Israel imeangukia pua mgogoro na Wapalestina, wamepoteza mengi na pakubwa

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,626
46,270
Bila kwenda mbali kuhusu Historia ya mgogoro na vita inayoendelea sasa kati ya Israel na Hamas ukanda wa Gaza ni wazi Utawala wa Netanyahu umekosea pakubwa kimkakati katika hii vita.

Kuanzisha vita mara nyingi huwa ni jambo rahisi sana ila kuimaliza na kutimiza malengo huwa jambo gumu sana na la kutoa jasho kila sehemu. Ni mara chache sana vita huwa zinaenda jinsi mikakati na malengo yalivyopangwa.

Baada ya ugaidi wa September 11 US walienda kwa pupa katika vita vya Afghanistan na Iraq. Kilichotokea ni kwamba utawala wa Taliban ulianguka ndani ya miezi miwili ya uvamizi ila US wakaendelea na vita visivyoisha kwa miaka 20 na matumizi ya zaidi ya Dola Trillion 2 wakitumia kila siku ya vita hiyo $million 300. Hatimaye US wakaondoka Taliban wakatoka milimani na kwenye mapango wakaingia Kabul na sasa wanaendelea kuitawala Afghanistan.

Mfano mwingine wa karibuni kabisa ni jinsi Urusi waliivamia Ukraine wakijua watafanya Operation ya wiki moja Kyiv ianguke waweke kibaraka wao, sasa kwa miaka miwili bado wanaendelea na vita visivyoisha huku majirani zake wakizidi kujiunga NATO, huku ni hesabu kwenda mrama kabisa.

Israel nayo imeingizwa kingi kwa Hamas. Ni kweli kitendo cha Hamas kuvamia na kuua raia 2000 upande wa Israel kisingeweza kuvumilika bila kujali kiini cha huo mgogoro wa muda mrefu, ila Israel kuingia Gaza na kuua raia mara kumi zaidi(20,000) nacho hakiwezi kuvumiliwa hata na washirika wake.

Matokeo yake sasa ni kwamba Israel imewaweka katika hali ngumu washirika wake wa magharibi. Japo West hawakubaliani kabisa na Hamas pia hawakubaliani na jinsi Israel inavyoendesha vita hiyo japo hawasemi kwa sauti kubwa. Baadhi ya maseneta na wanaharakati wa US wanapinga kabisa nchi yao kuendelea kupia Israel silaha, wanasiasa wengi wa Ulaya wenye ushawashi wanapinga pia jinsi hali ya vita Gaza inavyoendelea.

Israel japo ni kama wanakaribia kuisawazisha kabisa Gaza kwa mabomu bado inaonekana vita haitaisha na suluhu haitapatikana kwa muda mrefu sana kwa sababu kwa kuanzia wenyewe hata hawana mpango wowote kabisa wa maana wa jinsi ya kudilia na Wagaza zaidi ya milioni 2 baada vita hii. Ile huruma waliyopewa na sehemu kubwa ya dunia baada ya uvamizi wa Hamas inaishilia na mahusiano yao na Waarabu yaliyokuwa yameanza kuwa mazuri sana kuna uwezekano mkubwa yakaharibika kabisa kwa sasa.

Vita mara nyingi ni kama kuingia katika kichaka cha miba ya michongoma, unaweza kuwa unajichomoa upande mwingine kumbe upende mwingine unajiingiza, kutoka huwa sio rahisi sana.
 
Yani hao Wa Israel huwa siwaelewi,unaambiwa toka miaka na miaka chochote kinachofanyika Palestina Israel ndio wana control mpaka chakula.Eneo lenyewe ni dogo but hao mateka toka wachukuliwe na HAMAS hawajawahi kupatikana,sasa unajiuliza upi umahili wa hilo jesho la Israel??
 
