Jafo awazuia Raia wa kigeni kufanya baadhi ya Biashara Nchini

Jafo awazuia Raia wa kigeni kufanya baadhi ya Biashara Nchini

Abdul Said Naumanga

JF-Expert Member
Joined
Jan 28, 2024
Posts
745
Reaction score
1,470
Kumekua na malalamiko na mijadala juu ya uwepo wa utitiri wa raia wa kigeni, hususan Wachina, katika baadhi ya biashara, especially zile ndogondogo hadi zile za kati hasa katika maeneo ya Dar Es Salaam, na hata masokoni ya mikoani. Wengi wamehoji namna wageni hawa wanavyoingia sokoni kwa nguvu ya mitaji mikubwa, miundombinu ya kisasa na mtandao wa kiusafirishaji kutoka China, huku wakishindana moja kwa moja na wafanyabiashara wazawa katika sekta ambazo hazihitaji teknolojia ya hali ya juu, kama uuzaji wa bidhaa rejareja, vipuri, saluni, usafi na ujasiriamali wa kawaida. Sauti za malalamiko haya zimekuwa zikipazwa si tu na wafanyabiashara, bali hata viongozi wa jumuiya za biashara, na hatimaye serikali imeamua kuchukua hatua.

Mnamo tarehe 25 Julai 2025, Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk. Selemani Jafo, alitoa amri ya kuzuia raia wa kigeni kujihusisha na baadhi ya biashara “The Business Licensing (Prohibition of Business Activities for Non-Citizens) Order, 2025”

Katika amri hiyo, biashara 15 zimepigwa marufuku kufanywa na raia wa kigeni. Biashara hizo ni pamoja na:​
  1. kuuza bidhaa rejareja (isipokuwa supermarket),​
  2. uhamishaji wa pesa kwa simu,​
  3. urekebishaji wa simu na vifaa vya kielektroniki,​
  4. saluni (isipokuwa ndani ya hoteli au kwa utalii),​
  5. usafi wa mazingira,​
  6. ununuzi wa mazao mashambani,​
  7. biashara ya vibeti na maduka ya vitu vya kale,​
  8. biashara za uwakala na udalali,​
  9. uchimbaji mdogo wa madini​
  10. na nyingine nyingi zinazogusa ujasiriamali wa kawaida wa Mtanzania.​
IMG_5538.jpeg
Amri hii imepokelewa kama hatua ya kulinda uchumi wa ndani, ajira na mazingira ya ushindani wa haki. Lakini pia amri hii pia imetengeneza makosa ya jinai na adhabu zake kupitia kifungu cha 3(3). amri hiyo inasema kuwa raia wa kigeni akikiuka marufuku atatozwa faini isiyopungua shilingi milioni 10 au kifungo cha hadi miezi sita, huku Mtanzania anayemsaidia akifungwa hadi miezi mitatu au kulipa faini ya milioni tano.
IMG_5539.jpeg
 
Ni hatua muhimu kulinda ajira za wazawa. Wakiachwa free hawa wageni kuna siku atakuja mchina mmoja kufundsha somo langu la mwandiko
 
Yupo sahihi hata sisi hatuwezi kufanya shughuli yeyote kwenye Nchi za watu unafanya shughuli kwa vibali ulivyopewa tu na unasumbuka kweli kuvipata sio kirahisi rahisi tu kama ilivyokua hapa kwetu..
 
Kumekua na malalamiko na mijadala juu ya uwepo wa utitiri wa raia wa kigeni, hususan Wachina, katika baadhi ya biashara, especially zile ndogondogo hadi zile za kati hasa katika maeneo ya Dar Es Salaam, na hata masokoni ya mikoani. Wengi wamehoji namna wageni hawa wanavyoingia sokoni kwa nguvu ya mitaji mikubwa, miundombinu ya kisasa na mtandao wa kiusafirishaji kutoka China, huku wakishindana moja kwa moja na wafanyabiashara wazawa katika sekta ambazo hazihitaji teknolojia ya hali ya juu, kama uuzaji wa bidhaa rejareja, vipuri, saluni, usafi na ujasiriamali wa kawaida. Sauti za malalamiko haya zimekuwa zikipazwa si tu na wafanyabiashara, bali hata viongozi wa jumuiya za biashara, na hatimaye serikali imeamua kuchukua hatua.

Mnamo tarehe 25 Julai 2025, Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk. Selemani Jafo, alitoa amri ya kuzuia raia wa kigeni kujihusisha na baadhi ya biashara “The Business Licensing (Prohibition of Business Activities for Non-Citizens) Order, 2025”

Katika amri hiyo, biashara 15 zimepigwa marufuku kufanywa na raia wa kigeni. Biashara hizo ni pamoja na:​
  1. kuuza bidhaa rejareja (isipokuwa supermarket),​
  2. uhamishaji wa pesa kwa simu,​
  3. urekebishaji wa simu na vifaa vya kielektroniki,​
  4. saluni (isipokuwa ndani ya hoteli au kwa utalii),​
  5. usafi wa mazingira,​
  6. ununuzi wa mazao mashambani,​
  7. biashara ya vibeti na maduka ya vitu vya kale,​
  8. biashara za uwakala na udalali,​
  9. uchimbaji mdogo wa madini​
  10. na nyingine nyingi zinazogusa ujasiriamali wa kawaida wa Mtanzania.​
Amri hii imepokelewa kama hatua ya kulinda uchumi wa ndani, ajira na mazingira ya ushindani wa haki. Lakini pia amri hii pia imetengeneza makosa ya jinai na adhabu zake kupitia kifungu cha 3(3). amri hiyo inasema kuwa raia wa kigeni akikiuka marufuku atatozwa faini isiyopungua shilingi milioni 10 au kifungo cha hadi miezi sita, huku Mtanzania anayemsaidia akifungwa hadi miezi mitatu au kulipa faini ya milioni tano.
Shida yetu sisi ni utekelezaji wa sheria.sheria zipo nzuri sana lakini hakuna usimamazi.mchina anaweka machine za kubet na kukusanya pesa wabongo tunashangilia na kuwaona wachina wajanja sana.wabongo tuna shida sana.
 
Shida yetu sisi ni utekelezaji wa sheria.sheria zipo nzuri sana lakini hakuna usimamazi.mchina anaweka machine za kubet na kukusanya pesa wabongo tunashangilia na kuwaona wachina wajanja sana.wabongo tuna shida sana.
Na hilo ndo tatizo kuu
 
Back
Top Bottom