Is Lowassa again?

Mie nashangaa! sioni tatizo hapa, jee tatizo ni nini? ni Hemed kumuona Lowasa? au Lowasa kuwaandikia psrc? na nnadhani Lowasa ameweka wazi kabisa kuwa sheria zifuatwe. Bado nnashangaa tatizo ni nini?

Sidhani kwa wale wanaosema kuwa awamu hii itaimaliza nchi walikuwepo wakati awamu ya kwanza inang'atuka, kwa kuwakumbusha tuu, hakuna awamu iliiwaacha nchi hii kavu na kwenye umaskini mkubwa kama awamu ya kwanza, awamu ya msifiwa nyerere.

NYERERE alivyong'atuka, benki kuu iliwashwa moto na kaikubakishwa hata dola moja ya kufutia machozi, Jee mnakumbuka? NYERERE alivyong'atuka,tulikuwa hata mafuta ya kwenye gari hatuna kwa kuwa tulikuwa hatuna fedha za nje za kununulia, kumbuka mzee ruksa alivyochukuwa nchi aliwaita wazee wa dar pale diamond akawaelezea kuhusu hili na ikambidi atumie mbinu za haraka za kwenda kuomba libya na imf na iran na kwingineko (hotuba ya mikuki miwili, mzee ruksa diamond.

Yaani hatukumbuki tulivyokuwa tunapangishwa foleni za unga, mchele, sukari, sabuni,viwembe, viberiti. KWA KIFUPI HATA WEMBE WA KUNYOLEA ilIkuwa hakuna BILA FOLENI

Nadhani wengi mnaoandika humu kusemasema hovyo, kama hii mada ya Lowasa, hata sijui tatizo nini? Nadhani wakati wa nyerere mlikuwa hampo au kwa waliokuwepo na wanachangia habari hizi zisizo na mantiki, basi ni wafupi wa kumbukumbu.

Sasa jamani mbona yeye (nyerere) hatumsemi alivyotuwacha pabaya kiuchumi! tunamsifu tuu?

Hebu waacheni hawa kina lowasa na kikwete wafanye vitu vyao, JEE, kwa ukweli wenu kabisa hamuoni kazi wanayoifanya? au ni chuki tuu za kibinafsi?

Kaangalie neno chuki binafsi kwenye kamusi ya kiswahili lina maana gani kabla ya kuja kukurupuka hapa.
 
Sasa kama Waziri Mkuu ambaye amekuwa mbunge kwa miaka nenda rudi na mwenye forum kubwa anapitwa na kijana mdogo toka Kigoma kwenye mawazo ya watu; sidhani hiyo ni chuki binafsi. Ningekuwa mimi Lowassa ningekaa chini na kujiuliza "what am I doing wrong"
 
michukp5b25dby9.jpg


Credit Michuzi blog
 
whatever it is,sioni any foul play hapo aliyofanya Lowassa,na sioni sehemu amabayo EL ameshinikiza hiyo bei amabayo ndio issue hapa,mbona mnamlaumu EL wakati tatizo mnajua liko wapi? kwa kweli kwa mwendo huu tunarudi kule kule kwenye spin ambazo hazina maana yeyote...EL hajashinikiza mtu yeyote hapo ni sawa awa na kuwaambia hao PSRC fanyeni kazi yenu acheni kusumbua watu mana ukweli kiwanja kilikuwa kinauzwa ila PSRC nao walikuwa wanataka kuvuta chao(sio siri tunajua rushwa iko vipi)
 
Koba, hivi unajua maana ya kuingiliwa madaraka? Haya ndiyo yaliyotaka kumfanya Rashid ajiuzulu. Umewapa watu majukumu waamini kuwa watatekeleza wakishindwa unawatimua. Sasa kuwaingilia na kuwapa shinikizo vya nini?
 
mara ngapi tunaenda sehemu tunasumbuliwa tunaamua kwenda mbele kwa wakubwa zao ili kusaidiwa?hata US ambapo naamini rushwa iko chini sana lakini mara ngapi tunasema let me talk to your manager/supervisor tena EL kasema waziwazi msaidieni katika sheria na taratibu zilizopo...sioni rushwa wala kuingiliwa mtu kazi yake na kaambiwa tuu fanya kazi yako.
 