Yani hao Wa Israel huwa siwaelewi,unaambiwa toka miaka na miaka chochote kinachofanyika Palestina Israel ndio wana control mpaka chakula.Eneo lenyewe ni dogo but hao mateka toka wachukuliwe na HAMAS hawajawahi kupatikana,sasa unajiuliza upi umahili wa hilo jesho la Israel??
Kama wangekuwa wanapigana na jeshi rasmi basi labda tungeweza kuona umahiri wao kama ilivyokuwa katika six days war, ila Hamas sio jeshi rasmi. Pia hata hao mateka unaweza kukuta ni propaganda za pande zote mbili tu
 
Kwanza Israel hahitaji huruma kutoka kwa yeyote maana anajua tangu kuumbwa kwa Dunia yeye anapitia chuki tu. Rejea mauaji ya Wayahudi zaidi ya milion 5 kule German.

PILI Israel yeye anataka hata leo hao wa palestina wafutike kabisa ili yeye ajitawale. Na inavyoonekana huu mgogoro umemfurahisha sana Israel maana baada ya hapa Hamas hawatakaa ajitawale tena pale Gaza.

Tatu, Marekani pale ilipo inafurahia sana maana kwenye vita kama hizi ndipo biashara na uchumi wake unakua sana kwa mauzo ya silaha. Hao wanasiasa unaosema hawapendezwi na vita ya Gaza ndio ambao sasa hivi wanamshinikiza Biden kuipiga Iran kutoka na shambulio la drone lililouwa wanajeshi 3 wa USA kule Jordan.

Dunia ina unafiki mwingi sana.

Ona matrilion anayopata USA kutokana na hizi vita
Screenshot_20240130-090939_Telegram.jpg
 
Bila kwenda mbali kuhusu Historia ya mgogoro na vita inayoendelea sasa kati ya Israel na Hamas ukanda wa Gaza ni wazi Utawala wa Netanyahu umekosea pakubwa kimkakati katika hii vita.

Kuanzisha vita mara nyingi huwa ni jambo rahisi sana ila kuimaliza na kutimiza malengo huwa jambo gumu sana na la kutoa jasho kila sehemu. Ni mara chache sana vita huwa zinaenda jinsi mikakati na malengo yalivyopangwa.

Baada ya ugaidi wa September 11 US walienda kwa pupa katika vita vya Afghanistan na Iraq. Kilichotokea ni kwamba utawala wa Taliban ulianguka ndani ya miezi miwili ya uvamizi ila US wakaendelea na vita visivyoisha kwa miaka 20 na matumizi ya zaidi ya Dola Trillion 2 wakitumia kila siku ya vita hiyo $million 300. Hatimaye US wakaondoka Taliban wakatoka milimani na kwenye mapango wakaingia Kabul na sasa wanaendelea kuitawala Afghanistan.

Mfano mwingine wa karibuni kabisa ni jinsi Urusi waliivamia Ukraine wakijua watafanya Operation ya wiki moja Kyiv ianguke waweke kibaraka wao, sasa kwa miaka miwili bado wanaendelea na vita visivyoisha huku majirani zake wakizidi kujiunga NATO, huku ni hesabu kwenda mrama kabisa.

Israel nayo imeingizwa kingi kwa Hamas. Ni kweli kitendo cha Hamas kuvamia na kuua raia 2000 upande wa Israel kisingeweza kuvumilika bila kujali kiini cha huo mgogoro wa muda mrefu, ila Israel kuingia Gaza na kuua raia mara kumi zaidi(20,000) nacho hakiwezi kuvumiliwa hata na washirika wake.

Matokeo yake sasa ni kwamba Israel imewaweka katika hali ngumu washirika wake wa magharibi. Japo West hawakubaliani kabisa na Hamas pia hawakubaliani na jinsi Israel inavyoendesha vita hiyo japo hawasemi kwa sauti kubwa. Baadhi ya maseneta na wanaharakati wa US wanapinga kabisa nchi yao kuendelea kupia Israel silaha, wanasiasa wengi wa Ulaya wenye ushawashi wanapinga pia jinsi hali ya vita Gaza inavyoendelea.

