Jaji Bomani awachafua wazanzibari

Jaji Bomani awachafua wazanzibari

GHIBUU

JF-Expert Member
Joined
Jan 13, 2011
Posts
4,432
Reaction score
3,016
Na Gwamaka Alipipi
18th December 2015

Aliyewahi kuwa Mwanasheria Mkuu na Jaji mstaafu, Mark Bomani ameshauri liundwe jopo la wataalam wa masuala ya uchaguzi kubaini na kuzifanyia kazi dosari zilitokea katika mgogoro wa uchaguzi Zanzibar.

Jaji Bomani amesema jopo hilo lijumuishe wajumbe kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Idara ya Uchaguzi ya Umoja wa Madola (Commonwealth), Umoja wa Afrika (AU) na liongozwe na Jaji Mkuu.

Aidha, amesema baada ya kuundwa kwa jopo hilo, daftari la wapiga kura lipitiwe kwa umakini kubaini dosari hizo kisha uchaguzi urudiwe haraka hata ikiwezekana ndani ya siku 30 tangu kuundwa kwa jopo hilo.

Alisema kama mgogoro wa Zanzibar hautapatiwa ufumbuzi haraka, madhara yake ni makubwa kwa taifa kwa kuwa hakutakuwa na serikali halali iliyochaguliwa na wananchi.

Jaji Bomani ametoa kauli hiyo tayari zimepita siku 73 tangu matokeo ya uchaguzi mkuu kufutwa na Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha kwa kile kilichoelezwa kuwapo kwa kasoro kadhaa zilizojitokeza wakati wa kupiga na kuhesabu kura.

Kufutwa kwa matokeo hayo, hadi sasa muafaka wa kutatua mgogoro huo visiwani Zanzibar haujapatikana, huku mgombea urais kupitia Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad akidai kuwa yeye ndiye mshindi wa uchaguzi huo.

Maalim Seif anadai kuwa alipata kura 200,007 sawa na asilimia 52.87 baada ya chama chake kukusanya fomu za matokeo vituoni na kufanya majumuisho.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Jaji Bomani alisema baada kurudiwa kwa uchaguzi huo, jopo hilo litatakiwa liendelee kuwapo wakati wa kurudia uchaguzi, ili lishuhudie mwenendo wote wa uchaguzi.

Alisema kabla ya uchaguzi huo kurudiwa, wagombea wote pamoja na vyama vyao wale kiapo kwa kuahidi kukubali matokeo ya uchaguzi wa marudio.

Jaji Bomani alisema mgogoro uliopo sasa Zanzibar, hauwezi kupatiwa ufumbuzi bila kufuata sheria na katiba.

?Njia pekee ambayo inaweza kumaliza mgogoro huu wa Zanzibar ni kwa uchaguzi kurudiwa bila ya kuchelewa, lakini chini ya masharti ya haki, uwazi na yanayoridhisha,? alisema Jaji Bomani.

Aliongeza kuwa Maalim Seif asiendelee kujitangaza kuwa mshindi na wala asiogope uchaguzi kurudiwa kwani wananchi waliompigia kura hapo awali watarudia kufanya hivyo katika uchaguzi wa marudio na pengine kuongezeka.

Alisema kujitangaza kuwa mshindi, haileti maana yoyote kwa kuwa ZEC, ndiyo inayomtangaza mshindi kisha kuapishwa na Jaji Mkuu.

AKERWA NA RUSHWA
Jaji Bomani alisema anasikitishwa na vitendo vya rushwa au matumizi ya fedha chafu vilivyokuwa vinatokea wakati wa uchaguzi mkuu uliopita.

Alisema baadhi ya wagombea kwa kiasi kikubwa walikuwa wanatumia fedha chafu kama hongo na kushinda uchaguzi na kueleza kuwa: ?Hilo jambo linastahili kukemewa na kulaaniwa.?

KATIBA MPYA
Jaji Bobani alisema mchakato wa kupata Katiba mpya uendelee, lakini mpaka mgogoro wa Zanzibar utakapotatuliwa na kupatikana kwa serikali mpya ya Zanzibar.

