anapendekeza kuuvunja muungano katika rasimu yake wakati akiiwasilisha bungeni ili kuhakikisha wananchi wa Pande mbili za muungano wanachukiana sana. Vitu vingine hata sisi wananchi tulikuwa hatuvijui . Sasa muda wake wa kuandika rasimu umekwisha kwa nini usitulie mzee Wangu upumzike baada ya kazi Ngumu? Kwanini unaona mawazo ya Tume yako pekee yanafaa ? Huoni wabunge wa bunge la katiba nao wanawawakilisha wananchi kwa mfano vijana, wanawake, wavuvi, wafugaji, wakulima, wafanyakazi, waajiri, wafanyabiashara, wanasiasa,NGO, wananchi kupitia wawakilishi majimboni. Je hayo makundi yote yaliyobaki bunge unaona mawazo yao waliyoyatumia kuboresha rasimu ya Tume hayana maslah kwa wananchi? Mi naomba mzee Wangu usitumike vibaya na kikundi kidogo cha wanasiasa na wafadhili wao ambao wana mipango yao ya 2015 wanajitahidi kuipigania kwa mgongo wako bila wewe kujua. Achana nao. Usipoteze nguvuzako waachie wanasiasa walumbane majukwaani na kwenye makongamano. Wananchi kwa mujibu wa sheria watapiga kura kufanya maamuzi. Hiyo ni katiba yao. Kazi yako umemaliza. Sitta kamaliza. Watanzania wataamua lini tumsubiri mwenye mamlaka aliyekuteua wewe na bunge la katiba atasema.

Nawewe unajihisi umeongea kitu cha maana sana,,,,,!!!!
 
Jana nimecheka sana nilipoangalia taarifa ya habari saa mbili usiku. Na takribani magazeti yote leo yameandika vile vile jamani? "NAWASUBIRI MTAANI-WARYOBA"
HIVI huyu mzee amechanganyikiwa nini? Bila aibu kabisa anasema anawasubiri wabunge wa Bunge Maalum la Katiba Mtaani wapambane, ili iweje? Yeye kama nani wakati alishamaliza kazi yake? je ni kazi yake kuwashawishi wananchi kukubali Rasimu yake au hajui maana ya rasimu?.
Tuamini kuwa yalioko kwenye rasimu yake ni mawazo yake na sasa anakwenda kutafuta ushawishi wa wananchi kuyakubali? Kama yalioko kwenye rasimu yake nj maoni ya watanzania 17000 kati ya mil.45 si asubiri tu wananchi wapelekewe ya rasimu ya tatu wenyewe wachambue ipi ni ipi?
Mwisho mnieleweshe tu wandugu wapenzi jana kulikuwa na nini kwenye mkutano ule na wandishi wa habari? Kituo cha sheria na haki za binadamu walikuwa wanaadhimisha siku ya kuanzishwa kwao? Ilikuwa ni uzinduzi wa kitabu cha Senkodo Mvungi au Waryoba aliitisha mkutano na wandishi wahabari kuelezea mchakato wa Katiba Mpya?
 
Huu ni mnyukano sijui itatufikisha wapi. huko tuendako nchi yetu itazidi kusambaratika.
We need maridhiano zaidi kuliko ubabe na mwisho wote tutapoteza.
Ooooh my Tanzania amani yetu ipo ICU na madaktari wakuweza kukuhudumia wamegoma
huku wakilumbana na kuonyeshana ufahari wa nani atakula paja, maini nafirigisi. wanalipwa 300,000 kwa siku
na still wanalalamika ubaridi umezidi ndani ya ukumbi wanapopiga story.
Wakati mkulima wa nkasi maindi yanaoza, Temeke hospital watoto 3 na wazazi wao kitanda kimoja na TCU ikiwatema zaidi ya 20,000 kwa kukosa mikopo.
Inauma sana.
 
