Cute Wife
JF-Expert Member
- Nov 17, 2023
- 2,786
- 7,567
Wakuu,
Jaji Warioba ameendelea kuonyesha busara zake. Kama mpaka Spika na Bunge lake wanatoa tuzo kwa Rais, kusifia utendaji wake bora, chombo hicho kitakuwa na uhuru? Jaji Mkuu na Spika kutwa wapo kwenye vikao vya Rais, utasema mihimili hii inajitegemea?
Anasema walitoa mapendekezo mazuri kuhakikisha mihimili hiyo inakuwa huru, lakini mengi hayajatekelezwa japokuwa yalipokelewa na kukubalika.
Nachoka mimi shemeji wa Mwandambo!
======
Katika mahojiano na kituo cha Jamhuri, Jaji Mstaafu Warioba anasema walitoa mapendekezo kwenye mgawanyo wa madaraka kati ya serikali bunge na mahakama, ikionekana Bunge na Mahakama havikuwa imara, ili viimarishwe na kufanya kazi kwa kujitegemea.
Kwenye Bunge, wakasema kwakuwa tuna "Presidential System", mawaziri wasiwe kwenye Bunge, bunge lijisimamie (independent), Mawaziri Rais atatetua, ili tutenganishe serikali na bunge.
Mahakama pia walisema ipewe uhuru, ikiwemo kuwa na mahakama ya juu zaidi na pamoja na uhuru wa kifedha, ambapo kwa bunge imefanyika lakini kwa mahakama bado wanategemea hazina - mapendekezo hayo yalikubalika lakini hayajatekelezwa.
Sasa hivi Imekuwa kawaida na ni nchi pekee kwamba Jaji Mkuu na Spika wanahudhuria vikao vya Rais. Yaani inaonekana Bunge na Mahakama ni sehemu ya Executive. Tumesema hii kwamba sio vizuri, ni kama utaratibu wa Dictatorship kuona Spika na Jaji Mkuu wanakuwa washauri wa Rais.
Anasema, wananchi wakiwaona , wakiwa wanahudhuria vikao vya Rais, hawataamini kwamba wanapata maagizo kutoka kwa Rais, watakuwa wanazunguma! Hili linaendelea mpaka sasa. Ukiona Spika anakwenda kwenye kikao cha Rais, anazungumza pale wabunge wale watafuta.
Jaji Warioba ameendelea kuonyesha busara zake. Kama mpaka Spika na Bunge lake wanatoa tuzo kwa Rais, kusifia utendaji wake bora, chombo hicho kitakuwa na uhuru? Jaji Mkuu na Spika kutwa wapo kwenye vikao vya Rais, utasema mihimili hii inajitegemea?
Anasema walitoa mapendekezo mazuri kuhakikisha mihimili hiyo inakuwa huru, lakini mengi hayajatekelezwa japokuwa yalipokelewa na kukubalika.
Nachoka mimi shemeji wa Mwandambo!
======
Katika mahojiano na kituo cha Jamhuri, Jaji Mstaafu Warioba anasema walitoa mapendekezo kwenye mgawanyo wa madaraka kati ya serikali bunge na mahakama, ikionekana Bunge na Mahakama havikuwa imara, ili viimarishwe na kufanya kazi kwa kujitegemea.
Kwenye Bunge, wakasema kwakuwa tuna "Presidential System", mawaziri wasiwe kwenye Bunge, bunge lijisimamie (independent), Mawaziri Rais atatetua, ili tutenganishe serikali na bunge.
Mahakama pia walisema ipewe uhuru, ikiwemo kuwa na mahakama ya juu zaidi na pamoja na uhuru wa kifedha, ambapo kwa bunge imefanyika lakini kwa mahakama bado wanategemea hazina - mapendekezo hayo yalikubalika lakini hayajatekelezwa.
Sasa hivi Imekuwa kawaida na ni nchi pekee kwamba Jaji Mkuu na Spika wanahudhuria vikao vya Rais. Yaani inaonekana Bunge na Mahakama ni sehemu ya Executive. Tumesema hii kwamba sio vizuri, ni kama utaratibu wa Dictatorship kuona Spika na Jaji Mkuu wanakuwa washauri wa Rais.
Anasema, wananchi wakiwaona , wakiwa wanahudhuria vikao vya Rais, hawataamini kwamba wanapata maagizo kutoka kwa Rais, watakuwa wanazunguma! Hili linaendelea mpaka sasa. Ukiona Spika anakwenda kwenye kikao cha Rais, anazungumza pale wabunge wale watafuta.