Kuhusu migogoro ya ardhi na ile ya wafugaji na wakulima, Jaji Bomani alisema: ?Serikali inapaswa kuweka kipaumbele cha hali ya juu kwa sekta ya ufugaji kutambuliwa.?

CHANZO: NIPASHE


Bonge 19/12/2015 kwa 10:01 mu ? Jibu
Aibu kwa Mark Bomani, bora angenyamaza kimya kulinda hadhi yake, Bila shaka amekurupuka pasi na kufanya uchambuzi wa kina katika jambo hili.
Hebu tuzichambue hoja zake za kipuuzi:
Amesema: ?liundwe jopo la wataalam wa masuala ya uchaguzi kubaini na kuzifanyia kazi dosari zilitokea katika mgogoro wa uchaguzi Zanzibar?
Kwanza, mgogoro wa Zanzibar ni wakutengeza baada ya CCM kushindwa kwa lugha nyengine ?hakuna mgogoro? ni ujanja wa kung?ang?ania madaraka tu!
Pili, dosari zipi anazozizungumza hali ya kuwa hakuna fomu za malalamiko kutoka kwa mawakala wa vyama? Bora angependekeza jopo liundwe kuchunguza Dosari nyingi za wazi zilizotokea katika uchaguzi wa Tanganyika lakini amefumbia macho kwa kuwa CCM imelazimisha ushindi.
Amesema: ?jopo hilo lijumuishe wajumbe kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Idara ya Uchaguzi ya Umoja wa Madola (Commonwealth), Umoja wa Afrika (AU) na liongozwe na Jaji Mkuu?
Huyu mzee alikuwepo wapi wakati Jumuiya ya Madola, Jumuiya ya Ulaya, Umoja wa Africa, Jumuiya ya Afrika Mashariki na SADC walipotoa ripoti yao kuwa uchaguzi hususan wa Zanzibar ulikua huru, haki na uwazi na wamesikitishwa kufutwa kwa uchaguzi. Anadhani hawa jamaa ni wapumbavu kama yeye, eti leo uwaite tena wachunguze upuuzi wa CCM?
Amesema: ? baada ya kuundwa kwa jopo hilo, daftari la wapiga kura lipitiwe kwa umakini kubaini dosari hizo kisha uchaguzi urudiwe?
Kabla ya uchaguzi wapinzani walipiga kelele nyingi kuhusu daftari la wapiga kura, Yeye alikuwepo wapi wakati huo ili kupendekeza kuwa liundwe jopo la kupitia daftari hilo? Huyu mzee punguwani! Leo baada ya CCM kushindwa anakuja na hoja za kipuuzi za kuchunguza daftari.
Eti ?uchaguzi urudiwe haraka? Swali, kipengele kipi cha katiba au sheria ya uchaguzi kinachompa mamlaka Jecha kufuta uchaguzi? Je uchaguzi ulioharibika ni wa raisi tu? Wawakilishi wote walishakabidhiwa vyeti vya uthibitisho wa ushindi na uchaguzi ulishamalizika tokea 25 Oktoba. Jamani huyu ni mwanasheri gani? Au alikuwa ameshalewa? Je, sababu zipi za msingi zinazopelekea kurudiwa kwa uchaguzi? Kura 5 zilipigwa katika kituo kimoja, wasimamizi walewale, wapigakura haohao, kura 4 zilienda sawa lakini ya uraisi wa Zanzibar zimeharibika!
Huyu Mzee ni kibaraka wa CCM na usomi wake tanautilia mashaka, ameshindwa kutaja hoja za walio wengi wanaodai kuwa uchaguzi ulikuwa huru, haki na wazi hivyo hakuna haja ya kurudia uchaguzi bali mshindi wa uchaguzi atangazwe. Yeye amekariri hoja za CCM eti ?Njia pekee ambayo inaweza kumaliza mgogoro huu wa Zanzibar ni kwa uchaguzi kurudiwa bila ya kuchelewa?. Wazanzibari tunakwambia, uchaguzi haurejewi na mara hii Tanganyika mtaonja joto ya jiwe kwa hili mpaka mtakapoitema Zanzibar.
Jaji Bomani alisema mgogoro uliopo sasa Zanzibar, hauwezi kupatiwa ufumbuzi bila kufuata sheria na katiba. Shabash! Katiba na sheria zipo wazi kuwa, uchaguzi ulishamaliza tokea tarehe 25, Mwenyekiti wa tume hana mamlaka ya kufuta uchaguzi, hakuna chama kilichowasilisha fomu za malalamiko, wawakilishi walishapewa vyeti vya ushindi, wabunge na Raisi wa Jamhuri walishaapishwa, majimbo 31 yalishatangazwa, kilichobaki ni kumtangaza mshindi wa uraisi wa Zanzibar.
Hivi Bomani na CCM wenzio mnaogopa nini kuachia madaraka hali ya kuwa wananchi walishaamua kuwaondoa madarakani?
Mnachoweza kufanya ni kuchelewesha kutenda haki lakini hamuwezi kuepuka wimbi la mabadiliko, mkijaribu kuforce mtaiyona people?s power, na Tanzania haitatawalika tena!


