Jaji Mkuu Kushiriki Hukumu ya Lema

Du sasa kweli wadau huyu Jaji mkuu ndo atatenda haki au ndo wanatuzuga ili tujue ishue ya lema wameishughulikia kikamilifu ? mm hawa ccm siwaamini kabisaaa.
 
Kama jaji mkuu yumo, wajitahidi watende haki maana itakuwa aibu ya mwaka kama naye ataingia katika kurudia makosa ya aliyetengua ubunge wa lema!

Kwa hiyo unachotaka ni ku-rule in favour of Lema /Chadema na sio haki kutendeka! Kama Chadema wakishindwa kwenye kesi unaita aibu kwa serikali,what if serikali ikishindwa inakuwa ni aibu kwa nani? Isitoshe kwa nini unafikiria kushindwa kwenye kesi ni aibu,au hujui ukijenga fikra zako katika itikadi hiyo ipo siku utaogopa kudai haki yako kwa kuogopa aibu ya kushindwa. Badilika kifikra..think...usichoke!
 
Tundu Lissu ni kiboko ni kati ya wanasheria wachache sana duniani ambao sio waoga aliwachana live kitu ambacho kwa upande wa ccm hawakiwezi kabisa

Na bado akawavua nguo kwa kuwafahamisha kuwa waziri hana mamlka ya kuunda tume isipokuwa rais!! wakabaki wanakodoa macho utafikiri panya kakamatwa na mtego
 
ukae ukijua hakutakua na jipya kwenye hi hukumu
sababu Majaji wote badala yakufanya kazi yao watafanya kazi kutokana na instraction za kiongozi wao

ningumu sana kumbishia ama kukataa ushouri wa anaye kupa ugali
 
Exclusive:Lema amerudishiwa ubunge wake.
Keep it in your mind because you will screming it later
 
wadau wa JF,
Ninasikiliza kipindi cha magazeti cha RFA nimesikia kuwa jaji chande atasikiliza kesi ya lema akishirikiana na jaji kimaro na jaji masati. kwa hiyo yule mwanafunzi wa open university ndg mbarouk mbarouk kapigwa chini. kumbe tundu lisu alisema kweli. viva cdm!

hivi ile kesi ya yule jamaa wa mtandao wa wizi wa magari Tanzania kutoka kule arusha bado inaendelea?
 
Kama judge mkuu kaamua kushikilia hiyo? Je anakwenda kubariki hukumu ya kihuni ya jaji alietangulia au anakwenda kuonyesha umahiri wake wa kisheria,?
Juzi juzi tulimsikia RC wa Arusha akisema amani kwanza, haki baadae.
Hii kauli ina maana gani kwa Taifa??
 
Huyu chizi alishafukuzwa na makopo yake sioni sababu ya kuendelea kumzungumzia.Hata baraza la kata linaweza kusikiliza rufani ya Lema.

mingoi kwa lugha yetu ni mwanamke mwenye waume wengi sanaaaaaa

Viva kamanda lema

V
SENGEREMA
 
Daah, Naomba Lema ashindwe katika Rufaa yake. Ni heri zaidi Kamanda Lema awe kitaani akiwaburuza na M4C bwana. Akiwa na misutisuti ya ubunge m4c haitanoga banaaa hahahahaaaaaa
 
Mbona niliwahi kusikia kuwa hata jaji mkuu pia hajawahi kiandika judgement yeyote?!
Mwenye ukweli juu ya hili tafadhali atujuze!
 
Jaji Mkuu Augustino Ramadhan? yule aliyepindisha hukumu ya mgombea binafsi kutaka fadhila baada ya kustaafu(makamu mwenyekiti tume ya katiba)
Mh JM Chande hawezi kumuuzi boss wake, Yangu macho

Mbarouk hawez kuwepo kwa sababu siku hiyo kuna mtihani wa OLW 146,ambao alikuwa ame-carry,iyo pepa yupo pa1 na washikaj wa2 wapo humu jf.lakin aftr exams bak to buznes as ussual
 
Kwa kweli Mh Lissu nampenda sana na hakika kuingia kwenye kesi ya Lema tutegemee mambo mazuri maana huyu Mh ni mahiri wa kujenga hoja zenye mashiko
 
Why Jaji mkuu kwenye rufaa ya LEMA? Kesi yake ilikuwa ngumu sana majaji wengine kushindwa?, au kutakuwa na utashi wa siasa ndani yake?

HIVI jaji mkuu hana kazi za kufanya mbona kesi ngumu kama za EPA hakuhusishwa? Huyu ametumwa tu na adui namba moja wa Lema JK kuvuruga hukumu ili magamba waendelee kutumia rasilimali za wakazi wa Arusha. Wako majaji kibao competent iweje huyu mwakilishi wa CCM awe kwenye kundi la watoa hukumu. Ukisikia kesi ya kuamuliwa na simba ndiyo hii .
 
Wameamua kumuengua bwana mbarouk baada ya kupata taarifa tindu lissu kaongezwa katika list ya mawakili wa upande wa utetezi. mbarouk na lissu ni vitu viwili tofauti kabisa (lila na fila hazitangamani). Naona sasa kiwango cha lissu ni cha kumpambanisha na jaji mkuu, inamaana hakuna majaji wengine ambao wanauwezo wa kupambana na lissu?
Naomba upande wa batrida wamuongeze werema upande wa mawakili wake apo tuone bonge la senema.
 
Kama judge mkuu kaamua kushikilia hiyo? Je anakwenda kubariki hukumu ya kihuni ya jaji alietangulia au anakwenda kuonyesha umahiri wake wa kisheria,?
Juzi juzi tulimsikia RC wa Arusha akisema amani kwanza, haki baadae.
Hii kauli ina maana gani kwa Taifa??


Nataka viongozi wakubwa wa serikalini watueleze ni lini amani ilitoweka Arusha na nani aliitowesha na ni lini ilirudi. Lema hajawahi ua mtu au kupiga ila utasikia amani Arusha ilitoweka. HIvi Dar, Songea, Mbeya na juzi Iringa, Tarime n.k hivi nako huko kuna Lema! Wao wasema wanataka jimbo ila wasijaribu kujidai Arusha hakuna amani. Amani Arusha haijawahi toweka kwani hakuna watu waliohama makazi wala kukimbilia nchi jirani na hapakuwepo watu wanapigana vita bali raia waliamua kudai haki yao.
 
Back
Top Bottom