Itakuwaje Bunge likikataa kuthibitisha Serikali kuhamia Dodoma?

KAWETELE

JF-Expert Member
Dec 11, 2015
681
1,611
salaamu wana JF

1469598008214-jpg.371697


Serikali ya awamu ya tano chini ya Mtukufu Rais, imedhamiria kuhamia dodoma kutimiza ndoto ya muasisi wa taifa hili. ni jambo jema ingawa limekuja ghafla mno kiasi wachambuzi wa mambo wanahoji uharaka wa jambo nyeti kama hilo.

Ikumbukwe kwamba suala la kuhamia dodoma haikuwa hata miongoni mwa top 3 mwa vipaumbele vya serikali, pengine serikali imejiridhisha baada ya kuona viwanda na elimu vimefanikiwa sasa serikali imejikita kuhamia dodoma.

Maswali ninayojiuliza hapa.
Tayari watumishi wamelazimishwa kuhama, na imetangazwa yale majumba ya serikali yanayotazamana na bahari yatapigwa minada, na watakao kataa kuhama watakuwa wamejifukuza.,

1. Je, iwapo bunge litakataa kupitisha hiyo sheria, itawalazimu Serikali kurudi dar? gharama zote hizo nani atafidia?

2. Na kama serikali ina uhakika wabunge watapitisha, haioni kuwa serikali ipo juu ya Bunge, na zile lawama za serikali kuwa mmliki wa bunge hasa baada ya naibu spika wa bunge kuteuliwa na mkuu wa serikali aje agombee ili aje aisimamie serikali hiyo hiyo, zitakuwa zinajidhihirisha wazi wazi?

3. Mbona tukiwa shule tunaambiwa makao makuu ya nchi ni Dodoma, je mitaala ilikuwa inapingana na sheria?

Tafadhari naomba kufahamishwa hasa kisheria kwa wenye uelewa wa hili.
 
Tatizo bunge halina meno tena, limeshageuzwa kuwa moja ya taasisi za serikali.
Mimi binafsi sina imani tena na bunge hili la sasa. Ni dhahiri kuwa MAGU analimiliki kwa asilimia 97.
Hivyo chochote anachotaka kipitishwe na bunge kitapita tu!
 
Kesi ya ngedere unampelekea nyani halafu unategemea ushinde? Bunge litapitisha tu.Ila naona kizaazaa cha bajeti ya kuhamia huko. ["Sikilizia muziki wake sasa"(in Gwajima's voice)].
 
salaamu wana JF

1469598008214-jpg.371697


Serikali ya awamu ya tano chini ya Mtukufu Rais, imedhamiria kuhamia dodoma kutimiza ndoto ya muasisi wa taifa hili. ni jambo jema ingawa limekuja ghafla mno kiasi wachambuzi wa mambo wanahoji uharaka wa jambo nyeti kama hilo.

Ikumbukwe kwamba suala la kuhamia dodoma haikuwa hata miongoni mwa top 3 mwa vipaumbele vya serikali, pengine serikali imejiridhisha baada ya kuona viwanda na elimu vimefanikiwa sasa serikali imejikita kuhamia dodoma.

Maswali ninayojiuliza hapa.
Tayari watumishi wamelazimishwa kuhama, na imetangazwa yale majumba ya serikali yanayotazamana na bahari yatapigwa minada, na watakao kataa kuhama watakuwa wamejifukuza.,

1. Je, iwapo bunge litakataa kupitisha hiyo sheria, itawalazimu Serikali kurudi dar? gharama zote hizo nani atafidia?

2. Na kama serikali ina uhakika wabunge watapitisha, haioni kuwa serikali ipo juu ya Bunge, na zile lawama za serikali kuwa mmliki wa bunge hasa baada ya naibu spika wa bunge kuteuliwa na mkuu wa serikali aje agombee ili aje aisimamie serikali hiyo hiyo, zitakuwa zinajidhihirisha wazi wazi?

3. Mbona tukiwa shule tunaambiwa makao makuu ya nchi ni Dodoma, je mitaala ilikuwa inapingana na sheria?

Tafadhari naomba kufahamishwa hasa kisheria kwa wenye uelewa wa hili.
Hawana jeuri hiyo. Wale wazee wa ndiiooo!!!? Sahau kabisa
 
Back
Top Bottom