Bwana Koba Ahsante...naongeza

Ukiritimba huwa unawafuata Wakiritimba! EL hana kosa lolote alilolifanya aliona kuna ukiritimba ndio sababu akashinikiza...sasa kama alikiuka taratibu yeyote basi wote PRSC na EL walikiuka na wasemwe kwa pamoja...!
Huku kutapatapa kwa kuongelea viongozi tu, kila unakoenda kwenye midahalo lazima mtu atajwe ndio watu kukurupuka na kuanza kutapatapa...ebo!
 
wengi wenu ni spin master na mko driven na sababu zenu za kutomkubali huyu jamaa(mimi pia sioni kama ni PM mzuri) lakini kwenye hii issue specific sioni kibaya alichofanya
 
Eeeeh, Halisi; hujawahi kucharuka hivyo, kuna nini ndugu yangu!

Baadhi ya watu wanataka tukubali maovu yanayotendeka leo katika serikali hii, kwa sababu tu hatujipangi foleni kununua nyembe za kunyolea n.k.

Ukitafakari kidogo 'logic' ya mawazo haya utatambua kuwa bei yetu ni ndogo mno.
 
wengi wenu ni spin master na mko driven na sababu zenu za kutomkubali huyu jamaa(mimi pia sioni kama ni PM mzuri) lakini kwenye hii issue specific sioni kibaya alichofanya

Kama posting ya 'Halisi' hapo juu bado haikufanyi uweze kudadisi, basi hakuna sababu inayoweza kukufanya utilie mashaka ya dili zima.
 
ndio yale yale badala ya kudeal na tatizo linalohusika,mnaanza kuleta na visivyohusika,oooh rushwa hapo EL kavuta mara ooohh kaingilia watu kazi...nimeona watu wameandikiwa barua na US Senator kuwasaidia kupata visa itakuwa EL kumwandikia investor asaidiwe ambaye anatulipa kodi,acheni hizo ila kama kuna rushwa hapo mseme ni ipi
 
Kama posting ya 'Halisi' hapo juu bado haikufanyi uweze kudadisi, basi hakuna sababu inayoweza kukufanya utilie mashaka ya dili zima.

...hakuna cha kudadisi hapo,rushwa wala kuingiliwa kazi mtu mnatakia tuu kuifanya big deal
 
...hakuna cha kudadisi hapo,rushwa wala kuingiliwa kazi mtu mnatakia tuu kuifanya big deal

It is a big deal kwa sababu anakiuka taratibu za kazi. Besides, from billion madafu to mamillion madafu, why? Kuna haki ya kudadisi.
And why so much finality in statement ...... 'hakuna cha kudadisi hapo, rushwa wala kuingiliwa kazi mtu'...... Hiyo barua sio kuingilia kazi?
 
nakushauri uwaulize PSRC kwanini waliuza hicho kiwanja kwa bei ya kutupa karibu na bure?
 
but how do measure the success of TAKUKURU?is it the number of investigations and arrests they make or their successful convictions of walarushwa?
by the way mimi namuona Hosea kama a really qualified msanii kweli,anavyoongea na watu na jinsi anavyoshughulika rushwa nabaki kumwomba Mungu tu...nasikia anasema kuwa hawamuwezi Mkapa kwa vila Katiba inamlinda;so the question is;yeye Hosea ni lawyer by profession,hivi alichofanya Hitler kipindi kile au Makaburu dhidi ya weusi huko "Bondeni" ambapo Kaitba husika ziliyabariki...was that RIGHT,LAWFUL & FAIR?...to come to the point,je kwa kukiri kuwa Mkapa ana kinga ya kikatiba hivyo hawamuwezi,does that mean Hosea anakubaliana na watz kuwa kulikuwa na matumizi ya ovyo kabisa ya madaraka na ofisi wakati Mkapa alipokuwa Rais na kuwa ni kinga tu ndo inawazuia kumchunguza?...jamani my head is spinning faster na nahisi kuzimia!!!!

Kama hawezi kumchunguza Mkapa kwa sababu ya katibu YONA je?
 
Back
Top Bottom