Nadhani ITV hapa hawahusika ila "bao la mkono ndio linahusika.
Huu unaweza kuwa ushahidi mwingine wa rafu zinazochezwa.
Acheni Kuchafua vituo vya watu hiyo picha imetoka kwenye screen ya tume ITV walicho fanya ni kuivuta tuu...huu sasa ni ujinga na utoto...uliopitiliza..!Kwanza hueleweki..
Hii television ifungiwe, television imejaa ukanda na ukabila, television inapika propaganda kuwatetea mafisadi, hii television ifungiwe tu ile iwe fundisho kwa wengine!
ficha upumbavu wako. matokeo ya uraisi yanatangazwa na tume tu na si vinginevyo
Great thinker hapa!
Binafsi nimepata screen shot nyingi kwa whatsupp ambazo hazitally sijui watu wanazipata wapi au wanatengeza kwa computer ILA...
Kwa utafiti mdogo na baada ya kufuatilia nika gundua kuna wanatoa taarifa za matokeo kule wilayani/mikoani wakati bado hazija hakikiwa na tume kama sheria inavyo elekeza.
Naamini wote tuna fahamu kuwa matokeo yanayo takiwa YATAMBULIKE kisheria ni yale tu yaliyo tangazwa na Tume ya Uhaguzi. Hayo mengine ni FAKE kisheria na wanao ya post kwenye social media wasitumie uhuru wao vibaya wa kupotosha ukweli...
Kwa akili ya kawaida tu, tume ya uchaguzi inajumuisha watu wanaojua Hesabu na Statistics vizuri, hawawezi kupitisha data FEKI kama hizo ambazo hata mwanafunzi wa darasa la tano anaona kuna makosa!!!
Tatizo ni kuwa watu wetu wengi ni copy paste...hawatumii akili zao kufikiri..kila wakiona wanafikiri ni kweli!
Unajua Tume ina-understimate nguvu ya social media, dunia ipo connected sana sasa hivi ukilinganisha na miaka mitano nyuma. Sasa hivi almost kila mtu yupo hewani, ilibidi waangalie njia nyingine za kutangaza matokeo.
Sioni sababu ya kuzuia matokeo ya urais kutangazwa moja kwa moja kutoka vituoni, vituo vyote vina representatives toka vyama vyote kwa hiyo wote waki-sign hata matokeo yakitangazwa hakuna shida. Kusema kura zipelekwe dar waanze ukaguzi ndo kitu kinaleta complications. Wao wangekua wanachukua namba direct kutoka vituoni wana-update direct kwenda kwenye database alafu wana-release kwenye press data in real time.
Ndio system nchi zote zilizoendelea wanatumia, sijui watu weusi tuna matatizo gani huku africa.
Wanajamvi Tuchangie hoja zenye mantiki na kuelimishana kwa faida endelevu ya jamvi letu. hebu tujumuishe hizo asilimia..... ni zaidi ya 100. Je huko ITV wanashindwa kufanya hesabu ya darasa la pili? Tutetee hoja zenye mashiko na si ujinga.
Ni kweli kabisa jana wamezua kizaa zaa huku mtaani kwa takwimu zao za uongo na upotoshaji mkubwa...nmewapigia sim hawajapokea nikaamua kuwatumia sms waache huu upotoshaji wa makusudi lakin hadi hiv sasa cjapata majibu yao..hili jambo halikubaliki hata kidogoo kwa chombo cha habari kama itv kuupotosha umma kwa maslai yao binafsi