Jaja apiga shuti moja tu dakika 82

Jaja apiga shuti moja tu dakika 82

Lupweko

JF-Expert Member
Joined
Mar 26, 2009
Posts
24,940
Reaction score
26,796
Mshambuliaji ghali wa Yanga, Mbrazili, Geilson Santos ‘Jaja’, juzi Jumamosi alicheza mchezo wake wa nne wa Ligi Kuu Bara alipokutana na Simba kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar, lakini alishindwa kuisaidia timu yake baada ya kupiga shuti moja tu langoni.

Jaja aliyesajiliwa na Yanga akitokea nchini Brazil ambapo analipwa mshahara wa dola 3,000 kwa mwezi (zaidi ya shilingi milioni nne za Kitanzania), alipiga shuti hilo dakika ya 73 akiunganisha pasi aliyopewa na beki wa kushoto wa timu hiyo, Oscar Joshua.


Straika huyo mwenye mwili uliojengeka kimazoezi, alicheza mchezo huo kwa dakika 82 na kulazimika kwenda benchi kumpisha Mganda, Hamisi Kiiza ‘Diego’ ambapo mpaka anatoka alifanikiwa kupiga mipira sita ya vichwa huku vichwa viwili vikiwa fyongo.

cc: mkolaj, Makoye Matale, Ududu, bujashi25, Balantanda
 
Nimeanza kukosa imani na hawa wazungu. Maksimo wape nafasi kiiza na javu tuone wataisaidiaje timu!
 
Kwa hesabu kama hizo, pointi moja ya Simba ilipatikana kwa maandalizi ya shilingi ngapi dhidi ya maandalizi ya Yanga kwa pointi hiyohiyo; ubao aliyoukalia Kwizera ulinunuliwa kwa kiasi gani cha usajili wake ukilinganisha na wa Said Ndemla; fedha anazolipwa Maximo zimeshanunua pointi ngapi dhidi ya anazolipwa Mexime? Mpira, kama ilivyo dunia, ni duara. Hauna mbele wala nyuma, juu wala chini. Kutaka kila kitu chake kitabirike kama hali ya hewa ni kutoelewa maana nzima ya mchezo wenyewe, uchezaji, wachezaji na wadau wake wengine.
 
Wauza matikiti maji na mpira wapi na wapi? Huyo nyonyo alibahatisha tu siku alipotupia mbili ngao ya jamii.
 
Mchezaji anatoka nchi kubwa anatakiwa aje na acheze sio tumpe muda, labda wakina Ngonyani!
Dirisha dogo linamuhusu JAJA.
 
Jaja anajua kuji-position sema hakupewa mipira mingi kwa jinsi fomesheni ilivyoonekana inatakiwa iwe, niliangalia ile krosi moja aliyotokea na kupiga kichwa kilichotoka sentimita chache nikamuona ni hatari AKIWEZESHWA
 
Umbea tu ww umepiga mangapi
Mimi sikupangwa kwenye kikosi. Sasa wachambuzi wa soka wanaposema kiungo fulani amezunguka kilometa kadhaa ndani ya dakika tisini, nao ni umbea? Hakuna umbea hapo, soka ni mchezo unaochezwa hadharani, kila mtu anayeweza kushuhudia atashuhudia tu!
 
infwacti ukimpanga jaja mjiandae kucheza pungufu sababu hadi umlishe ndiyo atacheza tena usimpe mkononi hadi mdomoni
 
Cha kuangalia ni nafasi ngapi zilitengenezwa. Inajulikana Jaja ni mmaliziaji mzuri, je wale wa kumtengenezea walitengeneza nafasi ngapi? na huyo kiiza baada ya kuingia, alizitengeneza hizo nafasi mwenyewe?
BTW mi ni mnyama.
 
Cha kuangalia ni nafasi ngapi zilitengenezwa. Inajulikana Jaja ni mmaliziaji mzuri, je wale wa kumtengenezea walitengeneza nafasi ngapi? na huyo kiiza baada ya kuingia, alizitengeneza hizo nafasi mwenyewe?
BTW mi ni mnyama.
Salute kwako mkuu kwa kuongea kimpira inaonekana wewe ni mfuatiliaji wa soka sio Jabulani yeye atakuwa mfuatiaji wa netball...
 
Wengne wengi awapendi ukweli
Lakini ukweli wa huyu mchezaji Jaja ni huo

Hii ni mimba ambayo kama anasubiri itamzalsha mtoto mwenye
Ebola...ni bora kabla ukaamua kuichechetua kabisa kabisa


Cheki naame maria stopes ma dk wengi wakuondoa mimba kama hizi🙂 🙂 🙂
 
Tumpe muda,,,, mimi naona tatizo ni viungo, badala ya kupanga mashambulizi wao wanaokoa tu.
 
kweli ninakubali tanzania hawajui mpira kazi yao midomo tena midomo inayonuka
 
hivi okwi alifunga kama alivyoahidi kuwa tar 18 yanga watalia eeh!!!
 
Mshambuliaji ghali wa Yanga, Mbrazili, Geilson Santos ‘Jaja’, juzi Jumamosi alicheza mchezo wake wa nne wa Ligi Kuu Bara alipokutana na Simba kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar, lakini alishindwa kuisaidia timu yake baada ya kupiga shuti moja tu langoni.

Jaja aliyesajiliwa na Yanga akitokea nchini Brazil ambapo analipwa mshahara wa dola 3,000 kwa mwezi (zaidi ya shilingi milioni nne za Kitanzania), alipiga shuti hilo dakika ya 73 akiunganisha pasi aliyopewa na beki wa kushoto wa timu hiyo, Oscar Joshua.


Straika huyo mwenye mwili uliojengeka kimazoezi, alicheza mchezo huo kwa dakika 82 na kulazimika kwenda benchi kumpisha Mganda, Hamisi Kiiza ‘Diego’ ambapo mpaka anatoka alifanikiwa kupiga mipira sita ya vichwa huku vichwa viwili vikiwa fyongo.

cc: mkolaj, Makoye Matale, Ududu, bujashi25, Balantanda

hatutaki ushauri wako kashauri timu nyingine zipo nyingi Yanga iacheni kama ilivyo mpira hujui unajifanya unacoment
 
Cha kuangalia ni nafasi ngapi zilitengenezwa. Inajulikana Jaja ni mmaliziaji mzuri, je wale wa kumtengenezea walitengeneza nafasi ngapi? na huyo kiiza baada ya kuingia, alizitengeneza hizo nafasi mwenyewe?
BTW mi ni mnyama.

Inakatisha tamaa wewe kama kiungo kuona Jaja akiwa mbele yako,unaweza hata usimpe mpira mana unajua ataharibu tu.
 
Tukubali au tukatae Kiiza ni bora kuliko Jaja na Msuva ni bora kuliko Countinho katika nafasi anayopangagwa.
 
Back
Top Bottom