Jaji Bomani awachafua wazanzibari

Jaji Bomani awachafua wazanzibari

Na hili la Maalim Sefu kujipa nafasi ya ZEC na kujitangaza mshindi nalo mnalisemeaje. na ile idadi ya wapiga kura iliyozidi kule Pemba watu wakae kimya, hizo siyo dosari zisisemwe? unafki huo. uchaguzi urudiwe tu. CUF wajiamini. kama ushindi ni wao wataupata tu.
Wewe unasema wapiga kura walizidi huko Pemba.
Sasa nikuulize swali moja tu jepesi, hivi si kila kituo kulikuwa na mawakala wa vyama vyote?
Sasa kama mawakala hao, pamoja na wa vyama vya CCM na CUF waliweka saini ya fomu za matokeo, ikiwa na maana walikuwa wamejiridhisha kuwa uchaguzi haukuwa na kasoro zozote.
Sasa huyo Jecha kukurupuka na kutangaza kuyafuta matokeo hayo tena bila kushirikisha makamishna wenzake wa ZEC, hivi huo bado
haujawa ushahidi wa kutosha wa mazingira kuwa Jecha 'aliamriwa' na CCM kutoa tamko hilo baada ya kugundua ya kuwa mgombea wao Dr Shein amebwagwa na Maalim Seif?
Kwa hali inayoendelea nchini mwetu ya CCM kutaka kung'ang'ania madarakani hata kwenye yale maeneo wanayojua dhahiri wameshindwa, kutakuja kuiletea maafa nchi hii.
Mfano halisi ni uchaguzi huo wa Zanzibar na hivi sasa umehamia kwenye uchaguzi wa mameya huku Bara.
Tumeshuhudia huko Tanga jana namna uchaguzi wa meya wa huko, namna msimamizi wa uchaguzi alivyoamua kumtangaza mgombea wa CCM ambaye alishindwa kuwa ndiye mshindi na mgombea wa CUF ambaye ndiye aliyeshinda akatangazwa kushindwa!
Hata hivyo kama lilivyotokea kwa Jecha baada ya kuyafuta matokeo ya Zanzibar 'akapelekwa' mafichoni, vivyo hivyo kwa msimamizi wa uchaguzi wa jijini Tanga, naye amesepa kwenda mafichoni mara tu baada ya kutangaza kuwa mgombea wa CCM kuwa ndiye aliyeshinda uchaguzi.
Hivi kama kweli msimamizi huyo angekuwa ametangaza kitu ambacho yeye aliamini ndicho sahihi, ni kitu gani kilichomtoa nduki baada ya kuyatangaza matokeo hayo??!!!!
 
Kama kweli jaji ameongea haya basi akapimwe akili!!!
Huyo Bomani ambaye aliwahi kuwa Mwanasheria Mkuu wa serikali, kwa kuyatamka hayo ameishusha taaluma yake ya uanasheria kwa kiwango cha hali ya juu sana.
Ninaamini kuwa huyo mzee ameamua kuiweka 'rehani' pale Lumumba hiyo taaluma yake ya uanasheria.
 
Na hili la Maalim Sefu kujipa nafasi ya ZEC na kujitangaza mshindi nalo mnalisemeaje. na ile idadi ya wapiga kura iliyozidi kule Pemba watu wakae kimya, hizo siyo dosari zisisemwe? unafki huo. uchaguzi urudiwe tu. CUF wajiamini. kama ushindi ni wao wataupata tu.

