Itawezekana Rais kukatwa kodi ya kiinua mgongo bila kubadili kifungu cha 43(2) cha Katiba?

Salary Slip

Platinum Member
Apr 3, 2012
49,325
152,136
Kifungu hiki kinataamka: "Mshahara na malipo mengine yote ya Raisi havitapunguzwa wakati Raisi anapokuwa bado ameshika madaraka yake kwa mujibu wa Katiba hii."

Hicho ni kifungu cha Katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 kinachoongelea Mashariti ya Kazi ya Raisi.

Kwa ufahamu wangu, Raisi anahesabika kuwa bado yupo madarakani mpaka pale mrithi wake (Raisi Mteule) atakapokuwa amekula kiapo cha kushika madaraka ya uraisi.

Hofu yangu hapa ni kuwa baada ya kuambiwa sasa Raisi atalipa kodi,jambo hili linaweza likasahaulika na mwisho wa siku tukaambiwa ilishindikana kukata kodi kiinua mgongo cha Raisi kwasababu katiba haikubadilishwa na wakati huo hata Bunge linaweza kuwa limeshavunjwa.

Kingine cha msingi hapa ni je sheria imetoa timeframe kwamba Raisi awe amelipwa kiinua mgongo chake wakati gani au iko kimya juu ya hili?

Nauliza hivi kwasababu Raisi ana privilege nyingi kiasi kwamba hata kiinua mgongo chake huenda hulipwa mapema kabisa kabla hata hajastaafu hivyo kunaweza kutokea contradiction kati ya sheria na katiba baada ya mabadiliko haya yanayoruhusu Raisi nae sasa kukatwa kodi ya kiinua mgongo.

Je,hili haliwezekani kutokea?

Kwanini uamuzi huu wa Bunge wa kukata kodi kiinua mgongo cha Raisi usiende sambamba na kubadili moja kwa moja kifungu hiki cha Katiba kwa kuongeza sharti jipa katika katiba hii juu ya Raisi sasa kukatwa hii kodi?
 
Kifungu hiki kinataamka: "Mshahara na malipo mengine yote ya Raisi havitapunguzwa wakati Raisi anapokuwa bado ameshika madaraka yake kwa mujibu wa Katiba hii."

Hicho ni kifungu cha Katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 kinachoongelea Mashariti ya Kazi ya Raisi.

Hofu yangu ni kuwa baada ya kuambiwa sasa Raisi atalipa kodi,jambo hili linaweza likasahaulika na mwisho wa siku tukaambiwa ilishindikana kukata kodi kiinua mgongo cha Raisi kwasababu katiba haikubadilishwa na wakati huo hata Bunge linaweza kuwa limeshavunjwa.
Na inawezekana wamesema makusudi ili mwisho wa siku waitumie katiba kutokukata kodi inayosemwa..
 
Kifungu hiki kinataamka: "Mshahara na malipo mengine yote ya Raisi havitapunguzwa wakati Raisi anapokuwa bado ameshika madaraka yake kwa mujibu wa Katiba hii."

Hicho ni kifungu cha Katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 kinachoongelea Mashariti ya Kazi ya Raisi.

Hofu yangu hapa ni kuwa baada ya kuambiwa sasa Raisi atalipa kodi,jambo hili linaweza likasahaulika na mwisho wa siku tukaambiwa ilishindikana kukata kodi kiinua mgongo cha Raisi kwasababu katiba haikubadilishwa na wakati huo hata Bunge linaweza kuwa limeshavunjwa.

Je,hili haliwezekani kutokea?

Kwanini uamuzi huu wa Bunge wa kukata kodi kiinua mgongo cha Raisi usiende sambamba na kubadili sasa kifungu hiki cha Katiba?
"Mshahara na malipo mengine yote ya Raisi havitapunguzwa wakati Raisi anapokuwa bado ameshika madaraka yake kwa mujibu wa Katiba hii." Kiinua mgongo kinalipwa wakati Raisi ameisha staafu. Hivyo kifungu hicho hakitahusika wakati huo.
 
Wabunge wamepigwa changa la macho. Watakao katwa mafao ni wabunge tuu
 
"Mshahara na malipo mengine yote ya Raisi havitapunguzwa wakati Raisi anapokuwa bado ameshika madaraka yake kwa mujibu wa Katiba hii." Kiinua mgongo kinalipwa wakati Raisi ameisha staafu. Hivyo kifungu hicho hakitahusika wakati huo.
Una uhakika mpaka siku Raisi Mteule anaapishwa anakuwa bado hajalipwa?Una uhakika malipo ya wakubwa hawa yanachelewa kama ya kwetu?Una uhakika mchakato wa kumlipa Raisi kiinuua mgongo unaanza baada ya Raisi kustaafu?
 
  • Thanks
Reactions: R.B
: "Mshahara na malipo mengine yote ya Raisi havitapunguzwa wakati Raisi anapokuwa bado ameshika madaraka yake kwa mujibu wa Katiba hii."

sasa hapa nadhani ni kuchanganya madesa,kwani kiinua mgongo si analipwa akishastaafu,wakati hayupo kwenye uongozi sasa hicho kifungu kinamhusu vipi hadi asikatwe kodi??
 
Una uhakika mpaka siku Raisi Mteule anaapishwa anakuwa bado hajalipwa?Una uhakika malipo ya wakubwa hawa yanachelewa kama ya kwetu?Una uhakika mchakato wa kumlipa Raisi kiinuua mgongo unaanza baada ya Raisi kustaafu?
sheria gani inaonyesha kiinua mgongo kwa rais anaweza kulipwa hata kama hajastaafu??
 