rasmi 18/12/2015 kwa 8:41 um ? Jibu
?
Khasara za Nyerere
In June, The Economist of London had declared, in an article entitled ?The Perils of Nyerere,? that the President had ?managed half the work of a python.? It continued: ?He swallowed Zanzibar all right but he did not crush its fighting force first. The live animal is a long time digesting, and its kicks are being felt hurtfully, and possibly even fatally, deep inside Tanganyika?s body politic.? Kutoka kitabu cha William Edgett Smith in We Must Run While They Walk: A Portait of Africa?s JULIUS NYERERE. p. 179.
Jarida la The Economist la London lilitangaza katika makala iitwayo ?Khasara za Nyerere.? Kuwa Rais [Nyerere] ?ameifanya nusu ya kazi ya chatu.? Makala inaendelea: ?Ameimeza Zanzibar, sawa, lakini hakuzizuwa nguvu zake za kujitetea kwanza. Mnyama [Zanzibar] yuhai na kwa muda mrefu amekuwa anaendelea kula, na mateke yake yenye kuumiza na yenye uwezo wa kuuwa yanapiga ndani ya tumbo la utawala wa Tanganyika.? From William Edgett Smith in We Must Run While They Walk: A Portait of Africa?s JULIUS NYERERE. Ukurasa wa 179
Quote kutoka facebook page ya Jamhuri Ya Watu Wa Zanzibar.
Huyo Jaji ni mmoja wa waendelezaji wa kazi ya Nyerere, kwa Zanzibar amenoa?

