Kutoka 6:1-8
1.Basi Yehova akamwambia Musa: “Sasa utaona mambo nitakayomtendea Farao.
+ Mkono wenye nguvu utamlazimisha awaruhusu watu wangu waende zao, na mkono wenye nguvu utamlazimisha awafukuze kutoka katika nchi yake.”
+
2 Kisha Mungu akamwambia Musa: “Mimi ni Yehova.
3 Nami nilikuwa nikimtokea Abrahamu, Isaka, na Yakobo kama Mungu Mweza-Yote,
+ lakini kwa jina langu Yehova
+ sikujitambulisha kwao.
+ 4 Pia, nilifanya agano pamoja nao kwamba nitawapa nchi ya Kanaani, nchi ambamo waliishi kama wageni.
+ 5 Sasa mimi mwenyewe nimesikia kilio cha uchungu cha Waisraeli, ambao Wamisri wanawatumikisha kama watumwa, nami ninakumbuka agano langu.
+
6 “Kwa hiyo, waambie Waisraeli: ‘Mimi ni Yehova, nami nitawatoa kutoka chini ya mizigo ya Wamisri na kuwaokoa kutoka katika utumwa wao,
+ nami nitawakomboa kwa mkono ulionyooshwa
* na kwa hukumu kubwa.
+ 7 Nami nitawachukua muwe watu wangu, nami nitakuwa Mungu wenu,
+ nanyi hakika mtajua kwamba mimi ni Yehova Mungu wenu anayewatoa kutoka chini ya mizigo ya Misri.
8 Nami nitawapeleka katika nchi niliyoapa
*kwamba nitampa Abrahamu, Isaka, na Yakobo; nitawapa ninyi iwe miliki yenu.
+ Mimi ni Yehova.’”
+