Israel japo ni kama wanakaribia kuisawazisha kabisa Gaza kwa mabomu bado inaonekana vita haitaisha na suluhu haitapatikana kwa muda mrefu sana kwa sababu kwa kuanzia wenyewe hata hawana mpango wowote kabisa wa maana wa jinsi ya kudilia na Wagaza zaidi ya milioni 2 baada vita hii. Ile huruma waliyopewa na sehemu kubwa ya dunia baada ya uvamizi wa Hamas inaishilia na mahusiano yao na Waarabu yaliyokuwa yameanza kuwa mazuri sana kuna uwezekano mkubwa yakaharibika kabisa kwa sasa.

Vita mara nyingi ni kama kuingia katika kichaka cha miba ya michongoma, unaweza kuwa unajichomoa upande mwingine kumbe upende mwingine unajiingiza, kutoka huwa sio rahisi sana.
Kwani Israel ikipata au kupoteza we Mrugaruga unafaidika na kipi hususani maisha yako binafsi?

Ubinadamu ni kazi/Humanity is a work.

Sent from my CPH2387 using JamiiForums mobile app
 
Kwanza Israel hahitaji huruma kutoka kwa yeyote maana anajua tangu kuumbwa kwa Dunia yeye anapitia chuki tu. Rejea mauaji ya Wayahudi zaidi ya milion 5 kule German.

PILI Israel yeye anataka hata leo hao wa palestina wafutike kabisa ili yeye ajitawale. Na inavyoonekana huu mgogoro umemfurahisha sana Israel maana baada ya hapa Hamas hawatakaa ajitawale tena pale Gaza.

Tatu, Marekani pale ilipo inafurahia sana maana kwenye vita kama hizi ndipo biashara na uchumi wake unakua sana kwa mauzo ya silaha. Hao wanasiasa unaosema hawapendezwi na vita ya Gaza ndio ambao sasa hivi wanamshinikiza Biden kuipiga Iran kutoka na shambulio la drone lililouwa wanajeshi 3 wa USA kule Jordan.

Dunia ina unafiki mwingi sana.

Ona matrilion anayopata USA kutokana na hizi vitaView attachment 2888080
Gaza kuitawala ni ngumu kwasababu ya ideology ya axis of resistence.
Huwezi itawala Gaza kamwe.
Maana huwezi ifuta Hamas kamwe .
Wanaoshadadia hii vita ni viongozi,ila uliwasikia raia wanavyopingana na hii vita wakishika mabango yasemayo "STOP WAR,WAR HAS NO WINNER BUT MUTUAL DISTRUCTION"?
Israel imeripotiwa kushuka kwa asilimia ya kasi ya ukuaji wa kiuchumi na kuwa na tatizo la kifedha kwasababu vita hii imekula bajeti kubwa ya nchi.
 
Gaza kuitawala ni ngumu kwasababu ya ideology ya axis of resistence.
Huwezi itawala Gaza kamwe.
Maana huwezi ifuta Hamas kamwe .
Wanaoshadadia hii vita ni viongozi,ila uliwasikia raia wanavyopingana na hii vita wakishika mabango yasemayo "STOP WAR,WAR HAS NO WINNER BUT MUTUAL DISTRUCTION"?
Israel imeripotiwa kushuka kwa asilimia ya kasi ya ukuaji wa kiuchumi na kuwa na tatizo la kifedha kwasababu vita hii imekula bajeti kubwa ya nchi.
Serikali zenye kiburi ndo huanguka kwa namna hiyo .. watu watakapo kosa ugali ndo wataanza kuelewa kwa sasa mambo hayajatight sana subiri kidogo ikfika mahali no importation ,exportation
 