Toa ushahidi
 
Wewe unasema wapiga kura walizidi huko Pemba.
Sasa nikuulize swali moja tu jepesi, hivi si kila kituo kulikuwa na mawakala wa vyama vyote?
Sasa kama mawakala hao, pamoja na wa vyama vya CCM na CUF waliweka saini ya fomu za matokeo, ikiwa na maana walikuwa wamejiridhisha kuwa uchaguzi haukuwa na kasoro zozote.
Sasa huyo Jecha kukurupuka na kutangaza kuyafuta matokeo hayo tena bila kushirikisha makamishna wenzake wa ZEC, hivi huo bado
haujawa ushahidi wa kutosha wa mazingira kuwa Jecha 'aliamriwa' na CCM kutoa tamko hilo baada ya kugundua ya kuwa mgombea wao Dr Shein amebwagwa na Maalim Seif?
Kwa hali inayoendelea nchini mwetu ya CCM kutaka kung'ang'ania madarakani hata kwenye yale maeneo wanayojua dhahiri wameshindwa, kutakuja kuiletea maafa nchi hii.
Mfano halisi ni uchaguzi huo wa Zanzibar na hivi sasa umehamia kwenye uchaguzi wa mameya huku Bara.
Tumeshuhudia huko Tanga jana namna uchaguzi wa meya wa huko, namna msimamizi wa uchaguxi alivyoamua kumtangaza mgombea wa CCM ambaye alishindwa kuwa ndiye mshindi na mgombea wa CUF ambaye ndiye aliyeshinda akatangazwa kushindwa!
Hata hivyo kama lilivyotokea kwa Jecha baada ya kuyafuta matokeo ya Zanzibar 'akapelekwa' mafichoni, vivyo hivyo kwa msimamizi wa uchaguzi wa jijini Tanga, naye amepelekwa mafichoni mara tu baada ya kutangaza kuwa mgombea wa CCM kuwa ndiye aliyeshinda uchaguzi.
Hivi kama kweli msimamizi huyo angekuwa ametangaza kitu ambacho yeye aliamini ndicho sahihi, ni kitu gani kilichomtoa nduki baada ya kuyatangaza matokeo hayo??!!!!

Ahsante sana

Nakumbuka kauli ya Rais wananchi warudi nyumbani baada ya kupiga kura, hakuna kulindwa kura, kila chama kina wakala wa kulinda kura,na kila kituo kuna list ya wapiga kura, jee walikuwa wapi hao mawakala?
 
CCM mna unafiki wa hali ya juu.
Uchaguzi ulishafanyika na ulikwisha.
Matokeo yote yalishatangazwa majimboni. Matokeo ya wawakilishi yaliishia kwa walioshinda uwakilishi kupewa vyeti wa ushindi. Matokeo ya kura za uraisi pia yalibandikwa majimboni. Ni matokeo hayo yanayompa mgombea wa CUF ushindi na ni matokeo hayo yanayoonesha mgombea wa nafasi ya uraisi kupitia CCM ameangukia pua.

CCM imeamua kubaka demokrasia na kumwamuru Mwenyekiti wa Tume "huru", ZEC afute uchaguzi na matokeo yake bila ya kuwepo na malalamiko yaliyowasilishwa na mawakala wa vyama.

Kurudia uchaguzi ni uhuni wa CCM wa kutaka kufunga goli la Nape. Kama CCM ilishinda uchaguzi ule Jecha angekuwa na ubavu wa kufuta uchaguzi au matokeo?

CCM mnaiharibu nchi hii, CCM mnaichezea amani ya nchi. CCM iheshimu maamuzi ya wapiga kura.

Siri iko nje, tokea 1995 CCM haijawahi kushinda uchaguzi mkuu huko Zanzibar lakini Mwanyekiti wa ZEC amekuwa akilazimishwa kumtangaza mgombea wa CCM ameshinda.

Mimi nashangaa kwa nini Msajili wa vyama hajakifuta CCM kwa uhuni huu wanaoufanya kwa miongo miwili sasa. Hapo ndio utafahamu maana ya Chama dola.

Imeripotiwa Makamo Mwenyekiti alitekwa nyara na vyombo vya dola ili asiendelee kutangaza matokeo ya uchaguzi. Kwa nini alichukuliwa na vyombo vya dola? Nani aliamrisha uhuni huo? Huyo aliyeamrisha ndie alivuruga uchaguzi.

Ni wazi hilo lilifanyika ili kuminya na kuzuia haki isitendeke na ni ubakaji wa demokrasia.

Kwa vyovyote wote, waliohakikisha wanazuia matokeo yasiendelee kutangazwa wamefanya hivyo kwa malengo ya kukibeba CCM na hiyo ndio "siri" ya ukasuku wa "uchaguzi urudiwe".

CCM na wanachama wa CCM wamejigeuza makasuku na kauli mbiu ni "uchuguzi urudiwe".

Kwa nini CCM haitaki yale matokeo yaliyotangazwa na yaliyobandikwa vituoni, majimboni baada ya kuhesabiwa kura yasitangazwe na mwenyekiti wa ZEC?

CCM inabaka demokrasia na kutishia amani ya nchi yetu.

Huu ni mtihani kwa Magufuli . Magufuli atabakia kuwa msema kweli na kuukana unafiki wa CCM? Nimkumbushe tu , Raisi Pombe wa Magufuli alisema "mimi nauchukia unafiki, mimi ni msema kweli na msema kweli ni mpenzi wa Mungu"

Raisi Magufuli ajiulize;je aliye mnafiki na anayepindisha ukweli na anayebariki au kufumbia macho dhuluma kutendeka ni mpenzi wa nani?
Pokea like zangu 100 kwa mpigo.
Huo ni ukweli mtupu wa asilimia 100 uliompa Mheshimiwa Rais wetu Magufuli ili autafakari na kuuchukulia hatua.
Kwa hiyo kazi imebaki kwake aidha kusuka au kunyoa.
 