Jibu: Moyo

Huyu bomani anakuja na maneno ya kilevi! Mimi nilivyosikia anataka kuzungumza na waandishi wa khabari nilidhani anataka kuwaambia kweli ccm kumbe kaja na upuuzi huu.
Uchaguzi urudiwe kwa sababu gani! Uchaguzi ulikuwa huru na usio na mizengwe ukilinganisha na chaguzi zote zilizopita huko nyuma, hapakuwa na malalamiko wakati wa uchaguzi kutoka katika vyama vyote, matokeo yameshatangazwa zaidi ya asilimia 50, kwa kuwa ccm wameshindwa ndio uchaguzi urudiwe! Au hamjaridhika mpaka mwataka wazanzibari tuuwane ndio muone raha?
Nataka nimrudi bomani kwa baadhi ya vipengele alivyovitaja:
1) Anasema paundwe tume itakayoshirikisha hao watu aliowataja na iongozwe na jaji mkuu.
Raddi: Hata muunde tume ya malaika hakutakuwa na maana yoyote wakati mshindi anajuulikana na kwamba ameshinda kihaki. Bali ni khasara ya kupoteza pesa na wakati na kusababisha machafuko ambayo yanaweza kupoteza roho za wazanzibari.
Eti tume hio iongozwe na jaji mkuu! Kwani ukisikia jaji mkuu ndio hafanyi makosa na ni muadilifu? Kama huyo jaji hana kazi na anatafuta la kufanya na aende akaishughulikie kesi ya mashekhe wa uamsho na waislaamu wengi wa tanganyika wanateseka gerezani kwa dhulma, kama ni muadilifu kweli aende huko akafanye huo uadilifu.
2) Anasema maalim asiogope kurudia uchaguzi?
Raddi: Kwani maalim ndie mwenye haki ya kura za wazanzibari? Maalim hana kura ya veto, kura yake ni moja sawa na kura ya mzanzibari yoyote , hivyo hio ni haki ya wazanzibari na hatutaki zaidi ya kupewa haki yetu sio vyenginevyo.
3) Anasema wagombea urais wale kiapo cha kukubali matokeo.
Raddi: Kwani alieshindwa kutamka kukubali kushindwa ni nani? Si sheni! wacha kula kiapo, kwani hivyo viapo vya kujiapiza si munakula kila siku kulinda katiba na sheria! Mbona nyinyi mnaokula viapo hinyo si ndio wa mwanzo mnaovivunja? Sasa hicho kiapo ukisemacho wewe kina utofauti gani na hivyo mnavyo vila kila siku? Au hiki cha mara hii watakuja mitume kukisimamia?
4) Anasema eti anasikitishwa na baadhi ya wagombea kutoa rushwa!
Raddi: Wacha uongo wako nyinyi majaji ndio wala rushwa nambari moja leo wajitia kusikitishwa na hilo!
Nakhitimisha kwa kusema kama wewe umetumwa umuingize maalim katika mtego huo basi tambua umechelewa na jua kuwa wazanzibari si wajinga ni watu wenye akili kuwapita nyinyi waTanganyika na ndio maana mpaka leo mwateseka na zanzibar hamli vikawashuka wala hamlali mukapumzika mpaka pale mtakapoitema zanzibar.
Hapa hakuna atakaerudia uchaguzi, kama nyinyi ni wababe na madikteta twendeni hivi hivi na kama munaweza mtawazeni sheni kuwa ni mfalme wa zanzibar.
Eti jaji mkuu! Mtu mzima ovyooooo kama uchaguzi uliharibika zanzibar basi na tanganyika pia ume haribika maana kura za ushindi wa magufuli nyengine zimetokea zanzibar na kama kurejea uchaguzi basi urejewe wa tanzania nzima maana huko tanganyika zimekamatwa kura malori kwa malori na nyengine kuonekana misituni zimetupwa na wapo watu waliopigwa mpaka kuchiririka damu kwa kukamatwa na kura feki na hayo yote yalizagaa katika mitandao ya kijamii lakini hilo hamkuliona kuwa ni tatizo, na huku zanzibar hatukuona hizo dosari mlizosema bali ni porojo tupu.
 
Rafiki 19/12/2015 kwa 8:58 mu ? Jibu
Asalaam alaykum wandugu wote, inasikitisha kuona wasomi wa Tanganyika hasa mtu aliyekuwa jaji mkuu na wadhifa kubwa katika serikali lakin ni ----- na halina elimu yeyote, vipi jaji mkuu hajuwi shariya wala katiba wala hajjuwi nani mwenye haki na nani asiyo na haki, huyu mzee huu ujaji kaupatiya kwa njiya gani au kimabavu tu. nendeni shuleni mukasome tena ili muje kuzungumza yalo na maana. Wanatilisha aibu kwa watanzania kup
wapo viongozi na wakubwa wa nchi wasiojuwa hata kuzungumza na waandishi wa habari.
asanteni

Alkali1 19/12/2015 kwa 12:19 um ? Jibu
Hili ni kundi la CCM ambalo hatujaliona hata siku moja likitetea haki na kukenea uovu au dhulma. Wazee hawa hawajajifanya wazee wa nchi kutetea haki. Wao siku zote wako na msimamo wa CCM japokuwa kinavyofanya ni dhulma. Kwa hivyo hatushangai kusikia kauli kama hizi kutoka kwa mzee Bomani. Alikuwa wapi Jaji Bomani wakati CCM wanateremsha matusi katika Bunge la katiba huku wakishangilia na kukata viuno ? Alikuwa wapi Jaji Bomani wakati CCM wakiikejeli demokrasia kwa kusema kuwa hawatowi serikali kwa vikaratasi? CCM atatuambia vipi Wazanzibari tuingie uchaguzi mwengine wakati chama chake kinanadi katika majukwaa kuwa haipo tayari kutoa madaraka Zanzibar kwa vikaratasi? Hatujaona majaji wala viongozi wa CCM wakikemea kauli hizo. Jaji Bomani na wenzako kuweni wakweli kukubaliana wa haki na ukweli ili muiepushe nchi na majanga ya ulafi wa kisiasa. CCM imeshindwa uchaguzi wa 2015 na mwenye haki ni lazima apewe. Hapa hapataki falsafa wala makongamano ya kupoteza wakati, nguvu na mali za wananchi. Tutumieni wakati huo, nguvu na mali hizo katika kuwaletea maendeleo wananchi.