Una uhakika mpaka siku Raisi Mteule anaapishwa anakuwa bado hajalipwa?Una uhakika malipo ya wakubwa hawa yanachelewa kama ya kwetu?Una uhakika mchakato wa kumlipa Raisi kiinuua mgongo unaanza baada ya Raisi kustaafu?
Aise mpaka sasa siamini kwa nini upinzani wamekosa hoja na wanabadili magoli tu...nyie viumbe hamna shukrani...kila siku mnaamka na vioja vya kijinga tu........Ngoja muisome namba vizuri tutaheshimiana tu
 
Hilo mbona linaeleweka walikua wanatafuta Kiki kwa sisi wananchi..ndomana baadhi ya wabunge walitishwa ambao hawaafiki bajeti hiyo wajitoe uanachama sasa uoga+kukosa kisaidia tumbo ikabidi waliridhie kishingo upande tu
 
: "Mshahara na malipo mengine yote ya Raisi havitapunguzwa wakati Raisi anapokuwa bado ameshika madaraka yake kwa mujibu wa Katiba hii."

sasa hapa nadhani ni kuchanganya madesa,kwani kiinua mgongo si analipwa akishastaafu,wakati hayupo kwenye uongozi sasa hicho kifungu kinamhusu vipi hadi asikatwe kodi??
Ingekuwa ni bora kama Katiba ikataamka moja kwa moja kuwa Raisi atakatwa kodi ya kiinua mgongo maana mchakato wa kumlipa Raisi kiinua mgongo sidhani kama huwa unaanza baada ya Raisi kustaafu.
 
Hilo mbona linaeleweka walikua wanatafuta Kiki kwa sisi wananchi..ndomana baadhi ya wabunge walitishwa ambao hawaafiki bajeti hiyo wajitoe uanachama sasa uoga+kukosa kisaidia tumbo ikabidi waliridhie kishingo upande tu
ni lini wabunge wa ccm walishawahi ipinga bajeti ya serikali yao hadi leo useme walikuwa na uoga na kuridhia kishingo upande??hivi hii bajeti unahisi ni mbovu kuliko zile zilizopita??
 
Ingekuwa ni bora kama Katiba ikataamka moja kwa moja kuwa Raisi atakatwa kodi ya kiinua mgongo maana mchakato wa kumlipa Raisi kiinua mgongo sidhani kama huwa unaanza baada ya Raisi kustaafu.
tatizo hapa nahisi unachanganya "lini analipwa" na "mchakato wa kumlipa" ni vitu viwili tofauti,kuanza kwa mchakato mapema hakumaanishi ndio ameanza kulipwa mapema hapana,tunaangalia lini atastaafu........
 
Kifungu hiki kinataamka: "Mshahara na malipo mengine yote ya Raisi havitapunguzwa wakati Raisi anapokuwa bado ameshika madaraka yake kwa mujibu wa Katiba hii."

Hicho ni kifungu cha Katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 kinachoongelea Mashariti ya Kazi ya Raisi.

Kwa ufahamu wangu, Raisi anahesabika kuwa bado yupo madarakani mpaka pale mrithi wake (Raisi Mteule) atakapokuwa amekula kiapo cha kushika madaraka ya uraisi.

Hofu yangu hapa ni kuwa baada ya kuambiwa sasa Raisi atalipa kodi,jambo hili linaweza likasahaulika na mwisho wa siku tukaambiwa ilishindikana kukata kodi kiinua mgongo cha Raisi kwasababu katiba haikubadilishwa na wakati huo hata Bunge linaweza kuwa limeshavunjwa.

Je,hili haliwezekani kutokea?

Kwanini uamuzi huu wa Bunge wa kukata kodi kiinua mgongo cha Raisi usiende sambamba na kubadili sasa kifungu hiki cha Katiba?
Salary Slip wewe sio Mbunge umeweza kuliona hilo lakini wale wabunge wa ccm zaidi ya 200 hakuna aliyeliona zaidi ya kushangilia na kujipongeza kwa makofi.
Hii maana yake nini? Ni kwanba hakuna faida ya uwepo wao pale kwani hawana tofauti na viti tuu. Na wanakuja hapa wabunge kama Juliana Shonza kujisifu umakini wakati jambo kama hilo hata hawalijui wanadanganywa kama watoto wa primary
 
ni lini wabunge wa ccm walishawahi ipinga bajeti ya serikali yao hadi leo useme walikuwa na uoga na kuridhia kishingo upande??hivi hii bajeti unahisi ni mbovu kuliko zile zilizopita??

Jaribu kuona nje ya box siyo ndani tu ndo utanielewa nimemaanisha nini? Mfano mzuri Ghasia yule amekubali kwa manufaa ya chama lakini mwili unakataa,vilevile kwa bajeti yoyote ili iwe nzuri lazima ipate challenge siyo unaipitisha kwa karibia 100% zote wakati kuna sehemu kibao zina utata.
Pili hi bajeti si mbovu kama zilizopita ila ina mapungufu yake
 
Salary Slip wewe sio Mbunge umeweza kuliona hilo lakini wale wabunge wa ccm zaidi ya 200 hakuna aliyeliona zaidi ya kushangilia na kujipongeza kwa makofi.
Hii maana yake nini? Ni kwanba hakuna faida ya uwepo wao pale kwani hawana tofauti na viti tuu. Na wanakuja hapa wabunge kama Juliana Shonza kujisifu umakini wakati jambo kama hilo hata hawalijui wanadanganywa kama watoto wa primary
hao wabunge wako wa ukawa hata walipokuwa nje hawakuliona hilo walikuwa wanang'ang'ania wote wakatwe kodi ikiwemo na rais sasa wewe unayewaponda wa ccm na kuwaacha wa ukawa naanza kupata shida...................
 
Back
Top Bottom