Itangazwe Rasmi Clouds Fm ni Radio ya Taifa

Itangazwe Rasmi Clouds Fm ni Radio ya Taifa

Chanel zenyewe zinaonyesha low quality kupitiliza, sauti mbovu kuliko hasa TBC2. vipindi vyake vingi vinaendeshwa kisiasa zaidi unadhani kwa sasa ndicho wananchi wanataka? Wengi wameelewa hilo na ndio maana utaona hata hao serikali wanakimbilia kwa private media zinazoendeshwa kiushindani hasa ktk zama hizi za digital
 
Watakuwa wanaangalia coverage wengi upenda kuangalia habari nyepesi,udaku,bongo flavor, shilawadu nk.
 
Kama uliangalia msimu wa fiesta, wakuu wa mikoa na wilaya walivyoichukulia fiesta kama tukio la kitaifa la kiserikali, Rais na viongozi wa kitaifa wanavyotembelea na kutoa taarifa kupitia clouds tv na redio, SIO KITU KIBAYA, ila tunaiua TBC kama shirika la utangazaji la kitaifa, ingekua vzur kama TBC ingepewa kipaumbele, kua ni chanzo cha taarifa mama na matamko ya kitaifa, inapoelekea watendaji hawatotoa taarifa TBC na kupeleka vyombo vya habari binafsi, TBC watachukua kutoka vyombo vngne vya habari....
TBC wajitathmini,



TBC wanajiua wenyewe kwa kukosa ubunifu!wamebweteka eti kwa sababu ni chombo cha umma basi watapeta, pale kuna uongozi bomu haijawahi kutokea! Mtu fulani pale eti kwa kuwa na phd (parmanent head damage) ya
kuungaunga basi anajiona Mungu mtu; kila kitu oh mimi nina phd! Haambiliki, hashauriki, watumishi hofu tupu! tbc ndio yafa hivyo labda hiyo phd iondolewe pale, ukiongea na staff wa tbc utasikitika utakayoyasikia kuhusu uongozi huo wa phd!!
 
SIKUMBUKI MARA YA MWISHO KUTAZAMA WALA KUSIKILIZA TBC,1,2 >Taifa<fm
 
Khaaaa .....nimeshtuka kucikia neno TBC hvi hii terevishen ya ubaguzi inasifia vitu ambavyo vya chama kimoja IPO daa mi nikikuta wanaangalia TBC kwanza naenda kuangalia comedy.....
 
If I am wrong you can correct me.

Nashangaa kuona hii sinema ya viongozi wa serikali badala ya kuhutubia kupitia TBC wanaenda clouds hii ina maanisha nini? au wameshajua kuwa TBC haina tena watazamaji? ni nani wa kulaumiwa kwa TBC kukosa watamaji?
 
TBC kama mdomo wa serikali imekosa ushawishi katika tasnia ya vyombo vya habari,licha ya umri na experience curve kubwa.Nashangaa chombo kinachokuwa funded na serikali,at the same time conduct normal business kinazidiwa na ITV inayojiendesha bila kupewa sapoti ya serikali.

Mambo kama haya Nape ndo alipaswa kuyashughulikia.Sio kuwakingia kifua wakina wema kwa minajiri ya kupata publicity tu.

Kuhusu clouds media.Hii ni organizesheni inayokuwa remoted na top security agency ya nchi yetu.JK alishawahi kutonya kwamba chombo hichi ndio chombo chenye ushawishi mpana katika utangazaji,kwa muktadha huo wanapaswa kukitumia kuseti agenda za serikali,aliyasema haya baada ya kufurahishwa na kampeni zinazoendeshwa na taasisi hii,kuwa zinawashika na kuwahamasisha watu kwa muda mfupi.Yani impact ni kubwa.

Kumbuka;yote haya huwa organized in exchange kwa clouds media kupata some privileges.Walinufaika sana wakati wa JK and I think they still command the same at the moment.
 
Ukilichoka land cruiser v8 basi tumia land cruiser Tx Prado .
Naona tibisi wengi wameichoka kuitzama haswa youth sasa wameona kituo kitakacho wasilisha interest zao ni Mawingu TV inaonyesha dhairi ndo chaneli inayofuata kuang aliwa na vjna ambao ndo wahusika wakuu wa nchi , japo kuwa zamani ilikuwa Nyota Tv
 
mm huwa najiuliza redio zingine zinajisiaje? wangekuwa wanafanya hayo tbc wala tusinge shangaa ila kupendelea radio moja binafsi huwa sielewi
Wanatafta radio ambayo inaskilizwa na watu wengi ili waweze kuskika. TBC taifa huwa inaskilizwa na kutazamwa na wachache sana hasa wazee.
 
Kila ukifungua TBC Taifa unasikia SHAMBA LA KILIMO NALIENDELE .....kilimo cha mihogo......
 
Back
Top Bottom