Mzambarauni Takao 19/12/2015 kwa 4:08 um ? Jibu
Huyu Mzee ananipa matatizo. Yaani kama yeye ana kiwango na umahiri wa mantiki asingetamka maneno hayo hapo chini kwani mimi mtu wa kawaida yananipa mchanganyiko na yanajizonga wenyewe kwa wenyewe.
Nanukuu maneno yake,
?Aliongeza kuwa Maalimu Seif asiendelee kujitangaza kuwa mshindi na wala asiogope uchaguzi kurudiwa kwani wananchi waliompigia kura hapo awali watarudia kufanya hivyo katika uchaguzi wa marudio na pengine kuongezeka?.
Maneno haya ukiyapekenyuwa utaona kuwa Mark Bomani anakiri ushindi wa Maallim Seif. Na nikiya-paraphrase manaeno hayo ni sawa sawa na kusema ,? Maallim usiogope kurudiwa kwa uchaguzi kwani utashinda tena tuu kama ulivyoshinda mwanzo, kwa kuwa wale wale wapiga kura waliokupa ushindi ndio wale wale ndio watakaokupa mara ya pili. Na safari hi kwa kuwa uchaguzi utasimamiwa na umoja wa madola basi utapeli wa CCM utadhibitiwa, na huenda ukapata kura zaidi ya awali?
Eee huu si ujuha kitu gani. Mark Bomani anmfanya Maallim mtoto endaye dede?. Yaani achukuwe kinyonyo akichovye asali kihsa amnyamazishe. These tactics are so humiliatingly cheap on the part Bomani that they border the fringes of idiocy.
Na haya masaala ya kuwaapisha wagombea kukubali kushindwa ni mtego ambao hata mtu awe na akili ya punda basi ataugunduwa.
Nanukuu
?Alisema kabla ya uchaguzi huo kurudiwa, wagombea wote pamoja na vyama vyao wale kiapo kwa kuahidi kukubali matokeo ya uchaguzi wa marudio?.
Hii ni kukusudia kumfunga na kumfumba mdomo Maalim asiwe na hoja hata wakichakachuwa kama wafanyavyo kawaida yao. Maallim usiyakubali haya abadan. Haya ni mazonge yamejaa ulimbo. Ukiingiya umekwisha.
Mark Bomani mzee tunakusihi weka rekodi nzuri ya memoirs yako. Mark Boman, as a lawyer with your mental capacity, it amazes me that you come up with this utumbo which is totally off the Mark. Zanzibar si rahisi kuifuta kama mnavofikiriya Watanganyika. Bora kapumzike take drift and get a life. Zanzibar ina wenyewe.
 
Hakuna pointi hapo bali naona mwandishi naye anatumia Zaidi jazba badala ya kujenga hoja. Ni kukurupuka kwingne huko.
 
Muda wa Rais wa sasa wa Zanzibar kukaa madarakani umeisha kisheria na kikatiba.

Hivi sasa anakula muda wa Rais ajaye, labda kuanzia mwaka huu tarehe za uchaguzi zibadilike zanzibar.

Maana mpaka sasa Rais ajaye amebaki na miaka 4 tu
 
Hivi kwani hao wazanzibari koloni letu?
Waachiwe tu wajiamulie wenyewe, si Zanzibar ni nchi?
Na ina katiba yake?
Wakielewana sawa, wakiumizana sawa, uchaguzi ni wao, si wetu.
 
Mungu aliweka mipaka ya kila nchi (kumbukumbu 32:8). Wazanzibari wapewe nchi yao
 
Hawa Kina Bomani washukuru mungu kuwepo kwao at the right time at the right place, hivyo wakapata favours zote walizopata. Ila ukisoma kilichoandikwa unagundua kuwa huyu ni mweupe kabisa. Ni kama vile anajaribu kujifanyia self promotion flani hivi.

