ITV inapojiunga na wale wanaoikebehi zanzibar

ITV inapojiunga na wale wanaoikebehi zanzibar

haya ndiyo matatizo ya uhuru wa kutoa maoni kila mmoja anaelewa atakavyo,nini maana ya kukebehi ? kama maudhui ya kilichoonyeshwa kinamuudhi mtu hiyo si tatizo la ITV ni tatizo la anaudhika,tufikie pahara tukubali kutokubaliana kwa amani, huyu anayedhani ITV wameonyesha kipindi kisichofaa yeye ndiye mwenye matatizo na anakebehi vipindi vya ITV. ndani ya ITV kuna vipindi vingi sana na vingine "vinakebehi" misimamo na matakwa ya mtu mmoja mmoja au kundi fulani na kufurahisha au kuelimisha kundi jingine. Ni vema tuwe na utamaduni wa kutafakari na kukubali changamoto ambazo wengine huziona ni kebehi... UHURU WA KUTOA MAONI si lazima maoni yawe ni ya kufurahisha jamii nzima, kwa mtazamo wangu maoni yako kuhusu ITV na Zanzibar ni kuwadhalilisha wazanzibar kanakwamba uwezo wao wa kufikiri ni pungufu
 
ITV ndo tv bora kuliko zote tz. mimi nikifungua tbc one huwa nafunga au kubadilisha chanel harakaharaka kwasababu huwa naona wananiudhi. wako biased na wanatengeneza mno taarifa.

kuhusu zenji, wazenji hamna jipya. kwanza kabisa, mimi nashangaa tu, ni kwanini wabara hatung'atuki kuwaacha mkajiunge na visiwa vya shelisheli au komoro. nyie ni mzigo mzito usobebeka. sijui kwasababu wengi wenu ni...ops sory, waswahili mno? au wavuvi mno?hahah.
 
mie sioni logic ya kukimbia ukweli

kuna matatizo ktk muungano na zanzibar ikiksema baada ya kuchukuliwa kwa upendo wa kudumisha muungano watu huona wanahitaji zaidi

ni kukaa na kuzungumza
 
muungano ni kwa manufaa ya nchi mbili kiusalama, kiuchumi, kisiasa na kijamii

muungano sio tatizo ikiwa watu watakuwa tayari kuzungumza na kuyatafutia suluhisho yale wanayotofautiana watu.

hata ndoa zilizodumu zilipita ktk kipindi cha majaribu, lkn nia njema za wanandoa zilisaidia kufanya wafike mbali. sasa tuwe majasiri wa kuzungumza na kutafuta ufumbuzi wa matatizo yetu
 
Sikubahatika kuangalia hicho kibonzo lakini naamioni kazi ya vibonzo ni kuelimisha na kukosoa. Hata Bush alikuwa anachorwa sana lakini hakuwahi kulalamika kwa hiyo sioni sababu ya kulumu ITV.
 
haya ndiyo matatizo ya uhuru wa kutoa maoni kila mmoja anaelewa atakavyo,nini maana ya kukebehi ? kama maudhui ya kilichoonyeshwa kinamuudhi mtu hiyo si tatizo la ITV ni tatizo la anaudhika,tufikie pahara tukubali kutokubaliana kwa amani, huyu anayedhani ITV wameonyesha kipindi kisichofaa yeye ndiye mwenye matatizo na anakebehi vipindi vya ITV. ndani ya ITV kuna vipindi vingi sana na vingine "vinakebehi" misimamo na matakwa ya mtu mmoja mmoja au kundi fulani na kufurahisha au kuelimisha kundi jingine. Ni vema tuwe na utamaduni wa kutafakari na kukubali changamoto ambazo wengine huziona ni kebehi... UHURU WA KUTOA MAONI si lazima maoni yawe ni ya kufurahisha jamii nzima, kwa mtazamo wangu maoni yako kuhusu ITV na Zanzibar ni kuwadhalilisha wazanzibar kanakwamba uwezo wao wa kufikiri ni pungufu

Kama unavyosema kuwa tuko katika dunia ya uhuru na kwa mantiki hiyo yeyote asiependa au kuudhiwa na jambo huwa na uhuru wa kusema. Wajibu wa mwengine ni kumpa hoja kumuonyesha vyenginevyo na sio kumuona kuwa ana kasoro. Kwa maana hiyo nafikiri kasoro ipo upande wako unaekurupuka na kumjudge mtu bila kwanza kuuliza kulikoni? Nina wasiwasi pengine hujui hata jambo lenyewe ninalolilalamikia lakini maadam lina sura ya kimuungano muungano na kwa vile unao mtizamo wako tayari kwa hilo unakurupuka tu
 
ITV ndo tv bora kuliko zote tz. mimi nikifungua tbc one huwa nafunga au kubadilisha chanel harakaharaka kwasababu huwa naona wananiudhi. wako biased na wanatengeneza mno taarifa.

kuhusu zenji, wazenji hamna jipya. kwanza kabisa, mimi nashangaa tu, ni kwanini wabara hatung'atuki kuwaacha mkajiunge na visiwa vya shelisheli au komoro. nyie ni mzigo mzito usobebeka. sijui kwasababu wengi wenu ni...ops sory, waswahili mno? au wavuvi mno?hahah.

Nje ya mada Bro.
 

Tafadhali fuatilia Kibonzo ninachozungumza pengine utaelewa kwanini nilikuwa na reaction unayoiona kwa huo wewe unaouona ni utani na Wazanzibari wanashindwa kuuchukulia kama utani.
 
Sikubahatika kuangalia hicho kibonzo lakini naamioni kazi ya vibonzo ni kuelimisha na kukosoa. Hata Bush alikuwa anachorwa sana lakini hakuwahi kulalamika kwa hiyo sioni sababu ya kulumu ITV.

Angalau wewe umekuwa muwazi na kutaka ufafanuzi wa ninachokizungumza.
Kwanza mchoro wenyew haukuwa sahihi na hili linathibitishwa na Waziri Mkuu Pinda. Mchoro ulikwa wa sanamu la watu wawili waioungana kila kitu isipokuwa Kichwa. Kichwa kimoja kilibeba jina la zenji na chengine Bara. Jee huu si ukweli tunaoukana sote?
KEBEHI iliomo ni kuwa kichwa cha Zenji kinasema "hii miguu ni yangu"
Nawaachieeni wenye hoja zaidi kutafakari.
 
Back
Top Bottom