Kama wangekuwa wanapigana na jeshi rasmi basi labda tungeweza kuona umahiri wao kama ilivyokuwa katika six days war, ila Hamas sio jeshi rasmi. Pia hata hao mateka unaweza kukuta ni propaganda za pande zote mbili tu
Vita yote aliyopigana Israel dhidi ya waarabu palikua na USA na UK nyuma yake,Nasir akisema kila tukisonga tunakutana na majeshi ya USA, misri ilipigwa mkwara ikaacha Vita,Syria naye aliyekua kamuweka kwenye Kona Israel akaacha,maana asingeweza peke yake,Hamas ingekua na tanks,anti air missiles hiyo nchi ingekua ishagawanyika nusu Israel nusu Palestine,hao machoko Vita hawawezi, Taliban hakuwa milimani,walikua wakipigana daily,labda Kama hukuwa ukifuatilia,rais kibaraka alikimbia vibaya mno wakati Taliban wanakaribia kuibeba Kandahar,na kule kuondoka haraka haraka watu kujazana airport ni dalili maji yalikua ya shingo, Soviet waliondoka hivyohivyo Afghanistan baada ya Vita vya zaidi ya muongo mmoja
 
Serikali zenye kiburi ndo huanguka kwa namna hiyo .. watu watakapo kosa ugali ndo wataanza kuelewa kwa sasa mambo hayajatight sana subiri kidogo ikfika mahali no importation ,exportation
Kaka yasha tight sanaa.
Walipiga tathmini wanauchumi deni la Israel linakimbilia kumeza asilimia kubwa ya GDP yake.
Kinachowaokoa jamaa USA na UK watafanya cha kufanya kumpatia debt relief.
Yani km kuishi ISRAEL inatumia akiba sasa.
Ndio maana hata askari waliwarudisha kupunguza bajeti pesa za uendeshaji vita zimekua haba.
 
Jeshi lisilo rasmi hutumia ugaidi na human shield.
Kwa hiyo hao human shield ni chuma zikipigwa risasi hawafi si ndio,, hizi ni propaganda zinazoenezwa na Israel na mashost zake ili ahalalishe kuua watoto,, kwa maana Hamas hata kama hawavai military gear lakini si wanaonekana wakiwa wamebeba rpg, smg.. Kinachosababisha mpaka waende wakaue watu hospital ni nini..
 
Yani hao Wa Israel huwa siwaelewi,unaambiwa toka miaka na miaka chochote kinachofanyika Palestina Israel ndio wana control mpaka chakula.Eneo lenyewe ni dogo but hao mateka toka wachukuliwe na HAMAS hawajawahi kupatikana,sasa unajiuliza upi umahili wa hilo jesho la Israel??

Hamas = Israel (wazayuni)
 
Kaka yasha tight sanaa.
Walipiga tathmini wanauchumi deni la Israel linakimbilia kumeza asilimia kubwa ya GDP yake.
Kinachowaokoa jamaa USA na UK watafanya cha kufanya kumpatia debt relief.
Yani km kuishi ISRAEL inatumia akiba sasa.
Ndio maana hata askari waliwarudisha kupunguza bajeti pesa za uendeshaji vita zimekua haba.
Walijua vita itachukua 4 week wa resume kwenye shuguli za kawaida kumbe wapi
 
Kwahiyo Israel kapigwa ila bado kashtakiwa kwa kufanya genocide? It doesn't up.
 
Yani hao Wa Israel huwa siwaelewi,unaambiwa toka miaka na miaka chochote kinachofanyika Palestina Israel ndio wana control mpaka chakula.Eneo lenyewe ni dogo but hao mateka toka wachukuliwe na HAMAS hawajawahi kupatikana,sasa unajiuliza upi umahili wa hilo jesho la Israel??
Usipoelewa ujue uwezo wako, ndio ulipoishia apo. Akili ya mwafrika haiwezi kulingana na akili ya myahudi
 
Back
Top Bottom