Nemesis
JF-Expert Member
- Feb 13, 2008
- 5,462
- 4,364
Hakuna anayejua kwa undani yanayoendelea katika misikiti na makanisa yanayotishia amani na utulivu wa nchi. Ni dhahiri vyombo vya dola vimeshindwa na haviwezi tena kurudisha hali kutokana na kampeni zinazoendelea.
Nimefuatilia matamko mbalimbali ya Waislam (BAKWATA), UAMSHO na wanaharakati wa dini hiyo toka uchaguzi wa 2010. Pia Tumeyaona yaliyofanyika Zanzibar, Mtwara, Mbagala (Temeke) na Kigoma pia. Pia mihadhara inaendelea maeneo mengi ya nchi hasa katika juma hili. Ukisikia yanayoongelewa yanatisha.
Kwa upande mwingine, kuna msululu wa jumbe za simu (sms) zinazunguka miongoni mwa Wakristo kila siku zikihamasisha maombi na zingine zinapindukia hata kutaka vita (mapambano ya mwili) dhidi ya Waislam. Kwa ujumla hali ni mbaya na inazidi kuwa mbaya kila siku.
Haya ndiyo yanayosikika, bila shaka yapo mengi na pengine kunamipango ya hatari sana inayoendelea katika misikitio na makanisa au waumini wa dini hizo mbili ambayo yanahitaji kuwa wazi na kuwekewa mikakati ya kuinusuru nchi.
Miaka ya 2000 nchi ya Rwada ilijenga shaka juu ya yanayoendelea mashule. Bunge la nchi hiyo liliunda kamati ya bunge na kufanya uchunguzi. Yaliyobainika yalikuwa makubwa na kulikuwa na uwezekano wa kurudi kwenye vita vya kikabila baada ya muda fulani (wanafunzi watakapokuwa wakubwa). Kamati hiyo ilitoa mapendekezo ambayo yalilazimisha kufanyika kwa mageuzi makubwa katika sekta ya elimu na kutokomeza kabisa elimu ya chuki na ubaguzi wa kihutu na kitusi.
Ni rai yangu, kuundwa kamati ya bunge, yamkini tutaondoa chuki, udini na hasira za kidini zinazopandikizwa kwa kasi ya ajabu.
Nimefuatilia matamko mbalimbali ya Waislam (BAKWATA), UAMSHO na wanaharakati wa dini hiyo toka uchaguzi wa 2010. Pia Tumeyaona yaliyofanyika Zanzibar, Mtwara, Mbagala (Temeke) na Kigoma pia. Pia mihadhara inaendelea maeneo mengi ya nchi hasa katika juma hili. Ukisikia yanayoongelewa yanatisha.
Kwa upande mwingine, kuna msululu wa jumbe za simu (sms) zinazunguka miongoni mwa Wakristo kila siku zikihamasisha maombi na zingine zinapindukia hata kutaka vita (mapambano ya mwili) dhidi ya Waislam. Kwa ujumla hali ni mbaya na inazidi kuwa mbaya kila siku.
Haya ndiyo yanayosikika, bila shaka yapo mengi na pengine kunamipango ya hatari sana inayoendelea katika misikitio na makanisa au waumini wa dini hizo mbili ambayo yanahitaji kuwa wazi na kuwekewa mikakati ya kuinusuru nchi.
Miaka ya 2000 nchi ya Rwada ilijenga shaka juu ya yanayoendelea mashule. Bunge la nchi hiyo liliunda kamati ya bunge na kufanya uchunguzi. Yaliyobainika yalikuwa makubwa na kulikuwa na uwezekano wa kurudi kwenye vita vya kikabila baada ya muda fulani (wanafunzi watakapokuwa wakubwa). Kamati hiyo ilitoa mapendekezo ambayo yalilazimisha kufanyika kwa mageuzi makubwa katika sekta ya elimu na kutokomeza kabisa elimu ya chuki na ubaguzi wa kihutu na kitusi.
Ni rai yangu, kuundwa kamati ya bunge, yamkini tutaondoa chuki, udini na hasira za kidini zinazopandikizwa kwa kasi ya ajabu.