Anasema njia pekee ni kurudia uchaguzi yeye kama nani?unaendaje kwenye negotiation table ukiwa na hardline approach kama hiyo?

Halafu huyu ndio alikuwa mwanasheria mkuu, ashukuru wakati huo vyombo vya habari vilikuwa havina uhuru,it's clear huyu alikuwa werema mwengine.

kwa uzee alionao, alitakiwa ajipumzikie aachie damu mbichi sio kuleta viherehere.., hawa ndio makongoro alisema wameingia kwenye chandimu wasikasirike kupigwa matobo.

Magufuli hebu mpe huyu hopeless mwengine hata kicheo cha mjumbe wa tume flani huko, benchi limekuwa kali sana.
 
Ni Shidaaa!! Hivi Huu Mfumo Wa Vyama Vingi Tumeingia Kwa Nia Ya KUPATA MISAADA Tu, Ili Tuonekane Kwa Wakoloni Wetu Tuna Demokrasia Ya Mfumo Wa Vyama VINGI!!!!?? Maana Ukitazama Kiuhalisia, Hakuna Demokrasia HALISI, Bali KIINI MACHO TU!!! Kama Vp Waufute Turejea Enzi Zile Za Kura Ya "NDIO Na HAPANA "Tu!! Picha Za Mgombea Ni Zile Jembe Na Nyundo!!!! USANII TUMECHOKA!!! Sasa Wazanzibar Ndio Wanafunguliwa Zaidi Hao, Coz 1964 Waliokuwa Na ELIMU Walikuwa Wachache, But 2015 Wako Wengi Zaidi Na Wanaisoma Na Kuitambua Katiba, History Na Sheria Zao Na Hata Huu Mkataba Wa Muungano!!! So Tusidhani Ni Wale Wale Tu Wa 1964!!! Kama Ilivyo Kwa Tanganyika Pia!! Hivyo Kwa Vile Muungano Ni Kitu Kizuri, Basi Tuuboreshe Kwa Kuweka MUUNDO Wa SERIKALI Zenye Uwazi Kwa MUUNDO, MAJUKUMU, WAJIBU Na MIPAKA Yake!! Na Hapa Tusimeze Na Kumung'unya Maneno MUUNDO Wa SERIKALI 3 Hauepukiki Kwa Hapa Tulipo Sasa!!! Kama Ilivyopendekezwa Ktk. RASIMU YA WARIOBA!! Otherwise Haya Ya MISUGUANO Na MALUMBANO Yataendelea Tu!! Na CCM KUENDELEA KUULINDA Muungano Huu Kwa NGUVU Ya Dora, Badala Ya KUJILINDA Wenyewe Kwa Kuridhiwa Na Pande ZOOTE Za NCHI Ambazo Zinaunda Muungano Huu!!!!
 
Hili nalo Tatizo! Uchaguzi wa Zanzibar uliharibika kwa sababu aliyeshinda siye aliyetakiwa kushinda! Katiba nayo inafuatwa na kutafasiriwa inavyopendeza wahitaji! Tunayaona pia yanayotokea kwenye chaguzi za mameya na wenyeviti wa serikali za mitaa...Angalabu Jaji angejijongeza kujadili ikiwa kweli Jecha kikatiba alikuwa nayo mamlaka ya kufuta uchaguzi mzima wa upande mmoja lakini kukubali matokeo ya upande mwingine aliyosimamia yeye na tume yake wakati huohuo!
 
Hivi kwani hao wazanzibari koloni letu?
Waachiwe tu wajiamulie wenyewe, si Zanzibar ni nchi?
Na ina katiba yake?
Wakielewana sawa, wakiumizana sawa, uchaguzi ni wao, si wetu.

Japokuwa bado ni mzima lakini ameshamezwa zaidi ya nusu. Ila miguu yake imeshafika mkiani! Kichwa hakimezeki na anapiga mateke! Chatu katulia tulii anajifanya mateke hayamuumizi! chatu mwenyewe anasema hajammeza, eti kamuhifadhi! Asijeakamezwa na chatu mwingine! Teh.....wazungu wa tanganyika bana..
 