Mayor....uchaguzi wake Tanga.Mayor.......uchaguzi wake kinondoni.......na Mayor uchaguzi wake Ilala.Tuiombee Burundi amani.
 
Jaji Bomani hawezi kupendekeza liundwe jopo hapohapo akisema uchaguzi urudiwe, angeacha jopo liamue.
 
Ngigana Watanzania wa Zanzibari Uchaguzi umeishapita, Tafadhari kuondoa hii kadhia Matokeo yatangazwe, mshindi kwa asilimia sitini anajulikana!!
MaCCM kubali kushindwa Uchaguzi wa Zanzibari, mpeni Maalimu Seif na CUF nchi!!!
Fanyeni maridhiano wakiwa na Serikali yao, mnataka tulipuliwe mabomu??
 
Last edited by a moderator:
Inasikitisha sana kama nchi kuwa na watu kama bomani.Unategemea kuwa watakuwa wakombozi kwa weledi walio nao lakini wanageuka vibaraka wachumia tumbo.
 
Duuuh huyu bomani hora angekaa kimya tu kuliko kujidhalilisha huku

Tatizo la watu wa kina Bomani ni kutanguliza UKEREKETWA NA UKADA na si TAALUMA NA UKWELI, huu ni ugonjwa kwa wataalamu wetu na hata washauri wa viongozi wetu wakubwa. Kwa hali hii watu wasimshangae jaji Bomani bali ekemewe .
 
Tatizo la watu wa kina Bomani ni kutanguliza UKEREKETWA NA UKADA na si TAALUMA NA UKWELI, huu ni ugonjwa kwa wataalamu wetu na hata washauri wa viongozi wetu wakubwa. Kwa hali hii watu wasimshangae jaji Bomani bali ekemewe .

Tusisahau kwamba kutenganisha majukumu masuala yauchaguzi na muungano ni kuwatukana na kuwadhihaki waasisi wa muungano walio uunganisha kwa ishara ya mchanga. Hakika km matokeo ya uchaguzi Zanzibar ni batili basi na huku bara tunaongozwa na serikali batili.
 
Tuendako ni hatari sana na kama swala la Zanzibar litachukuliwa kizarau....wataanza kujitoa muhanga tena zaidi bara
 
Alichokifanya Maalim ni sawa na mwanafunzi wa kidato cha nne alieliona jina lake kwenye karatasi ya waliofaulu kwenye ukuta wa shule na kusema kuwa amefaulu ila anasubiria kutangazwa kwenye redioni tu.
 
Uchaguzi mkuu Zanzibar, Chaguzi za mameya Tanga, Ilala, Kinondoni-zinaonyesha dhahiri ni chama gani kinachovuruga chaguzi na amani Tanzania halafu vyombo vya dola vinaclaim kuwa na inteligensia.
 
Mkuu umenena haswa mimi kwa uono wangu tokea hapo zamani nilikuwa siamini kama tuna wasomi nchini ila kuna watu wenye njaa na kutaka kula yao isiwekewe kizuwio. Watu kama Shivji,Mwakyembe na wasomi wengine kwanini wanaweka maslahi ya chama kwanza kuliko nchi. Pia ukitaka kujua kama sisi Watanzania tuna matatizo ya akili angalia leo tuna Prof Ibrahim Lipumba ni Proffessor wa uchumi kwanini tusimtumie kuukuza uchumi?? lakini utaambiwa sio ccm. Ndio maana au mtu kasomea Medical lakini unamkuta yupo Bot na aliesomea Politics ndio utasikia waziri wa afya mmhh kweli sie masokwe.:crazy:
 
karibuni tutamuona jaji warioba kwenye itv atakuja kusema haya haya aliyosema jaji bomani kwa style tafauti kidogo lakini ujumbe utakuwa ule ule ni msimamo wa ccm,
ccm wanawabana hawa wazee kwenye koo kwa kamba ya pension na matibabu wanawaburuza kila wanapowahitaji kuwatumia
kwa wazee wenye kehma na busara kama hawa wanapokuja kukinzana na taaluma zao na ufahamu wa hali halisi ni aibu sana
 
Back
Top Bottom