"Kusikia kwa kenge mpaka damu imtoke masikioni...! " Muache Sitta na genge lake wamalizie wizi wao huo wa pesa zetu halafu wakione cha mtemakuni...Hawa ni kama viwavi ndani ya shamba la mahindi. Tutalipiga shamba zima dawa tuone kama kuna kiwavi atakaesalimika.....

Sitta ameishaanza kuwalalamikia waandishi wa habari eti hawampendi ndio maana wanamuandika vibaya na kwamba siku hizi anatumiwa messages za kumtukana!! Sitta kwa wakati huu is the most hated person zaidi ya hao wanaoitwa mafisadi papa!! Sijui atajisafishaje kutokana na najisi aliojipaka huko kwenye bunge la katiba!
 
Tume maarufu ya Mh jaji Warioba ya kukusanya maoni ilisheheni kila watu wenye sifa za aina yake!, kwa ufupi nitawa taja wachache; Dr Salim A Salim(Katibu mkuu OAU mstaafu), Mzee Butiku, R.I.P Dr Sengoro Mvungi, Prof Baregu, Polepole, n.k. Ili wananchi tuamini kuwa nanyinyi hamjatumia fedha zetu vibaya kama hao wanaoendelea kujadili katiba ambayo haitokani na maoni ya wananchi mliyo yakusanya, basi tunawaomba muanze mara moja kutetea maoni mliyo yakusanya bila aibu na bila kumuogopa mtu/kitu hapo ndio tutajua uzalendo wenu uko wapi. Maana haiwezekani kile mnacho kiamini kuwa ni kizuri kwa Taifa letu kiharibiwe huku wengi wenu mmekaa kimya!, lakini zaidi wananchi wanataka kama bahati mbaya katiba hiyo ikapitishwa ikapelekwa kwa wananchi kama ilivyo hivi sasa!, Mh Jaji Warioba na tume yako muungane nawengine kuwaelimasha wananchi waikatae katiba hiyo na hapo ndio tujua kuwa nanyi pia hamkutumia kodi zetu bure na ni wazalendo kwa Taifa letu.
 
Wale wajinga walikuwa wanalipwa 500,000 kwa siku na bado wakaja na Rasimu ambayo haina hata ibara moja ya wakulima, wafanyakazi, wafugaji, wasanii, wachimbaji wadogo wala ardhi, leo Waryoba anasema bila aibu eti anawasubiri wabunge wa bunge maalum la Katiba mtaani
 
Cybercrime, Katiba ya Warioba ilihusu mambo ya Muungano tu. Wasingeweza kujumuisha kila kitu. Mambo uliyoyataja kulingana na maelezo yao yangeshughulikiwa na katiba za nchi washirika.
 
"Kusikia kwa kenge mpaka damu imtoke masikioni...! " Muache Sitta na genge lake wamalizie wizi wao huo wa pesa zetu halafu wakione cha mtemakuni...Hawa ni kama viwavi ndani ya shamba la mahindi. Tutalipiga shamba zima dawa tuone kama kuna kiwavi atakaesalimika.....

Mzee warioba ni kati ya Tunu za taifa.
 
Nyie ibeeeeni ,tukorogeeeeeni,tudanganyeeeeeni siku tutakayo amua kuirudisha nchi yetu inapotakiwa kuwa kila mmoja wenu atajuta.mlivyo wajinga na huku mnapita mnasoma lakini mnajitia uziwi na upofu.iko siku yenu na Mungu alie juu atawaonyesha thamani ya mamlaka..yaone kwanza mfyuuuu
 
Sitta ameishaanza kuwalalamikia waandishi wa habari eti hawampendi ndio maana wanamuandika vibaya na kwamba siku hizi anatumiwa messages za kumtukana!! Sitta kwa wakati huu is the most hated person zaidi ya hao wanaoitwa mafisadi papa!! Sijui atajisafishaje kutokana na najisi aliojipaka huko kwenye bunge la katiba!

mkuu naona 6 na wapuuzi wenzake walio bungeni hawana nafasi ktk jamii ya watanzania wapenda haki.
 
Back
Top Bottom