Kama wee radi unakaa ukadhani siku moja au nyingine warioba, bomani na msekwa watizungumzia vibaya ccm basi utachelea sana, hata itokee ccm wanapita na kuua watu mamia mitaani wataamka na kusema ccm wana haki ya kujilinda na maadui zao,
Wanaishi na kura na kusaza wao na familia zao kwa ajiri ya mfumo wa nchii hii na wao ndio wanaofaidi na kama hujui wewe ambaye ni mpinzani wao kisiasa, tena upinzani ulioruhusiwa kikatiba, unaonekana adui na mhaini na unastahili hata mauti kwani wao kutofautiana nao kisera ni kama kukufuru, na huyo bomani alikuwa kimya kipindi chote cha uchaguzi, alikuwa anapima upepo na alikuwa akiogopa. Na pia hakufahamu aende upende gani kwani mvutano wa kisiasa ulikuwa mbaya kwake, sasa uchagguzi umeisha, anajipambanua na kujitokeza hadharani ili nae aonekane yupo ili apate hata nafasi ya kwenda kunywa chai ukulu ili akalete umbea jambo ambalo namsikitikia sana kwa utawala na utendaji wa magufuli hawatapata nafasi kwani huyu jamaa anawajua vizuri sana watu kama bomani, walipotokea na wanapoelekea, na inampasa atulie TRA waende kupitia vitabu vya hesabu vya serengeti bruwelizi, kwani kuna tetesi kwamba hakuna fair ground za kibiashara na makampuni mengine ya bia kwani kuna mengine hayaripi kodi kwa miaka mingi kwani wanaweza kuuza bia hata shilingi mia tano na bado wakapata faida, bado tuhuma nyingi ne za dhuruma,
Huko kote magufuli atafika na ukweli utajulikana, acha wengine waseme ila kwa wewe mhe jaji bomani hapana ni bora ukae kimya. Maana utapata aibu tuu, mambo ya wazanzibar waachie wenyewe huna lolote unalolijua kuhusu zanzibar,tafuta njia nyingine za kujikomba.
 
Hili nalo Tatizo! Uchaguzi wa Zanzibar uliharibika kwa sababu aliyeshindabsiye aliyetakiwa kushinda! Katiba nayo inafuatwa na kutafasiriwa inavyopendeza wahitaji! Tunayaona pia yanayoyokea kwenye chaguzi za mameya na wenyeviti wa serikali za mitaa...Angalabu Jaji angejijongeza kujadili ikiwa kweli Jecha kikatiba alikuwa nayo mamalaka ya kufuta uchaguzi mzima wa upande mmoja lakini kukubali matokeo ya upande mwingine aliyosimamia yeye na tume yake wakati huohuo!

Bomani kinachomsumbua ni UCCM. Kajikuta anashindwa kuwa mkweli mpaka hata usomi na madaraka aliyowahi kushika vinatiliwa mashaka. Ni aibu kubwa katika taaluma na umri wake
 
Duuuh huyu bomani hora angekaa kimya tu kuliko kujidhalilisha huku
 
Na hili la Maalim Sefu kujipa nafasi ya ZEC na kujitangaza mshindi nalo mnalisemeaje. na ile idadi ya wapiga kura iliyozidi kule Pemba watu wakae kimya, hizo siyo dosari zisisemwe? unafki huo. uchaguzi urudiwe tu. CUF wajiamini. kama ushindi ni wao wataupata tu.
 
Na hili la Maalim Sefu kujipa nafasi ya ZEC na kujitangaza mshindi nalo mnalisemeaje. na ile idadi ya wapiga kura iliyozidi kule Pemba watu wakae kimya, hizo siyo dosari zisisemwe? unafki huo. uchaguzi urudiwe tu. CUF wajiamini. kama ushindi ni wao wataupata tu.

Unaweza kututajia jimbo ambalo limezidi idadi ya wapiga kura kule pemba,zec wenyewe ndio wamemtangaza maalim kwa kubandika matokeo ya kura vituoni,na je kama idadi imezidi vp kuhusu uchaguz wa magufuli nao pia urejewe?
 
Bomani kinachomsumbua ni UCCM. Kajikuta anashindwa kuwa mkweli mpaka hata usomi na madaraka aliyowahi kushika vinatiliwa mashaka. Ni aibu kubwa katika taaluma na umri wake
Kwa mwenendo huu tutaendelea kushuhudia mambo yasiyoeleweka na kujenga taifa lililogawanyika.
 
Na hili la Maalim Sefu kujipa nafasi ya ZEC na kujitangaza mshindi nalo mnalisemeaje. na ile idadi ya wapiga kura iliyozidi kule Pemba watu wakae kimya, hizo siyo dosari zisisemwe? unafki huo. uchaguzi urudiwe tu. CUF wajiamini. kama ushindi ni wao wataupata tu.
CCM mna unafiki wa hali ya juu.
Uchaguzi ulishafanyika na ulikwisha.
Matokeo yote yalishatangazwa majimboni. Matokeo ya wawakilishi yaliishia kwa walioshinda uwakilishi kupewa vyeti wa ushindi. Matokeo ya kura za uraisi pia yalibandikwa majimboni. Ni matokeo hayo yanayompa mgombea wa CUF ushindi na ni matokeo hayo yanayoonesha mgombea wa nafasi ya uraisi kupitia CCM ameangukia pua.

CCM imeamua kubaka demokrasia na kumwamuru Mwenyekiti wa Tume "huru", ZEC afute uchaguzi na matokeo yake bila ya kuwepo na malalamiko yaliyowasilishwa na mawakala wa vyama.

Kurudia uchaguzi ni uhuni wa CCM wa kutaka kufunga goli la Nape. Kama CCM ilishinda uchaguzi ule Jecha angekuwa na ubavu wa kufuta uchaguzi au matokeo?

CCM mnaiharibu nchi hii, CCM mnaichezea amani ya nchi. CCM iheshimu maamuzi ya wapiga kura.

Siri iko nje, tokea 1995 CCM haijawahi kushinda uchaguzi mkuu huko Zanzibar lakini Mwanyekiti wa ZEC amekuwa akilazimishwa kumtangaza mgombea wa CCM ameshinda.

Mimi nashangaa kwa nini Msajili wa vyama hajakifuta CCM kwa uhuni huu wanaoufanya kwa miongo miwili sasa. Hapo ndio utafahamu maana ya Chama dola.

Imeripotiwa Makamo Mwenyekiti alitekwa nyara na vyombo vya dola ili asiendelee kutangaza matokeo ya uchaguzi. Kwa nini alichukuliwa na vyombo vya dola? Nani aliamrisha uhuni huo? Huyo aliyeamrisha ndie alivuruga uchaguzi.

Ni wazi hilo lilifanyika ili kuminya na kuzuia haki isitendeke na ni ubakaji wa demokrasia.

Kwa vyovyote wote, waliohakikisha wanazuia matokeo yasiendelee kutangazwa wamefanya hivyo kwa malengo ya kukibeba CCM na hiyo ndio "siri" ya ukasuku wa "uchaguzi urudiwe".

CCM na wanachama wa CCM wamejigeuza makasuku na kauli mbiu ni "uchuguzi urudiwe".

Kwa nini CCM haitaki yale matokeo yaliyotangazwa na yaliyobandikwa vituoni, majimboni baada ya kuhesabiwa kura yasitangazwe na mwenyekiti wa ZEC?

CCM inabaka demokrasia na kutishia amani ya nchi yetu.

Huu ni mtihani kwa Magufuli . Magufuli atabakia kuwa msema kweli na kuukana unafiki wa CCM? Nimkumbushe tu , Raisi Pombe wa Magufuli alisema "mimi nauchukia unafiki, mimi ni msema kweli na msema kweli ni mpenzi wa Mungu"

Raisi Magufuli ajiulize;je aliye mnafiki na anayepindisha ukweli na anayebariki au kufumbia macho dhuluma kutendeka ni mpenzi wa nani?
 
Bomani kakubali kutumika kwa maslai ya ccm.siku zote hizo 73 alikuwa wapi???.
 
Back
Top Bottom